Mrejesho wa mwezi mmoja baada ya kuacha kazi

nimefikia hapa
IMG_20180918_091022.jpg
IMG_20180918_091016.jpg
IMG_20180916_082202.jpg
IMG_20180916_082155.jpg
IMG_20180916_082209.jpg
 
Kuacha kazi ili ujiajili unahitaji uwe na akili maalumu, watu wana Mahindi yanaozea ndani hayana soko, nimeshuhudia Songea mwaka Jana mamia ya heka za mbaazi Wakulima wamegoma kuvuna, sababu gharama za kuvuna ni kubwa kuliko bei ya mbaazi.

Kuna Dada yangu aliacha kazi eti anaenda kulima matikiti, kilio alichonacho sasa....

Tuwe tunafuatilia siasa kidogo, wengine alipoingia tu Mtukufu kwa kauli zake za mwanzo tuliona ana mtazamo mbaya na secta binafsi, na ndio kinachotokea.
 
Hongera sana kwa ujasiri na hatua uliyochukua. Kuna baadhi ya kazi za kuajiriwa ni kama utumwa flani hivi huku return yake ikiwa ndogo. Wengine hawana ujasiri wa kujitoa kwa kuwa hawana uhakika wa kusurvive bila kale kazawadi kanakotolewa kila mwisho wa mwezi japokuwa hakakidhi haja
 
Safi, ukimaliza mwaka mmoja pia usisahau kutupa mrejesho wa maendeleo yako.
 
Ref my previous post

Namshukuru mwenyezi Mungu muumba wq mbingu na ardhi kwa pumzi na afya njema aliyonijaalia

ilinichukua miaka mitano na nusu kuacha kazi ya serikalini nashukuru Mungu kwa walionisupport juu ya uamuzi wangu huo

nliwakwepa wale wote ambao nlihic watanikatisha tamaa hasa wazazi wangu ilibidi nimtengenezee mazingira ya kutokuniomba hela ya kila mwezi kwa kumwekea pooltable linalomwingizia 150000 kila mwezi

Ninachofanya baada ya kuacha kazi

Ninalima matikiti maji,Zukini na pilipili za kuwasha nimeanza na tikiti maji heka 3 pilipili za kuwasha nusu heka na zukini nusu heka

Zukini na pilipili ndo zao ninalolitegemea kulifanya liwe zao la biashara nimelilima chache kwasababu ckuwahi kulima zukini na pilipili so natafuta experience

tikiti ziko poa ntawaonyesha picha za zilipofikia

Biashara

nimefanya biashara ya mbolea ya mavi ya kuku kwa muda wa week 2 nimeingiza faida ya laki4 though changamoto imekuja kwenye savings kila nkipata hela mahitaji ya shamba yanaongezeka mf dawa mbolea ya dukani kuwalipa posho vibarua nk

Uzuri wa kujiajiri

unaamua ufanye nini muda gani mwenyewe yaani kama nkiamua nisafiri hata nw naweka mipango sawa naenda popote inshort nipo huru

changamoto kuubwa nliyoiona

Savings na mifuko ya jamii

faida inapaswa ihifadhiwe kiac kikubwa kuliko kukitumia mara nyngi tunatumia hela pale tunapokua nazo tusipokua nazo ni ngumu sana kuzitumia natamani nijifunze mbinu ya kisave

natamani nijiunge na ule mfuko binafsi wa penshen tatizo huku Jaribu(kibiti) hakuna hicho kitu

View attachment 848013View attachment 848015View attachment 848016

Sent using Jamii Forums mobile app
ZUKINI NI NINI WANA JF?
 
nalilima Tz ni Lushoto ila nimejaribu kwanza robo heka likikubalindo ntakua nalima hili tu coz linakomaa kwa siku 50 unavuna mara4/5 halina comptition sokoni! wadudu hawaliathiri sana
 
nalilima Tz ni Lushoto ila nimejaribu kwanza robo heka likikubalindo ntakua nalima hili tu coz linakomaa kwa siku 50 unavuna mara4/5 halina comptition sokoni! wadudu hawaliathiri sana
Soko lake lipoje na utauzia wapi
 
kisutu nna namba ya dalali wa hilo zukini Ila nasikia Zenj ndo wana nunua bei nzuri hadi 2500 /kg
 
40 Reactions
Reply
Back
Top Bottom