Mpasuko CHADEMA, Nini kifanyike?

Mpasuko CHADEMA, Nini kifanyike?

Hakuna ubishi kwamba chadema ndio chama kikuu cha upinzani angalau kwa sasa nafasi ambayo awali ilikuwa ikishikiliwa na cuf ambao nao waliirithi kutoka kwa NCCR-MAGEUZI ile ya Mrema na Marando ambae kwa sasa yuko chadema huku Mrema yeye akiwa na chama "chake" siku hizi.

Lakini katika hali ya kusikitisha taarifa kutoka chanzo cha kuaminika(mshauri mkuu wa chadema)zinaeleza kwamba ndani ya chedema kuna mpasuka mkubwa kuhusu nani anapswa kuandaliwa kugombea urai kati ya mwenyekiti mbowe na katibu dr slaa.Ama hakika hii si habari njema sana kwa wapenda demokrasia na mabadiliko kiujumla.

Ushauri wangu ili kunusuru hali hii ya mpasuko isizidi kusambaa,Mbowe na slaa wake pembeni,hii itawavunja nguvu wapambe wao,watakuwa hawana tena kinachowatofautisha na pia itwapa muda mzuri mwenyekiti na katibu wake kushiriki mchakato huru wa kuitafutia chadema mgombea akaekidhi matarajio ya chama hicho ambayo siamini kama ni just kuwwa chama kikuu cha upinzani tu.

Mi naanza kuonyesha njia,majina haya sita kati yao anaweza kuipeperusha vyema bendera ya chadema kwenye urais.

1:Kitila Mkumbo(dr)
2:Zitto Kabwe
3:Halima Mdee
4:Abdallah Safari(prof)
5:Godbless Lema
6:Tundu Lisu

Nawasilisha.

Huu sio mpasuko hata kidogo! Ni mawazo tofauti ya wadau wa CDM. Mwishowe atapatiakna mmoja. Ukiona hakuna anayetoa wazo tofauti, hapo kuna walakiniand most probably kuna elements za kukosa demokrasia. Watu lazima watofautiane katika mawazo, ila at the end wanafikia uamuzi wa wengi.
Na hiyo list yako, sidhani kama kunamtu ana ushawishi mkubwa kama Slaa alivyo. Kitila ni nani, watanzania wangapi wanamfahamu jamani!!! na wengine humo katika list yako
 
Unajua hakuna kitu kibaya kama kufanya vitu kutoka ndotoni, huyu bwana mie huwa nasoma tu mada zake huwa sichangii sababu huwa zinakuwa chini juu, ila hapa napenda awe anajipanga kidogo kwa kulazimisha migogoro sehemu yenye amani ni mbaya sana!!!!
 
Aiseee! hapo kwenye red mkuu, tofauti huleta migogoro na mipasuko katika chama vitu ambavyo mwisho wa siku na yaliyoikumba NCCR Mageuzi na wengine.
Mkuu usinikumbushe NCCR Mageuzi, kilichotokea Tanga sitakisahau. Muulizeni Anthony Komu, Joseph Selasini na Mabere Marando.
 
Unajua hakuna kitu kibaya kama kufanya vitu kutoka ndotoni, huyu bwana mie huwa nasoma tu mada zake huwa sichangii sababu huwa zinakuwa chini juu, ila hapa napenda awe anajipanga kidogo kwa kulazimisha migogoro sehemu yenye amani ni mbaya sana!!!!

Hii habari ya Kitila kusema kuhusu mgogoro imejirudia humu; Kitila si aje akanushe ama akubali kwamba aliyasema hayo kwani kuna dhambi gani?
 
Mkuu unaonekana una roho ya kuchangia sana maendeleo ya kushuka kwa utendaji ndani ya CDM,ningekushauri hoja hii ya CCM ipelekwe hukohuko kuliko kutupotezea mda wetu hapa jamvini kwani tuko busy na kunyakua majimbo kwanza...kwani urais wa CDM unakuhusu nini wewe ama unadhani makundi ya ccm ndo makundi ya CDM
 
Hakuna ubishi kwamba chadema ndio chama kikuu cha upinzani angalau kwa sasa nafasi ambayo awali ilikuwa ikishikiliwa na cuf ambao nao waliirithi kutoka kwa NCCR-MAGEUZI ile ya Mrema na Marando ambae kwa sasa yuko chadema huku Mrema yeye akiwa na chama "chake" siku hizi.

Lakini katika hali ya kusikitisha taarifa kutoka chanzo cha kuaminika(mshauri mkuu wa chadema)zinaeleza kwamba ndani ya chedema kuna mpasuka mkubwa kuhusu nani anapswa kuandaliwa kugombea urai kati ya mwenyekiti mbowe na katibu dr slaa.Ama hakika hii si habari njema sana kwa wapenda demokrasia na mabadiliko kiujumla.

Ushauri wangu ili kunusuru hali hii ya mpasuko isizidi kusambaa,Mbowe na slaa wake pembeni,hii itawavunja nguvu wapambe wao,watakuwa hawana tena kinachowatofautisha na pia itwapa muda mzuri mwenyekiti na katibu wake kushiriki mchakato huru wa kuitafutia chadema mgombea akaekidhi matarajio ya chama hicho ambayo siamini kama ni just kuwwa chama kikuu cha upinzani tu.

Mi naanza kuonyesha njia,majina haya sita kati yao anaweza kuipeperusha vyema bendera ya chadema kwenye urais.

