Mpaka Kieleweke Si Mbowe

Status
Not open for further replies.
Dunia ina mambo na mambo yenyewe si madogo, wakutukanwa wanatukana na wakujua wanajulikana hakuna kulia. New chapter open kwa kuheshimiana bila kujuana.
 
Asha unasema eti mimi nimeanzisha kuwa Mpaka Kieleweke ni Mbowe? Vipi ukitoa ushaidi mkuu ili nikubali kukosolewa,

Ninasubiri ushahidi wa mimi FMES, kuanzisha kuwa Mpaka Kieleweke ni Mbowe, ukiuonyesha mkuu nitakubali kosa, ila kama huna ushahidi naomba useme wazi kuwa huna na ningewaomba Mods wakushughulikie kwenye hili iwapo huna ushahidi na ukiwa nao naomba Mods pia wanishughulikie ipasavyo, maana si unajua mimi ni jina moja hapa na siku zote huwa niko responsible na kila ninalosema, sijawahi kukimbia kivuli changu au maneno yangu!

Otherwise, sisi wote hapa ni watu wazima kama Mpaka Kieleweke sio Mbowe, hivi ni kweli wewe Asha ndiye uliyepaswa kumuongelea? Yaani yule mtu mzima hawezi kusema mwenyewe? Halafu mbona ni wengi hapa JF waliowahi kusingiziwa majina na mimi nikiwa mmoja wapo mbona hukujitokeza kutetea, WHy huyu Mpaka Kieleweke?

Mkuu hivi kweli nia na madhumuni yako on this topic hasa ilikuwa ni nini, kutuambia au kutotuambia? Maana mkuu sio siri kuwa nimeshitushwa mpaka kwenye mifupa knowing aliyeko nyuma ya hili jina la Asha, lakini nasubiri ushahidi mkuu! Ili baadaye nikuonyeshe jinsi Chinga alivyoitwa godoro la muungwana, jinsi Chinga alivyoitwa kifaa cha muungwana, aliponitumia huu ujumbe niliwamuambia kuwa mezea tu kuna siku yatageuka haya!

Dear My esteemed JF members, Tanzania inatutegemea,Dunia inatutegemea kupafanya sehemu salama/amani ya kuishi watu wengi pamoja na mimi NAIMANI SANA NA JF MEMBERS baadhi wako dedicated kwa jamii na WENGINE NDIO WANALETA malumbano ya majina yasio na maana chukua ujumbe fanyia kazi kosoa or add value to it, ndio maana majina ya JF mostly are not real,Haya ya kuanza kulumbana yatapoteza lengo na maana halisi ya JF.
TUBADILIKE JAMANI.
 
Mkuu wangu maneno yako ni mazuri sana tena mazito, ila yamekuja very late kwa sababu the damage has been done kwa watu wengi sana hapa JF na hii tabia, ambayo imekuwepo hapa kwa muda mrefu sana,

Nashangaa leo kwa mara ya kwanza umekuuma sana vipi kwani mkuu? Hivi unajua kuna watu mapka waliacha kuingia hapa kwa kutajwa majina yao? Mbona kwenye kusema jina la Chinga na kazi yake Foreign wakati fulani hapa kuna hata watu wanaoheshimika hapa walishiriki na hukulalamika? Why leo mkuu?

Unajua ninahisi kuwa leo hapa JF kuna jambo, lakini binafsi nimeshitushwa sana na haya ya leo! Msimamo wangu mkuu siku zote uko wazi tena very clear, kuwa anayeanza ni lazima nimjibu na huwa ninatoa tahadhari mapema, kuwa kama huna hoja acha maana ukianza matusi ya nguoni kwa huwa sina tatizo kujibu, kwa sababu baaada ya kulazimishwa sana kuhusu my ID, nikajifunza dawa ni moja tu nayo ni kutafuta ID za wale wanaonichokoza na believe me ninazo, kwenye hilo I have no respect,

kama ni sheria iheshimiwe kwa wote sio akisemwa jina Chinga ni sawa ila akisemwa Kileweke basi iwe tatizo

Halafu FYI msimamo wangu hapa kukataa watu kutajana majina umekuwa wazi kabisa kama umekuwa mfuatiliaji. Nimejitokeza kukemea watu wakijaribu kubashiri nani ni nani! So its not the first time, sijaanzia na mpaka kieleweke. Labda lapekee hapa ni kuwa safari nimefungua thread kabisa kukanusha. Ni kutokana na uzito wa Bwana Mbowe kama Mwenyekiti wa CHADEMA. Ilipokuwa kwa Kitila na wengine nilisema tu katika thread ya mtu aliyezua huo uzushi tu.

As far As I am concerned, message delivered, case closed, I am out on this

Nawakatika mjadila mwema, tujifunze kujadili issues badala ya persons!

