Mpenzi wangu ananitukana sana!

Mpenzi wangu ananitukana sana!

Mkuu kama ni graduate ungetaja elimu yako huku kuna ma Ceo,Mameneja,wajasiriamali. Ungeweza kushauriwa na kusaidiwa pia kuliko kuendelea kutumikiswa kingono kisa hifadhi .
naona umemix
 
Pengjne ni jokes tu mkuu kama unakwenu ludi tu pia huenda ndo mlivo zoeana ivo so kua mpole vumilia
 
Habarini wapendwa. Nina jambo linaniumiza sana naombeni ushauri. Ninaishi na mwanaume mwaka wa pili sasa unaenda.

Naombeni msinihukumu kwanini naishi bila ndoa, nilipitia changamoto kubwa sn mpaka kufikia kukosa mahali pa kuishi huko nyuma kwahiyo kimbilio likawa kuishi na mpenzi wangu.

Tatizo sikuhizi ananitukana sana matusi ya nguoni. Yaani kosa dogo utasikia we mse*, wewe na mengine makubwa zaidi. Mbaya zaidi wakati mwingine ananitukana mbele za watu yani navumilia mpaka nachoka sasa.

Naombeni ushauri wa mawazo nifanyeje. Plz msinikejeli. Natamani sana kuondoka lakini kwasasa sina pa kwenda, nimemaliza chuo juzi nasubiri angalau nipate neema ya kazi ndo nitaweza kuondoka ila kwasasa nishaurini tu
Changamoto za maisha zikupeleke kwa bwana halafu akuheshimu? Endelea kusubiri maana kipo unachokitaka kwake, utakipata
 
Ukaishi kwa mwanaume hajakuoa khaaa kwanza usiogope kutukanwa lazima utukanwe ndo akili ikae sawa..
Unajua anakutumia, anakulala , unamuhudumia kama mmeo ili upate pendo kwake sasa heri leo anakutukana atakuletea mwanamke humo.ndani na hutamwambia kitu.
1: akufukuzae hakwambii tookaaaaaaaa.
2: kabla hujakaa naye ulikuwa unaishi kwa nani?
3: ondoka hapo usijizeeshe bure kisa huna pa kuishi.
4: huwezi kosa wazazi wote then ukawa hauna kaka au dada au shangazi au yoyote wa ukooo huo no uongo.
5: usipende kwenda ishi kwa mtu na kumnyenyekea kupita kiasi kisa waogopa kutimuliwa
6: jiongeze my dear age inakimbua hiyo utakosa wa kukuoa kisa mwanaume na yeye hawezi kukuoa huyo anakutumia tu.. yeye kuoa ataoa ila wewe utakuwa unazeeka tu mwili na kila kiungo chakp kitakuwa kizee nani atakaye kubali kuoa mtu kazeeka tayar?
7:.maisha ni kutafuta hata kufagia barabara upate hela yako mwenyewe ujitegemeee msipende kuishi kwa degree mtatesekaa sana, ishi km hujasoma huna elimu uone kama hautasonga mbele.

By kungwi mtoto.
 
"Nsubiri nipate kazi ndo niondoke" ....... Kumbe hata naww umetega ? .

Natania...Anakutukana akiwa katika hali ipi?? Ni chapombe?? .

Huna pa kwenda? ... Ndo kutaka Kuendelea kuishi mjini??.

Sasa basi, ili kuondoa lawama, asije kukulaumu wakat ambao umemuacha sababu unepata kazi, ni vema ufanye maamuzi ya kuondoka katika wakat huu huu ambao Unanyanyaswa na kutukana .

Ukija ondoka sababu umepata kazi, itaonekanaga wee ni mdada usokua na Fadhila wala shukran . Na watu hawataona kua ulikua ukitukanwa.

Yes life ni gumu mno , usione mbwembwe za humu ukazitaman , life ni gumu sana , Rudi kwa wazazi mdada, Wakat huo ukipigana .
Umenena vyema
 
Hayo matokeo ya kujipeleka Kwa mwanaume kwa kulazimisha!
Tena namsifu huyo mwanaume Walau amethubutu kuonesha kuwa hayuko tayari kugandwa kama ruba!
Sifurahii matusi lakini kimsingi hapo huyo jamaa hakupendi kuishi na Wewe , alikuwa anapita tu njia!
 
Achilia mbali hayo matusi yake, nipe kipimo cha upendo wake kwako. unahisi anakupenda?
 
Nikadhani unabaki hapo kulea mtoto kumbe hata mtoto huna? Sifa yenu waha ni uvumilivu sina cha kukushauri coz sion unasubiri nn hapo, huna pa kwenda wewe ni mlemavu?

Njoo nikupeleke kwa mama yangu umsaidie kazi za nyumbani Huduma utapata kama kawa ila nijuavyo watu kama wewe mnajiliza mitandaoni kutafuta huruma MTU akitaka kukupeleka kijijini huwezi kwenda.
Sasa baki hapo unyooshwe.

Ila hii njia ni nzuri wanaume wenye huruma watakuwa walishajaa pm😀
 
Habarini wapendwa. Nina jambo linaniumiza sana naombeni ushauri. Ninaishi na mwanaume mwaka wa pili sasa unaenda.

Naombeni msinihukumu kwanini naishi bila ndoa, nilipitia changamoto kubwa sn mpaka kufikia kukosa mahali pa kuishi huko nyuma kwahiyo kimbilio likawa kuishi na mpenzi wangu.

Tatizo sikuhizi ananitukana sana matusi ya nguoni. Yaani kosa dogo utasikia we mse*, wewe na mengine makubwa zaidi. Mbaya zaidi wakati mwingine ananitukana mbele za watu yani navumilia mpaka nachoka sasa.

Naombeni ushauri wa mawazo nifanyeje. Plz msinikejeli. Natamani sana kuondoka lakini kwasasa sina pa kwenda, nimemaliza chuo juzi nasubiri angalau nipate neema ya kazi ndo nitaweza kuondoka ila kwasasa nishaurini tu
Unashughuli ya kufanya? Tuanzie apo kma huna jitaidi utafute ili uanzee kuishi kwa kujiwekea akiba maana mda c mrefu atakufukuza au atakueshimu anafanya ivyo sababu anahisi ww umekuwa mzigo kwakwe
 
pole bi mdada, ulienda kwake kirahisi sana,na ndiyo hivyo anakuchukulia kirahisi sana. madamu amemaliza shule,kuwa mvumilivu for some times huku ukisubiria chako. matusi hayaunguzi mwili bhana,tangu uzaliwe hadi sasa umetukanwa matusi mangapi hadi uhofu???
 
Back
Top Bottom