Mponda: Nitajiuzulu kuepusha vifo na si shinikizo la madaktari!

Waziri wa Afya Dr Haji Mponda amesema yeye atajiuzulu ili kuokoa roho za watanzania ambao wataathirika na mgomo mpya wa madaktari na si kwa shinikizo! Hayo aliyasema jana usiku kwenye kikao cha dharura cha baraza la mawaziri cha kujadili mgomo mpya wa Madaktari na Manesi! Hata hivyo Mponda ametoa rai kwamba watanzania wawe makini sana na jinsi watu wanavyotumia migogoro kwa maslahi yao binafsi huku wakisababisha maafa makubwa kwa raia wasio na hatia. Na kusema kuwa kama wana taaruma wakiingia kwenye ushabiki wa siasa nchi itaingia kwenye mgogoro mkubwa na kudhoofisha ustawi wa taifa letu!

Nadhani mponda amesahau kuwa kujiudhuru hakuna rangi, kwamba akijudhuru hivi inakuwa vile, akaijiudhuru vile inakuwa hivi. Sisi tunachotaka yeye ajiuzuru yaani aachie kiti cha uwaziri, kama alikuwa anataka kujiudhuru kwa sababu ya kuepusha vifo si angekuwa ameshajiudhuru???kwani hakuna wagonjwa waliokufa kutokana na mgomo wa mwanzo???
 
JK Anaweza kumkatalia Kujiuzulu, lakini baada ya Mponda aje Pinda, na Baadaye JK.
Tumechoka Wajameni, Rais yupo kama hayupo!! Kwani alilazimishwa kugombea? Si aligombea akiwa anajua kuwa ataweza, na ana majibu ya Matatizo ya Watanzania!!! Matokeo yake ana matatizo kuliko majibu.

Naoana muelekeo ni huko! Lakini tofauti yetu na Misri ama Libya ni kwamba baada ya miaka mitano huwa tunatoka majiani kupiga kura na tuna nafasi ya kuondoana kwa kutumia sanduku la kura.
 
natamani na wanajeshi wagome ili waziri wa ulinzi nae ajiuzulu, mabomu yameua watu mno pasipo sababu
 
anaogopa nini kusema kuwa kazi imemshinda?
hakuna cha kusema eti kunusuru maisha ya wananchi hapo.
KWANI HAO MADAKTARI SI WANANCHI?? MBONA HAWATENDEWI HAKI???
ukweli ni kwamba SERIKALI IMESHINDWA KAZI..................
WALIPE WANACHODAIWA KAZI ZIFANYIKE.
 
Nani agome ili NGELEJA nae ajiuzulu?maana naona nae kagoma kuachia ngazi
Siku zake naye zinahesabika, akiachia huyu ndio utakuwa utaratibu wa kuwabwaga viongoz wababaishaji mana Rais hawez kuwamwaga maswahiba wake.
 
Waziri wa Afya Dr Haji Mponda amesema yeye atajiuzulu ili kuokoa roho za watanzania ambao wataathirika na mgomo mpya wa madaktari na si kwa shinikizo! Hayo aliyasema jana usiku kwenye kikao cha dharura cha baraza la mawaziri cha kujadili mgomo mpya wa Madaktari na Manesi! Hata hivyo Mponda ametoa rai kwamba watanzania wawe makini sana na jinsi watu wanavyotumia migogoro kwa maslahi yao binafsi huku wakisababisha maafa makubwa kwa raia wasio na hatia. Na kusema kuwa kama wana taaruma wakiingia kwenye ushabiki wa siasa nchi itaingia kwenye mgogoro mkubwa na kudhoofisha ustawi wa taifa letu![/QUOTE]

Kilikuwa ni kwa siri na hii ni taarifa iliyovuja au?? Na kwa nini unapoona mawingu ya mvua usianze kuchukua tahadhari mpaka inyeshe ndiyo utavute mwavuli..??
Ninadhani hii serikali ya best yangu JK ina laana ileeeeeeeeeee...Sawasawa na kula nyama ya mtu..utaendelea tu..watu hawana uchungu kabisaaaa na taifa lao.
Kulewa madaraka ni janga la taifa...
 
hivi bora nini sasa!!ni heri watz 20000 wafe kwa ajili ya vichwa viwili tuuuu!au na raia tuandamane kuitoa serikali hii madarakani!!!?kwanini!! kwakua imeshindwa kazi!huyo wazir ni mteule wa mkuu wa kaya!watu wanakufa jamaa anangangania kupanda ml kilimanjaro! jamani are serious kweli!!?
 
huyu ni Dr wa mambo ya ugavi hivi kwa nini JK hakumpeleka pale BOHARI KUU awe ana deal na distribyusheni ya maboksi ya mavitabu ya kiada na ziada...
 
Waziri wa Afya Dr Haji Mponda amesema yeye atajiuzulu ili kuokoa roho za watanzania ambao wataathirika na mgomo mpya wa madaktari na si kwa shinikizo! Hayo aliyasema jana usiku kwenye kikao cha dharura cha baraza la mawaziri cha kujadili mgomo mpya wa Madaktari na Manesi! Hata hivyo Mponda ametoa rai kwamba watanzania wawe makini sana na jinsi watu wanavyotumia migogoro kwa maslahi yao binafsi huku wakisababisha maafa makubwa kwa raia wasio na hatia. Na kusema kuwa kama wana taaruma wakiingia kwenye ushabiki wa siasa nchi itaingia kwenye mgogoro mkubwa na kudhoofisha ustawi wa taifa letu!

