asakuta same
JF-Expert Member
- Mar 1, 2011
- 14,829
- 5,029
Ndugu wana JF,Naomba msaada wenu wa mawazo katika hili.
Mimi ni kijana mwenye miaka 28.Kwa bahati nzuri au mbaya nimekuwa busy sana na shule na sasa nikahic nitafute mwenza wa kuweza kuishi naye.Bidii hizo zikazaa matunda karibu mwaka mmoja uliopita.
Mwezi uliopita akaja kunitembelea na katika kupiga piga story tukajikuta tunaanza mambo yetu (kitandani) japo ni dhambi kabla ya ndoa,kilichonishangaza na kunistua kwa afya yangu ni pale ambapo kale ka kwanza hakakumaliza hata dakika moja,na uume haukusimama tena kwa zaidi ya masaa mawili.Na nilikuwa natokwa na jasho jingi sana.Jamani mnanishaurije jamani.Mara nyingi huwa napata maumivu ya mgongo.
Naomba msilete utani hapa,mnishauri vizuri kama ni dawa za kienyeji au za kizungu au mnamfahamu daktari wa kunitibu tatizo langu mnisaidie kunielekeza.Mpenzi wangu ananipenda nami nampenda sana lakini kasema kama ni hivyo watoto watapatikanaje,ni heri arudiane na mpenzi wake wa zamani maana yeye hakuwa hivyo.
Natanguliza shukrani zangu kwako wewe utakayenipa mawazo ya kunijenga,nilitamani mwishoni mwa mwaka huu twende nyumbani kwao kujitambulisha na mwisho wa siku tufunge ndoa takatifu
hakuna mwanamke wa kuoa hapo ,unajitafutia matatizo wewe mtu.
hiyo ni kwasababu ndiyo mara ya kwanza , kwani std 1 ulikuwa unazijua hesabu za kuzidisha?
jiamini ,na jaribu kurelax to the maximum.