Mr. Kuku Farm ni aina mpya ya DESI?

Mr. Kuku Farm ni aina mpya ya DESI?

Kuna jamaa wanaitwa Mr Kuku Farms, wanasema wanafanya ufugaji wa kuku na wanahkmiza watu kuwekeza kwa ahadi kwamba unavuna mara 2.

Nimeona wamepost na shuhuda mbalimbali motomoto kama zile za kwa mwamposa. Mmoja anasema aliwekeza sh laki 3.5 na anategemea kuvuna 8M.

Swali nalo jiuliza kwanini iwe rahisi kupata fedha kiasi hiki kwa muda mfupi kuliko bank yeyote au soko la hisa?

Napata wasiwasi isije kuwa ni DESI imerudi kiani maana huwezi pata mara 2 kirahisi hivi wakati kuna makampuni yanafuga kuku nanyanapata hasara.

Naomba kwa yeyote anaye jua hawa Mr kukus ni wafugaji kweli wa kuku?

Je, kama kuna mtu amesha fanya nao uwekezaji , atupe ushuhuda wake motomoto?

Je, kwanini kama ni biashara ya uwekezaji wasifanyie soko la hisa DSE?

Serikali ipo wapi kutoa ufafanuzi wa jambo hili walau watu tufuse million kwa myda mfupi.

Kwa wale ambao mnataka kuona shuhuda motomoto tembelea instagram Mr_kukus

Nataka nijitose kwa kuwekeza mil 2 ili zikisha komaa nihune kama mil 80 ndani ya miaka 2.

Sent using Jamii Forums mobile app

Nikweli kabisa watu watalia sana hasa wale wa mwisho wanatoa riba kwa mfumo wa faida ila BOT na vyombo vya Ulinzi vimulike hapa watu watalia sana.
 
Asante sana mkuu.wengine wameishia kunita wakala..kitu kikubwa ambacho nimejifunza watanzania wengi hatusomi na tunapenda kujibu kihisia zaidi.Na kibaya ni kwamba hawataki kufanya study ya ndani zaidi kuhusu jambo jipya.Mfano watu wamekua wakiziponda network marketing sijui utapeli blah blah lakini makampuni yapo na yanaendelea kufanya kazi mengine hana miaka zaidi ya kumi yanafanya kazi.

Na kumbuka pia wakati mfumo mpya kutuma pesa kwa mpesa watu walikua wanapinga sana tena sana wakisema sijui pesa zitaibiwa ni bora nitumie Benki kutuma pesa.

Humu hadi Leo kuna watu wana amini kua kununua vitu online ni utapeli blah blah....

Kwahiyo ukitaka kufanya mamuzi ya kufanya investing au kitu chako ni bora uende uende legitimate sites kufanya research yako ya bidhaa na aina biashara.mfano watu wamekalili kua ukitaka kununua shares lazima tufanye floating of shares on capital markets kama dar es salaam stock exchange lakini wanasahau kua kina venture capital funds...ambazo ni vikundi vya watu ambavyo wana pool funds together na kuinvest kwenye biashara at certain amount of risk.(kama unavyo fahamu kila biashara ina risks zake).

Tanzania Bahat mbaya hatuna venture capital firms kwahiyo unakuta biashara hizi za enterprise zikiwa changa akitaka kupanuka inabidi aje kwa watu...individuals... Ili aweze pata funds za kuikuza biashara iwe kubwa ofcoz akiwa promise investors good returns...

Kwasababu eventually atakuja kustop kupokea individual investments..Maana hapo atakua amefanya projection zake zimekamilika biashara itaanza kuchanganya....

Nimekua nikimfatilia Mr kuku yangu 2017 alipo anza..na alipoalika watu Mara ya kwanza.mabanda yalikua local sana..na future wasn't bright.Lakini kuna watu waliamini ile biashara kua itakua...kwahiyo kina watu waliwekeza pesa kule mabanda yakajengwa etc 2017 Leo hii ndo wanaocheka all the way to the bank na kumbuka wapi waliosema kua pesa zenu zitapigwa sijui blah .sasa hivi mradi ile umekua sana I I think its worth billions..

Nimesema haya sio kwa kumshwishi mtu ila aende akafanye research yake....

Kina huyu jamaa wa south Africa anipango wa kua na ranch za ngombe Africa nzima.na mfumo ni huu huu..ukienda kwenye site take wealthlivestock.com.Yaani anasema unaweza ukawa unafuga ngombe bila kua shamban huku ukiendelea na kazi zako mjini popote duniani.na unawekeza pesa baada ya muda unavuna faida.wao watashugulika na kumkuza kumlisha hadi marketing....

ILA KWASABABU NI KITU KIGENI WATU WATAISHIA KUSEMA NI UTAPELI HAIWEZEKAN UFUGE NGOMBE NA WAKULETE FAIDA MARA DUFU NGOMBE HAO WAKIWA NJE YA INCHI.

Yaani kina disruptive concepts nyingi sana zitakuja ambazo zitabadilisha vitu vingi sana huko mbele kuna watu watachwa nyuma na kuna wengine watasonga mbele...

Sent using Jamii Forums mobile app
Acha kudanganya watu watu wana akili mpaka zinamwagika.. Kuku ni desi mwisho wa siku atakuwa na deni kubwa kuliko asset na mtaji alio nao why? Anatoa riba isio na uhalisia bila kukokotoa matumizi... Hakuna bihashara kubwa ya aina hii usidanganye watu wewe
 
hali iko hivi huko kwa Instagram yao, jamaa hawapokei simu za wateja wao
Screenshot_20200320-081620_GBInsta.jpeg
Screenshot_20200320-081608_GBInsta.jpeg
Screenshot_20200320-081554_GBInsta.jpeg
Screenshot_20200320-081543_GBInsta.jpeg
Screenshot_20200320-081521_GBInsta.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna Jamaa Yangu Leo Kaniambia Kuhusu Hii Biashara Na Kaenda Kuwaona Kabisa Ni Eneo Kubwa Sana Kuku Wanafungwa
Lakini Kufuga Siyo Issue, Yapo Mambo Mengi Sana Yamejaa Ukakasi Kwenye Mradi
 
Kuna Jamaa Yangu Leo Kaniambia Kuhusu Hii Biashara Na Kaenda Kuwaona Kabisa Ni Eneo Kubwa Sana Kuku Wanafungwa
Lakini Kufuga Siyo Issue, Yapo Mambo Mengi Sana Yamejaa Ukakasi Kwenye Mradi
 
Back
Top Bottom