Mpenzi wangu ananitukana sana!

Mpenzi wangu ananitukana sana!

Watu wanasema kirahis tu eti uondoke....
Kama hakupigi usiondoke komaa hapo hapo kwan matusi yanaua ? anza kuyazoea mdogo mdogo ,umemaliza shule tafuta hata ajira ya laki 4 hizi utapata fasta kuliko kusubir za mamilion ....bwana wako akikuona unaenda kazin ataanza kukuheshimu
Hayo matusi ni stress tu + anaona una
umekua mzigo !!!!!
 
Cha msingi rudi home ukaombe msamaha ili uwe free so acha kunyanyasika pasipo ulazma ila usiweke kiburi na jeur kwa wazaz wako
 
Mnaomshauri mwenzenu kuwa aendelee kuvumilia kuyaoga matusi hamuoni yaweza kuwa hatari kwako hapo baadae?
Mnapo sikia balaa limetokea mfano mwanaume amkata mapanga Mpenzi wake huwa haitokeagi gafla tu , ukifuatilia utakuja kugundua kuwa kulikuwa na viashiria vya hatari Kama hayo matusi na visa vingine!
Mwanamke anawaambia ndugu/wazazi wake Juu ya viashiria hivyo lakini wazazi au ndugu wanamwambia vumilia tu!
Sasa likijampata balaa kubwa kutoka Kwa Huyo bwana yasije yakaja majuto na kusema Kwanini asingeondoka Kwa Huyo bwana baada ya kuanza kuona viashiria ?!
 
Kama wewe ndie mhusika na umeweza kuandika kwa ufasaha hata tukakuelewa..... Basi nihitimishe kwa kusema kwamba, sioni neno la kukushauri kwasababu unazo akili timamu
Hahaa
 
Huyo mwanaume atakuwa " mtu wa kufungamana na kampani za walevi " mara nyingi ndii huwa hawana life skills " mazungumzo yao huwa yana jaa natusi matupu " unakuta kinywa kina tamka maneno machafu kama choo cha kilabuni ...

Achana nae haijui thamani yako huyo !"
 
Suluhu ya yote ni moja tu, tafuta kwako kwa kukaa kimyakimya. Hizo dharau zote kajua huna pa kwenda, hivyo anafanya anavyojisikia.

Pia huyo binti hakufai
 
Habarini wapendwa. Nina jambo linaniumiza sana naombeni ushauri. Ninaishi na mwanaume mwaka wa pili sasa unaenda.

Naombeni msinihukumu kwanini naishi bila ndoa, nilipitia changamoto kubwa sn mpaka kufikia kukosa mahali pa kuishi huko nyuma kwahiyo kimbilio likawa kuishi na mpenzi wangu.

Tatizo sikuhizi ananitukana sana matusi ya nguoni. Yaani kosa dogo utasikia we mse*, wewe na mengine makubwa zaidi. Mbaya zaidi wakati mwingine ananitukana mbele za watu yani navumilia mpaka nachoka sasa.

Naombeni ushauri wa mawazo nifanyeje. Plz msinikejeli. Natamani sana kuondoka lakini kwasasa sina pa kwenda, nimemaliza chuo juzi nasubiri angalau nipate neema ya kazi ndo nitaweza kuondoka ila kwasasa nishaurini tu
Tatizo uko naye sababu ya shida ulizonazo, na jamaa ameshajua mawazo yako pengine ndio maana ameshakuchoka
 
We dada kwani ulikuwa barmedi mbona huweki wazi ili tukusaidie?
 
Mimi nakushauri nenda kwa wazazi wako kwani hapo mwanzo ulikuwa si unaishi kwa wazazi wako
 
Back
Top Bottom