MREJESHO; Wa Kaka yangu aliyechanganyikiwa

MREJESHO; Wa Kaka yangu aliyechanganyikiwa

kiss ov love

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2025
Posts
9,363
Reaction score
16,092
Guys, yule kaka yangu niliyewaambia alipatwa na ukichaa kwa mara ya pili baada ya kukabidhiwa pikipiki mpya, sasa tulihangaika na tiba kwa mtaalamu.

Kwasasa ana nafuu kubwa kabisa japokuwa bado hajatulia kuna muda anakuwa anahisi kama watu wanaokuja kumuona wanataka kumfanyia vitu vibaya ila yote kwa yote ni jambo la kumshukuru Mungu kwani alivyo mwanzo na sasa hivi ni tofauti kabisa.

Sasa wakuu huyo mtaalamu kuna mambo alikuwa anayasema ni mazito sasa sijui kama ni kweli au lah! Hadi nabaki nachanganyikiwa.

Hii hapo chini ni picha ya hirizi tuliyoikuta nyumbani siku ya kwanza mtaalamu alivyokuja kuanza tiba ya kaka yangu.
 

Attachments

  • 20250506_000646.jpg
    20250506_000646.jpg
    359.4 KB · Views: 22
Huyo mganga atawapiga hela na kuwagombanisha ukooo na ndugu zenu mpaka mchoke wenyewe.

Utasikia shangazi yake kamroga, ama mama mkubwa ndie kamroga, ama ndugu fulani kamroga

Note : huyo mganga hatawaomba hela cash atawapiga hela kupitia vifaa na dawa, atawaelekeza maduka ya kununua dawa ambayo kuna matapeli wenzake.
 
Babes poleni, vipi mtaalamu alisema mambo mazito gani?

View attachment 3336096
Asante sana, la kwanza alilosema ni kwamba mtu anayefanya hivyo kwa ndugu yangu ni mtu katika familia na majirani na kingine ni kwamba hao watu wapo katika chama Chao hivyo kuna sadaka mwezi wa 6 na wa 12 kama wameshindwa kwa kaka yangu wanaweza wakanitoa mimi sadaka maana mimi ndiye mtoto wa kike wa mwisho na ndiye last born😪
 
Asante sana, la kwanza alilosema ni kwamba mtu anayefanya hivyo kwa ndugu yangu ni mtu katika familia na majirani na kingine ni kwamba hao watu wapo katika chama Chao hivyo kuna sadaka mwezi wa 6 na wa 12 kama wameshindwa kwa kaka yangu wanaweza wakanitoa mimi sadaka maana mimi ndiye mtoto wa kike wa mwisho na ndiye last born😪
WHAAAAT?
Duuh mambo ya waswahili ni hatari sana, poleni jamani.

Kwahiyo wewe unafanyaje sasa ili kuepuka kutolewa sadaka?
 
Asante sana, la kwanza alilosema ni kwamba mtu anayefanya hivyo kwa ndugu yangu ni mtu katika familia na majirani na kingine ni kwamba hao watu wapo katika chama Chao hivyo kuna sadaka mwezi wa 6 na wa 12 kama wameshindwa kwa kaka yangu wanaweza wakanitoa mimi sadaka maana mimi ndiye mtoto wa kike wa mwisho na ndiye last born😪
Pole sana Binti 😢
 
Back
Top Bottom