Mrejesho: Nimevunja uchumba wa watu

Mrejesho: Nimevunja uchumba wa watu

Heisenberg

JF-Expert Member
Joined
Apr 26, 2017
Posts
1,688
Reaction score
2,982
Habari za leo wakuu, Poleni na majukumu pia hongereni kwa kusheherekea vyema Sikukuu ya EID, japo kwangu haikuwa njema sana kutokana na shida nilizopitia.

Juzi nilikuja na Uzi nikiomba msaada nifanye nini juu ya majanga yaliyonikuta
Rejea:-

Leo nimeona Nilete mrejesho wa nini kimefanyika juu ya hili tukio.

Kikao cha Familia ya binti kimekaa leo Saa 4 asubuhi juu ya shauri la jamaa kudai mahari yake.

Watu wenye busara wamekaa na kuongea na kijana kuwa arudishe Moyo na waendelee na Process zao za uchumba kuelekea Ndoa.

Lakini kijana Amekuwa na Roho ngumu ssna kiasi cha kuto kusamehe. Hii ni kwasababu ameniona mara nyingi kwenye simu ya Mchumba wake na amesha muonya mara nyingi lakini binti amekuwa kiziwi, hivyo basi jamaa hawezi kuendelea na huo uchumba hivyo arudishiwe Mahari yake ajue nini cha kufanya.

Pia akaomba kama familia haina uwezo kwa wakati huo watoe chochote Tu hata elfu 10, ili mradi mahari imerudishwa.

Icho kikao mara kikageuga msiba watu karibia wote wakawa wanalia kwa kinachoenda kutokea.

Binti akaitwa kwenye kikao. Nae akawa analia. Akaulizwa kama anampenda jamaa, akasema anampenda sana kwani jamaa hakumpa muda wa kumsikiliza laa sivyo wangeyamaliza. Pia binti akaomba msamaha kwa kuiingiza familia kwenye matatizo.

Jamaa amepigiwa Magoti na mama yake na mama wa binti, ndio amekubali kuendelea na uchumba.

Mida ya saa 8 nimepigiwa simu na Deligation ya kikao nimepewa Onyo kubwa sana juu ya mahusiano yangu na binti. Nimekili sitarudiana naye tena na nimekata mawasiliano naye..

Nikaomba pia niongee na jamaa, nikaongea nae nimemuomba msamaha yeye kama mwanaume mwenzangu. Na jamaa amenisamehe kwa moyo mkunjufu kabisa.

Leo ndio nimeamini kuwa nimeachachana na huyu binti. Roho imeniuma sana maana yeye ndio mwanamke wa Ndoto yangu

Najiona kama nimeanza upya maisha bila huyu binti. Japo sikuwa na nafasi nae sana lakini nilikuwa nina amani.

Napenda kuwashukuru Nyote kwa michango yenu hadi kufikia kulimaliza Suala hili.
 
Ulisema kikao jmosi.

Wewe, mrembo na mchumba mnakaa mkoa tofauti na kwao binti.

Mchumba Kakukuta kwa mrembo saa 4 usiku kachukua tu vitu vyake kasepa na kusema neno halafu kasepa.

Mwendo wa masaa manne.

Jamaa kaenda kuomba kurudushiwa mahari Juzi leo tena yupo kwenye kikao.

Halafu kakusamehe na wewe kwa moyo mkunjufu. Na una ujasiri wa kupokea simu zao bila kuogopa.

Hii chai
 
Ushaharibu
Ulisema kikao jmosi.
Wewe, mrembo na mchumba mnakaa mkoa tofauti na kwao binti.
Mchumba Kakukuta kwa mrembo saa 4 usiku kachukua tu vitu vyake kasepa na kusema neno halafu kasepa.
Mwendo wa masaa manne.
Jamaa kaenda kuomba kurudushiwa mahari Juzi leo tena yupo kwenye kikao.
Halafu kakusamehe na wewe kwa moyo mkunjufu. Na una ujasiri wa kupokea simu zao bila kuogopa.
Hii chai
 
Ulisema kikao jmosi.
Wewe, mrembo na mchumba mnakaa mkoa tofauti na kwao binti.
Mchumba Kakukuta kwa mrembo saa 4 usiku kachukua tu vitu vyake kasepa na kusema neno halafu kasepa.
Mwendo wa masaa manne.
Jamaa kaenda kuomba kurudushiwa mahari Juzi leo tena yupo kwenye kikao.
Halafu kakusamehe na wewe kwa moyo mkunjufu. Na una ujasiri wa kupokea simu zao bila kuogopa.
Hii chai
Mimi kitambo nilijua hii ni chai ndo maana nikaulizia taarifa ya stars, angalia komenti ya pili ya uzi huu!!
 
Ndio kuna uzi uko humu jf akikanyaga tu kwa mafarao mikono inakusanywa Karia wetu na karia wa cape verde.
Nasikia kuna jamaa karipoti hapa kuwa nae ana tuhuma hivyo akitua tu Misri anadakwa kama Ahmad
 
Huyo jamaa mwenye mchumba ana roho ngumu aisee....

Hivi unapata Wapi ujasiri wa kuendelea na ndoa na huyo Kahaba?

Kunguru ni kunguru tu.. Huyo mwanamke anatendelea kutoombwa hata ndani ya ndoa.

Namsikitikia sana jamaa aliyemsamehe na kukubali kumuoa huyo malaya.
 
Back
Top Bottom