Mponda sema Watanzania tuwe makini na viongozi wa aina yako ambao wao wakotayari wanachi wateseke ilimradi Mshahara wako unaingia tu Unatupotezea Muda hii yote ni sababu ya ubovu wa aliekuteua ''Samaki moja bovu tupa yote bovu hii....''
 
Jf,! Naomba niwaambie ki2, kuna rafiki yangu m1, ni m2 wakaribu sana na dr mponda...baada ya kumuuliza kwanini dr Mponda hataki kujiuzulu wakati wa mgomo ule wa mwanzo, alichonibu, sikutaka kuamini, lakini ndo ukweli wenyewe. Dr Mponda aliandika barua kwenda kwa JK akitaka kujiuzulu, JK alimwambia, (naomba nimnukuu) ukijiuzulu, itaonekana ni kweli serekali inamatatizo, na madr wataonekana wanamadai ya msingi.wakifanikiwa katika hilo inamaana madai mengine inabidi yatekelezwe! Isitoshe,(hapa ndo aliponichefua) watanzania ni wepesi sana wa kusahau, we funika kombe mwanaharamu apite! Mbona Ngeleja na Mkulo hawajiuzulu na wizara zao zinakashfa kibao?...wanajf, Mponda na mama Nkya hakuna wa kujiuzulu hapo.!
 
Kumlinganisha JK na kocha wa Arsenal, Wenger ni kumkashifu kocha wa watu. We unaona JK ana mtu wa kumlinganisha naye? Hata mdogo wangu anayesoma std V, anajua JK ni kilaza.
 
Jf,! Naomba niwaambie ki2, kuna rafiki yangu m1, ni m2 wakaribu sana na dr mponda...baada ya kumuuliza kwanini dr Mponda hataki kujiuzulu wakati wa mgomo ule wa mwanzo, alichonibu, sikutaka kuamini, lakini ndo ukweli wenyewe. Dr Mponda aliandika barua kwenda kwa JK akitaka kujiuzulu, JK alimwambia, (naomba nimnukuu) ukijiuzulu, itaonekana ni kweli serekali inamatatizo, na madr wataonekana wanamadai ya msingi.wakifanikiwa katika hilo inamaana madai mengine inabidi yatekelezwe! Isitoshe,(hapa ndo aliponichefua) watanzania ni wepesi sana wa kusahau, we funika kombe mwanaharamu apite! Mbona Ngeleja na Mkulo hawajiuzulu na wizara zao zinakashfa kibao?...wanajf, Mponda na mama Nkya hakuna wa kujiuzulu hapo.!

Hilo nalo neno mkuu; Unganisha na mapendekezo ya Kamati Teule ya Bunge kwa Serikali kuhusu kashfa ya Richmond na hatua zilizotakiwa kuchukuliwa kwa watu kama Mkuu wa TAKUKURU, Mwanasheria Mkuu wa Serikali wakati huo na wengineo, nini kilifuatia baada ya mapendekezo hayo na watu hao wako wapi mpaka sasa.
 
Jf,! Naomba niwaambie ki2, kuna rafiki yangu m1, ni m2 wakaribu sana na dr mponda...baada ya kumuuliza kwanini dr Mponda hataki kujiuzulu wakati wa mgomo ule wa mwanzo, alichonibu, sikutaka kuamini, lakini ndo ukweli wenyewe. Dr Mponda aliandika barua kwenda kwa JK akitaka kujiuzulu, JK alimwambia, (naomba nimnukuu) ukijiuzulu, itaonekana ni kweli serekali inamatatizo, na madr wataonekana wanamadai ya msingi.wakifanikiwa katika hilo inamaana madai mengine inabidi yatekelezwe! Isitoshe,(hapa ndo aliponichefua) watanzania ni wepesi sana wa kusahau, we funika kombe mwanaharamu apite! Mbona Ngeleja na Mkulo hawajiuzulu na wizara zao zinakashfa kibao?...wanajf, Mponda na mama Nkya hakuna wa kujiuzulu hapo.!
duh.......kama kweli ipo kazi
 
Kama hujaelewa basi ww hujaenda shule! Kwa walioenda shule sawa sawa basi hapo wanaelewa kwa kupitia kitu kinaitwa "kontekscho miningi"

Hiyo "kontekscho miningi" nimeelewa vizuri sana bila utata, ila hii "taaruma" sijaielewa, ndio nini hiki?
 
Ni bora ajiuzuru, ubunge wenyewe kaupata kwa kuchakachua kura za Prof Mlambiti, asepe kinyake aisee.
 
Nataka kuweka wazi kuwa hili la madaktari ni la msingi,2natoa masaa 12 ajiuzulu.asipofanya ivyo nguvu ya umma itamwonesha kazi
 
Naupongeza uamuzi wa Dk mMponda kujuuzulu ili kuepusha vifo kwa Watanzania wasio na hatia. Hakuna haja ya kung'ang'ania cheo huku ukijua kwa kufanya hivo watu wataangamia
 
Back
Top Bottom