CORAL
JF-Expert Member
- Jun 26, 2011
- 2,827
- 1,858
Nimependa michango ya PLL, ZeMarcopolo na Kongosho kuhusu topic hii. Mwanamke anapenda mwanaume anayedhihirisha uanaume wake kwa kuwa mkali kidogo anapokosewa na pia mwenye uwezo wa kuweka kanuni na kuzisimamia na pia kumlinda iinapobidi. Hapo mwanamke anahisi anapendwa na yuko kwenye mikono salama.
Kuwa mpole mno na kushindwa kufanya maamuzi kuna mfanya mwanamke ahisi kama unapwaya na hufai kuwa mwanaume.Hii ni nature na haitegemei kabila wala taifa.
Kinachosemwa hapa sio kupigana makofi ngumi au kuwekana ngeu. Kinachozungumziwa ni kulaumu,kufoka au kuhoji maswali ya kipolisi kwa lugha ya ukali kidogo na ya msisitizo.
Mwanamke anapokukosea ukajifanya kana kwamba hakuna lililotokea anahisi humjali, humpendi na anafedheheka sana.
Kwa mfano fikiria labda ameenda kazini akasahau simu nyumbani na kurudi hadi jioni baada ya kazi. Sasa anamwambia shosti wake "sijui Ben atanifanya nini leo nimesahau simu atachukiaje akipiga simu bila kupokelewa". Labda shosti ataitikia "ama kazi unayo shoga yangu".
Vipi sasa jioni amerudi amakuta missed calls za Ben 8. Kwa kuogopa kumkwaza Ben anampigia jioni na kumpa pole na kazi na kumwambia kuwa anapenda sana amemmiss!. Lakini hamuulizi chochote kwa nini hakupokea simu je bibie atajisikiaje? Kumbuka shosti yake anangoja kwa hamu kesho kazini amwambie jinsi shemeji yake alivyowaka na jinsi bibie alivyompoza hasira. Lakini anaishia kumwambia hakusema lolote hana ishu kabisa! Si shosti atauliza kama shem ni mzima kweli?
Nadhani mfano huu unatosha kueleza ni kwa nini wanawake wanapenda tuwe wakali kiasi na kudhihirisha uamaume wetu. Kuwa mkali na kumfanya aombe msamaha kisha akasamehewa kunamfanya akupende zaidi na zaidi. Mahusiano yaliyopoa bila kulaumiana na kukaripiana mara mojamoja yanakosa msisiko na yanaweza kudidimia na kuisha.Vipi niambie jinsi mnavyopendana zaidi baada ya ugomvi mdogo!!! Pale bibie anavyokukumbusha akivyochanganyikiwa alivyoona jinsi ulivyomkunjia uso! Kisha unampa pole nakumwambia asirudie alichokifanya. Inaleta raha kama nini. Ugomvi unaozungumziwa hapa ni ule wa makosa madogo kama kutopokea/kuchelewa kupokea simu,kutojibu/kuchelewa kujibu sms, kuchelewa/kutotekeleza appointment, kuwa karibu na mtu fulani wa jinsiatofauti kwa nia njema bila kucheat,n.k. Na adhabu sio viboko,ngumi,mkong'oto n.k bali kufoka,kuhoji maswali kwa mkazo,kukunja uso, kitopokea simu,nk.
Kuwa mpole mno na kushindwa kufanya maamuzi kuna mfanya mwanamke ahisi kama unapwaya na hufai kuwa mwanaume.Hii ni nature na haitegemei kabila wala taifa.
Kinachosemwa hapa sio kupigana makofi ngumi au kuwekana ngeu. Kinachozungumziwa ni kulaumu,kufoka au kuhoji maswali ya kipolisi kwa lugha ya ukali kidogo na ya msisitizo.
Mwanamke anapokukosea ukajifanya kana kwamba hakuna lililotokea anahisi humjali, humpendi na anafedheheka sana.
Kwa mfano fikiria labda ameenda kazini akasahau simu nyumbani na kurudi hadi jioni baada ya kazi. Sasa anamwambia shosti wake "sijui Ben atanifanya nini leo nimesahau simu atachukiaje akipiga simu bila kupokelewa". Labda shosti ataitikia "ama kazi unayo shoga yangu".
Vipi sasa jioni amerudi amakuta missed calls za Ben 8. Kwa kuogopa kumkwaza Ben anampigia jioni na kumpa pole na kazi na kumwambia kuwa anapenda sana amemmiss!. Lakini hamuulizi chochote kwa nini hakupokea simu je bibie atajisikiaje? Kumbuka shosti yake anangoja kwa hamu kesho kazini amwambie jinsi shemeji yake alivyowaka na jinsi bibie alivyompoza hasira. Lakini anaishia kumwambia hakusema lolote hana ishu kabisa! Si shosti atauliza kama shem ni mzima kweli?
Nadhani mfano huu unatosha kueleza ni kwa nini wanawake wanapenda tuwe wakali kiasi na kudhihirisha uamaume wetu. Kuwa mkali na kumfanya aombe msamaha kisha akasamehewa kunamfanya akupende zaidi na zaidi. Mahusiano yaliyopoa bila kulaumiana na kukaripiana mara mojamoja yanakosa msisiko na yanaweza kudidimia na kuisha.Vipi niambie jinsi mnavyopendana zaidi baada ya ugomvi mdogo!!! Pale bibie anavyokukumbusha akivyochanganyikiwa alivyoona jinsi ulivyomkunjia uso! Kisha unampa pole nakumwambia asirudie alichokifanya. Inaleta raha kama nini. Ugomvi unaozungumziwa hapa ni ule wa makosa madogo kama kutopokea/kuchelewa kupokea simu,kutojibu/kuchelewa kujibu sms, kuchelewa/kutotekeleza appointment, kuwa karibu na mtu fulani wa jinsiatofauti kwa nia njema bila kucheat,n.k. Na adhabu sio viboko,ngumi,mkong'oto n.k bali kufoka,kuhoji maswali kwa mkazo,kukunja uso, kitopokea simu,nk.