1:Kitila Mkumbo(dr)
2:Zitto Kabwe
3:Halima Mdee
4:Abdallah Safari(prof)
5:Godbless Lema
6:Tundu Lisu

Nawasilisha.

....usoni kama mtu vile!
 
Aiseee! hapo kwenye red mkuu, tofauti huleta migogoro na mipasuko katika chama vitu ambavyo mwisho wa siku na yaliyoikumba NCCR Mageuzi na wengine.

Kukubali kutokubaliana, unaelewa hii. Chama kisicho na tofauti ni chama mfu. Ni kwamba mambo yanatakiwa yaishie ndani tena kistaarabu.
 
Jamani, mbona watu hamfanyi critical analysis!! sina ugonvi na Mh. Mbowe wala Mh. Dr. Slaa wote ni wapiganaji lakini kwa lengo la kuleta ushindani na CCM katika nafasi ya urais 2015 na hata kuweza kushinda kwa uchaguzi wa 2015 ni mtu mmoja tu ndani ya CDM ambaye anaweza kuwakosesha usingizi CCM. Lazima tukubali ushindani wa ngazi ya ubunge ni tofauti na ngazi ya urais. Kwa analysis yangu Mh. Dr. Slaa anaweza kusimama kwenye nafasi ya urais 2015 na Mh. Mbowe kwenye nafasi ya ubunge. Na analysis yangu, hata hypothetical skandal zinazoletwa hapa JF kuhusu slaa ni kutaka kuuhadaa uma ili waanza kuondoa imani naye wawe na uhakika wa ushindi. Muwe makini!!
 
Dr. Slaa atagombea urais na MBOWE atakuwa mgombea mwenza yani makamu wa rais au vise vesa, NENDA KAMWAMBIE ALIYEKUTUMA ULETE PROPAGANDA ZA UMBEA mwambie KUWA CHADEMA TUMEJIPANGA HATUVURUGWI NA MANENO YA UZUSHI.
 
Kwenye nyekundu hapo, ni mzigo kwa chama hivi sasa. Wakazi wa Arusha wanajuuuta kumchagua. matukio ya uharibifu yamezidi jijini hapa, Watalii wengi hivi sasa hawaendi tena kuhofia usalama wao na sasa wengi wanakwenga mikoa ya morogoro, kigoma na kwingine. Watu wenye busara zao jijini Arusha tunaona kama tumevuliwa nguo kutokana na watu wote wa jiji hili kuonekana kama ni wahuni tu. Ni zaidi ya mwaka mmoja tangu kumalizika kwa uchaguzi mkuu, lakini muda wote huo Mbunge huyo amekuwa akilumbana tu na Meya wa JIJI bila sababu yoyote ya msingi. Hakuna ambalo vijana wamekwishalipata pamoja na kwamba ndiyo waliompa umaarufu huo.

Usalama wa watalii uko mikononi mwa mbunge na sio polisi na vyombo vingine vya ulinzi na usalama ambapo mbunge wala sio mjumbe tafuta factor nyingine ya kukosekana kwa watalii uko bias kumhukumu Lema bila kumwangalia huyo meya
 
Wewe huna jipya ni wale wale tu,acha CDM isonge mbele,suala la urais litaamuliwa kwa busara kubwa sana muda wake ukifike na siyo kwa kutumia thread yako isiyo na mashiko,
 
Tatizo wana CHADEMA walio wengi bado wanabeza kuwepo kwa mpasuko huo, afadhali wewe KIM KARDASH umekubali ukweli na kutoa mapendekezo yako. Kama ulivyosema, tumezoea kuona vyama vya upinzani vikiibuka na kuzama kila kunapokucha na mifano mizuri ni hiyo uliyoitoa. Tofauti hizo zinazoleta mpasuko zisipo rekebishwa mapema hii CDM nayo itabaki historia kama ilivyokuwa NCCR Mageuzi ya Mrema.

huo mpasuko ni wenu sio wa chama hata muda wa kugombea uraisi bado sana mnajaribu kupiga majungu kabla ya wakati chadema sio nccr ,,,mgombea huwa anachaguliwa na vikao sio majungu ,chadema haija ibuka ghafla cdm inakuwa na bado mtakoma siku zinavyo kwenda ndio wananchi wanaelimika we tizama tu kampeni za sasa jinsi cdm inavyowatesa na kukuza au idadi ya wapiga kura na wabunge inaongezeka kila kukicha subiri uone idadi ya kura za arumeru zitakuwa mara dufu hasa ukizingatia ccmb: cuf kwishney na makada wa ccm kule wameeenda kupiga umbeya tu oooo vincent si wa ukoo wetu ,,,oooo mnasema mkichaguwa cdm hatuleti maendeleo mtafikiri pesa zinatoka ccm kumbe kodi zetu wote uwe nccr cuf kodi wanalipa acha ujinga fikiria vya maana hakuna umeme hakua maji japo tuna mito kibao lakini tunanunua maji toka uganda ruwenzori ,mfumuko wa bei vyote tulio wapa majukumu ya kuongoza nchi wameshindwa kuteleza nini inafanyika au tunaelekea wapi
 
Hii kitu mbona iko hapa muda mrefu mpaka slaa mwenyewe tulikua nae akiichungulia nyie mko wapi,sio siri tena hii,amkeni usingizini,yamewakuta safari hii,tunajaribu kuwasaidia.

We are very much concerned with ccm desitegration, cause the contry is shaked up! majizi yanakwiba usipime!!!!!
 
Back
Top Bottom