Asha
 
ndugu zangu mimi naomba msaada kwenye tuta,kutokana na comments nyingi hapo juu napata impression kwamba Bwana Mbowe is highly reverred humu ndani ya JF,that is fine with me,lakini comments nyingine mbona zinaandikwa kana kwamba JF ni tawi la CHADEMA? do we rebrand this blog to CHADEMAFORUMS? ni kijiswali tu!
 
ndugu zangu mimi naomba msaada kwenye tuta,kutokana na comments nyingi hapo juu napata impression kwamba Bwana Mbowe is highly reverred humu ndani ya JF,that is fine with me,lakini comments nyingine mbona zinaandikwa kana kwamba JF ni tawi la CHADEMA? do we rebrand this blog to CHADEMAFORUMS? ni kijiswali tu!

Inategemea umesimama upande gani wakati umeona hiyo "mbowe is highly revered humu ndani"? Mtu mwingine akisimama upande mwingine anaweza kusema inaonekana yeye "the most targeted politician in JF" kiasi kwamba tunaweza kuiita hii Anti-Mbowe forum. What do you think about that part? So, pinga unachopinga, tetea unachotetea, everything else will be sort out along the way, hapendwi mtu hapa, haogopwi mtu na hapendelewi mtu.. lakini pia haonewi mtu..!
 
Inategemea umesimama upande gani wakati umeona hiyo "mbowe is highly revered humu ndani"? Mtu mwingine akisimama upande mwingine anaweza kusema inaonekana yeye "the most targeted politician in JF" kiasi kwamba tunaweza kuiita hii Anti-Mbowe forum. What do you think about that part? So, pinga unachopinga, tetea unachotetea, everything else will be sort out along the way, hapendwi mtu hapa, haogopwi mtu na hapendelewi mtu.. lakini pia haonewi mtu..!
nimekupata kiongozi,ahsante kwa kuonyesha njia!
 
nani anayetaka kujua nani ni nani? Huu mtindo wa kujaribu kufuatilia hoja baada ya kujua msemaji ni nani unapoteza sana ladha ya hoja. Maana unasoma hoja huku ukiwa na preconceived ideas na prejudice tayari.. kumbe unayemfikiria ndiye kumbe siye!
Hiyo ndiyo mbaya zaidi,ila mie Namfahamu vizuri mpaka kieleweke,ni siyo Mbowe!

Ni mwanaharakati na mwanamageuzi toka anasoma shule
 
Pamoja na kuwa kauli mbiu ya hamasa ya Hakuna Kulala Mpaka Kieleweke ilibuniwa na Mwenyekiti Mbowe wakati wa kampeni, nataka kukanusha hapa kwamba mtu anayejiita Mpaka Kieleweke hapa Si Mbowe. Pamekuwa na jitahida sana za kumhusisha mwenyekiti wetu na Majina mawili hapa mtandanaoni, wakati Chinga alianzisha uzushi kwamba Mbowe ni Philimom Michael, Bwana FMES yeye ameanzisha Mpaka Kieleweke ni Mbowe. Nimekuwa nikifuatilia mienendo na michango ya watu hawa wawili na napenda niweke wazi kwamba hakuna Mbowe kati ya watu hao wawili.

Philemon Michaeil ni mwanahabari ambaye mpaka sasa yuko Dar es salaam.

Mpaka Kieleweke ni kada wa CHADEMA anayezunguka kati ya Dar es salaam na Dodoma.

Hata wakati ambapo mwenyekiti Mbowe akiwa nje ya nchi hawa mabwana wawili wameendelea kutoa michango yao kutoka Dar es salaam. Mathalani kwa sasa Mwenyekiti Mbowe yuko kikazi mashariki ya kati lakini bado mpaka kieleweke anaandikia michango yako toka Dodoma.

Kwa mchambuzi yoyote wa michango ya watu humu atagundua kuwa michango ya Mpaka Kieleweke haiendani kabisa na maoni na misimamo ya Bwana Mbowe katika masuala mbalimbali na kwa ujumla bwana Philemon Michael hana undani wa masuala ya kisiasa hususani yale yanayoihusu CHADEMA.

Nawakatia kheri

Asha

Asha,

Unapoteza bure muda wako kukanusha habari ambayo haipo.

Lengo la JF sio kutafuta nani ni nani lakini pia waswahili wanasema fumbo mfumbie mjinga, mwerevu hung'amua.

Vipi mwenzetu umekuwa PA wa Mpaka Kieleweke?
 
ndugu zangu mimi naomba msaada kwenye tuta,kutokana na comments nyingi hapo juu napata impression kwamba Bwana Mbowe is highly reverred humu ndani ya JF,that is fine with me,lakini comments nyingine mbona zinaandikwa kana kwamba JF ni tawi la CHADEMA? do we rebrand this blog to CHADEMAFORUMS? ni kijiswali tu!

