Amalrik TZ
JF-Expert Member
- Aug 9, 2020
- 340
- 300
Rangi ya ngozi yake ni nyeusi, urefu wa kimo tunaendana japo nimemzidi kidogo. Napenda sauti yake anaponiita mpenzi wangu Errick.
Ananishauri sana kuhusu maisha na pale ninapo mshauri kuhusu jambo lolote hulifanyia kazi bila kipangamizi chochote.
Vumi amekuwa faraja kwangu na nimezama kwenye penzi nzito la mtoto huyu wa kigogo mwenye miaka 26.
Mwishoni mwa mwaka jana baada ya wazazi wangu kunishikaza sana nioe nilimpeleka kumtambulisha nyumbani.
Tatizo limekuja pale Bi Mkubwa alipogundua tulikutana naye Baa na anafanya kazi ya kuuza Baa hapa mjini.
Bi Mkubwa hataki kumsikia kabisa na amekwisha mtolea shombo za kutosha na mara nyingine anaweza mtukana hata mbele yangu.
Wadau naombeni ushauri wenu kusema kweli mimi nampenda sana Vumi na natamani sana nimuite mke na awe mama wa watoto wangu.
Binafsi sijaona mapungufu yake kwangu lakini tatizo lipo kwa Bi Mkubwa siku hizi hataki hata afike home.
Ananishauri sana kuhusu maisha na pale ninapo mshauri kuhusu jambo lolote hulifanyia kazi bila kipangamizi chochote.
Vumi amekuwa faraja kwangu na nimezama kwenye penzi nzito la mtoto huyu wa kigogo mwenye miaka 26.
Mwishoni mwa mwaka jana baada ya wazazi wangu kunishikaza sana nioe nilimpeleka kumtambulisha nyumbani.
Tatizo limekuja pale Bi Mkubwa alipogundua tulikutana naye Baa na anafanya kazi ya kuuza Baa hapa mjini.
Bi Mkubwa hataki kumsikia kabisa na amekwisha mtolea shombo za kutosha na mara nyingine anaweza mtukana hata mbele yangu.
Wadau naombeni ushauri wenu kusema kweli mimi nampenda sana Vumi na natamani sana nimuite mke na awe mama wa watoto wangu.
Binafsi sijaona mapungufu yake kwangu lakini tatizo lipo kwa Bi Mkubwa siku hizi hataki hata afike home.