Chantaburi
JF-Expert Member
- Feb 23, 2012
- 749
- 194
WanaJF,
Hivi mtu unapoandika jambo usilojua ukaliandika tu kwa ushabiki huoni kuwa linakushushia hadhi? Kama kweli una nia ya kujua kwanini usiulize kilichojiri?
Nasikitishwa na hali hii ya kufanya mambo kwa ushabiki. Kikao kinachohusika ni kikao cha Kamati Tendaji mbili za wilaya ya Nyamagana na Ilemela. Mimi ndiye niliyeitisha kikao hicho. . Nimeshuhudia yaliyojiri, hakuna swala la makambi ya Mbowe na Slaa. Wala hakuna swala la wenje kutishia mtu ni taarifa iliyopikwa. Mimi nilimtoa kwenye kikao kijanaaliyesimamishwa baada ya mchakato hadi kufikia CC. Akagoma kutoka. Wala hakutishwa alitolewa na vijana.
Dr. Slaa uwe mkweli kwa tukio la Mwanza kwani hata mie nilikuwepo silaha ilitolewa kutokana na purukushani za mjumbe mmoja kung'anga'ania kuingia kwenye kikao kisicho muhusu.