Mmmhhhhh!!! Kama na wewe umeyaona hayo, then No Comments.
 
Inategemea umesimama upande gani wakati umeona hiyo "mbowe is highly revered humu ndani"? Mtu mwingine akisimama upande mwingine anaweza kusema inaonekana yeye "the most targeted politician in JF" kiasi kwamba tunaweza kuiita hii Anti-Mbowe forum. What do you think about that part? So, pinga unachopinga, tetea unachotetea, everything else will be sort out along the way, hapendwi mtu hapa, haogopwi mtu na hapendelewi mtu.. lakini pia haonewi mtu..!

MJJ,
Revered by wanaCHADEMA is an understatement, he is godly to them. Lakini eti he is the most targeted, that is a joke. How about JK, Lowassa, RA, Pinda, Chenge etc.?? This is a proMbowe Forum and not the other way round.
 
Kujaribu kutafuta nani ni nani katika ukumbi huu ni sawa na kujaribu kufanya utafiti wa kisayansi kuhusu vumbi liliowekwa kwenye viti vya wabunge. Naomba tuendelee kukwaruzana kwa njia ya nukta tu bila kupoteza nguvu kutafuta ni nani analeta hizo nukta. Unajua mkishaanza kufahamiana sana kisiasa ama mtashindwa kupingana wakati mwanachama mwenzako ametoa pumba ili kulinda heshima ya chama chenu, au mtapinga hata pale nukta za muhimu sana zimetolewa iwapo mnajua kuwa aliyezitoa yuko chama tofauti na cha kwenu.

Heri yangu nilishafukuzwa chama changu na kila mtu anajua wazi kabisa kuwa sina langu tena.
 
Asha nae.....umekuwa msemaji wa Mpaka kieleweke? A'fu humu wanafiki sana wakipigwa kwenye maeneo yao wanakuwa wakali.....lakini wenyewe wanasahau wanapiga kambai nyingine makombola...

Mimi ukinijua usiponijua haitaniathili sana sana unapoteza muda wako bure....
 
Ama kweli, mkuki kwa kondoo!

Kuhamanika kwako ni ishara kwamba ujumbe umefika. Msumari unachoma kote kote kwa kweli

Hebu kumbuka mjadala wa Chacha Wangwe kusimamishwa! Ni wewe uliyeanza kusema unajua nani yuko nyuma ya jina la Mpaka Kieleweke.

Mkuu huu ndio ushahidi ulionao kuwa mimi ndiye niliyeanza kumsema Kieleweke kuwa ni Mbowe? Nilifkiri una ushahidi wa kweli hapana mimi kwangu hapa nafikiri hata wananchi hapa watasoma ukweli ulipo sina haja ya kuendelea kubishana na upuuuzi! Kwa sababu huu ni upuuzi! Na I am too big for this, hii forum tumeambiwa mara nyingi sana sio ya Chadema na ninataka kuamini hivyo maana ndivyo ninavyoamini period!

Na kama huu uliouweka ni ushahidi wakutosha basi ninawaruhusu Mods wanichukulie hatua zinazotakiwa, lakini hata siku moja sitatishika na vitisho vya kutaka niwe bendera ya Chadema, hapana mengine sitakujbu kwa sababu ya kumuheshimu yeye mwenye mkuu Kieleweke, kwa sababu baada ya mimi kumshauri awaachie wengine ku-spin, alinitumia PM lakini kwa heshima yake siwezi kuiweka hapa wala hakusema maneno mengi unayonihukumu nayo hapa, na bado ninaendelea kumuheshimu kwa sababu sina beef naye hata siku moja, waliomuita Mbowe wako wazi kule kwenye thread ya Chacha Wange aliyoianzisha yeye Kieleweke, sio kazi yangu hapa JF kukanusha habari za member hata siku moja na hata nikiamua ni umauzi wangu ila siowezi kushinikizwa hata siku moja na anybody,

kama ni ujumbe hilo sina wasi wasi hata siku moja kuhusu kufika au kutofika, msimamo wangu ni ule kama una aamini kuwa ujumbe wako umefika, basi na mimi ninaamini pia wa kwangu umefika tena sana na zaidi kwenye hilo wala sina wasi wasi, maneno ya kumtaja Kieleweke kuwa ni Mbowe yako kule tena wazi na sio mimi niliyeyaanza, nilimuomba Kieleweke awaachie wengine ku-kuspin akanijibu kuwa amenielewa tena bila tatizo, na the next thing nikaona kwamba ni kweli amenielewa,

Wewe mkuu kusema ni haki yako kama ilivyo ya kwangu, mimi kama kawaiada jina moja tu sina mengi for that I am very proud off, kama sio sawa kutukanwa Chinga, basi isiwe sawa akitukanwa Kieleweke, huo ndio msimamo wangu. Mkuu Kieleweke kama kuna mahali nimekutaja kuwa wewe ni Mbowe nifahamishe nitakuomba radhi lakini so far sijawahi kukusema kuwa wewe ni Mbowe na unajua kuwa siku zote mimi na wewe heshima ni mbele zaidi na ninakutakia mafanikio na shughuli zako za kila siku.

