Tetesi za uongo
Hizi tetesi zinatuvurugia sana hapa Lumumba, huu mwaka usiogawanyika kwa mbili haufai kabisa.
Hakuna hata unachojua inabidi uhurumiwe tu.
Lowasa atawahenyesha
Wote na wahame tu, CCM wabaki nape,baba riz na rizwenyewe.
Jamaa muhuni kweli anasubiri mafuriko jagwani sijui yataanzia wapi.
Mbona unalia lia, kwani umejipangaje?.. teh teh mi ccm inaruka na kukanyagana
Huko wameishakuja kwa siri Naziri Karamagi, Andrew Chenge na Rostam Azizi na wezi wengine ambao ndio waliochanga Billion 12 zilizotumika kununua nafasi ya urais Chadema.Hao ndio wenye ubia wa urais wa Lowassa, akipata Lowassa wamepata wao.
We lazima utakuwa unafanya kazi chini ya ofisi ya Yericko Nyerere
Mpiganaji mahiri ni yule ambae yuko ndani ambae anatoa siri zote muhimu zinazosaidia kumwangamiza adui bila huruma.
Acha kumuiga Lizaboni kwa kutunga story zisizo na mashiko!
Mpasuko uko huko kwenu kwenye taasisi ya Wachaga. CCM wameshamtosa Yona Baharini na amemezwa na Papa au Nyangumi.
Pia mimi nimejulishwa jana na mmoja wa 'waratibu' wa kampeni ya Lowassa ya kwamba Kingunge atakihama chama mapema, ikiwezekana ndani ya wiki hii, ili kumuunga mkono EL. Tusubiri
Na iwe kweli
Daaaah safari ya matumaini imefika watoke tu kwani Ccm ndio baba hao au mama hao