Kwenu Mods na Invisible, kama huu ni ushahidi wakutosha kuwa mimi ndiye chanzo cha kumuita Kieleweke kuwa ni Mbowe nipeni adhabu na muiseme wazi hapa mimi sina tatizo hata siku moja kukubali adhabu kwa makosa niliyofanya!

Ahsante Mkuu
 
Yawezekana mimi ni maarufui pia , huenda siku moja nikataka kugombea JF President naweza kushinda kwani sitakuwa na haja ya kufanya kampeni kwani hizi ni kampeni tosha.

Kuna wachache ambao nawaamini wananijua,ila wapo wengi sana wanataka kunijua kuwa mimi ni nani itawachukua karne nyingine moja sasa sijui nitakuwa kikongwe sana maana mpaka sasa nimezeeka kiasi.

Ninaishi nje ya dunia ila nina mawasiliano ya karibu sana na duniani kwani niliwahi kuishi humo zamani za kale.

Anayetaka kunifahamu sharti awe na uwezo wa kuishi nje ya dunia na ndani ya Ardhi....
 
Yawezekana mimi ni maarufui pia , huenda siku moja nikataka kugombea JF President naweza kushinda kwani sitakuwa na haja ya kufanya kampeni kwani hizi ni kampeni tosha.

Kuna wachache ambao nawaamini wananijua,ila wapo wengi sana wanataka kunijua kuwa mimi ni nani itawachukua karne nyingine moja sasa sijui nitakuwa kikongwe sana maana mpaka sasa nimezeeka kiasi.

Ninaishi nje ya dunia ila nina mawasiliano ya karibu sana na duniani kwani niliwahi kuishi humo zamani za kale.

Anayetaka kunifahamu sharti awe na uwezo wa kuishi nje ya dunia na ndani ya Ardhi....

Mhhh.. mpaka kieleweke mbona watutisha? anyway umenikumbusha hadithi za maluhani!
 
Yawezekana mimi ni maarufui pia , huenda siku moja nikataka kugombea JF President naweza kushinda kwani sitakuwa na haja ya kufanya kampeni kwani hizi ni kampeni tosha.

Kuna wachache ambao nawaamini wananijua,ila wapo wengi sana wanataka kunijua kuwa mimi ni nani itawachukua karne nyingine moja sasa sijui nitakuwa kikongwe sana maana mpaka sasa nimezeeka kiasi.

Ninaishi nje ya dunia ila nina mawasiliano ya karibu sana na duniani kwani niliwahi kuishi humo zamani za kale.

Anayetaka kunifahamu sharti awe na uwezo wa kuishi nje ya dunia na ndani ya Ardhi....

Very loud simple and clear!
 
Yawezekana mimi ni maarufui pia , huenda siku moja nikataka kugombea JF President naweza kushinda kwani sitakuwa na haja ya kufanya kampeni kwani hizi ni kampeni tosha.

Kuna wachache ambao nawaamini wananijua,ila wapo wengi sana wanataka kunijua kuwa mimi ni nani itawachukua karne nyingine moja sasa sijui nitakuwa kikongwe sana maana mpaka sasa nimezeeka kiasi.

Ninaishi nje ya dunia ila nina mawasiliano ya karibu sana na duniani kwani niliwahi kuishi humo zamani za kale.

Anayetaka kunifahamu sharti awe na uwezo wa kuishi nje ya dunia na ndani ya Ardhi....

umaarufu kumbe ndio sifa ya kupata urais? una gharama kubwa kuumaintain pia. mafisadi wataendelea kuila Tanzania kama ndio mwendo huu.
 
Halafu FYI msimamo wangu hapa kukataa watu kutajana majina umekuwa wazi kabisa kama umekuwa mfuatiliaji. Nimejitokeza kukemea watu wakijaribu kubashiri nani ni nani! So its not the first time, sijaanzia na mpaka kieleweke. Labda lapekee hapa ni kuwa safari nimefungua thread kabisa kukanusha. Ni kutokana na uzito wa Bwana Mbowe kama Mwenyekiti wa CHADEMA. Ilipokuwa kwa Kitila na wengine nilisema tu katika thread ya mtu aliyezua huo uzushi tu.

As far As I am concerned, message delivered, case closed, I am out on this

Nawakatika mjadila mwema, tujifunze kujadili issues badala ya persons!

Mkuu wangu nimekusikia tena very loud and clear!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom