Morogoro: Selemani Msindi (Afande Sele) adakwa na kulazwa Korokoroni, mdomo wake wamponza

Labda kama ana kosa lingine, lakini kama ni hilo la kumlaumu Mungu itakuwa ni ujinga huu.

Sijaiona hiyo clip ya kulaumu lakini nimekutana na malalamiko kadhaa kwamba kakosea blah blah.

Kama angekashifu dini/imani ya Mwingine sawa maana hapo kosa ni kumuudhi mwingine...lakini Mungu huyu wetu sote kama Mtu ataamua kutukana kadri anavyojisikia sioni kama kama kuna mwenye mamlaka ya kumuadhibu mwingine, sana sana ni kumsihi asifanye hivyo mbele yako maana hupendi kusikia.
 
Msanii mkongwe wa muziki, Selemani Msindi maarufu Afande Sele, anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mjini Morogoro kwa mahojiano baada ya video yake iliyokuwa na maudhui ya kumlaumu Mwenyezi Mungu kwa kile alichodai hakutenda haki kuruhusu kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania Dkt. Magufuli.

Hivi karibuni Afande Sele alisikika akimlaumu Mungu kuruhusu Magufuli afe.

Mkuu wa Polisi Morogoro kasema kesho ataongea kinagaubaka sababu za kumkamata na kumlaza Korokoroni.

Zaidi soma: Afande Sele (Seleman Msindi), asomewa dua ya kufa kabla ya Ramadhan ya 2021 kufika, atuhumiwa kumkufuru Mungu

View attachment 1732037
Hii kesi nashauri wai-forward kwa Askofu, Mchungaji, au kwa Baba Paroko
 
Mimi ni Mkristo, Ukristo unaamini sana katika TOBA, Yesu anasema, "amin amin nawaambieni, atakae mkufuru Baba au mwana atasamehewa, lakini yeye atakae mkufuru Roho mtakatifu hatasamehewa" Afande Sele ni kweli alikufuru, hakatai kwamba alikufuru ( anoather credit kwa Mungu ) but kaomba RADHI kwa Mungu wake aliyemkufuru na kwa wote aliowakwaza; sasa najiuliza; jamuhuri itamshtaki kwa kosa lipi? Yaani nani anae mlalamikia afande Sele?
Binafsi ninaamini kabisa (kwa matamshi yake ) huyo Mungu aliyemkashfu kisha msamehe, kwasasa Seleman Msindi kaomba msamaha kwake
 
Umeisikiliza voice clip ya maneno ya Afande Sele kweli?

Mimi nimeisikiliza mwanzo mwisho. Hajakashfu dini wala imani ya mtu yeyote..

Yeye ana bifu na Mungu wake siyo na mtu au imani au dini ya mtu yeyote...

Ashtakiwe kwa kosa lingine labda la kwa kutumia sheria ya makosa ya kimtandao - Cyber Crime la " kutumia mtandao kurusha kashfa na matusi hadharani" lakini siyo hili la "kumtukana Mungu" maana halina ushahidi na haliwezi kuthibitika mbele ya sheria...
Ndio maana ukiingia kuswali msikitini, na kusali makanisani kuna muda upo, unaomba, kuongea, kutukanana wewe na Mungu wako kimya kimya kama una bifu naye unajua mwenyewe. Ukiliweka hadharani ni kashfa kwa wasio na bifu na Miungu yao.
 
Kama haina dini basi iruhusu watu kukashifu imani ya wengine?
Kakashifu imani ya nani? Mimi nilisikiliza ile clip. Haamini uwepo wa Mungu. Hili ni jambo la mtu binafsi. Alisema ataabudu hata jua. Huwezi kumlazimisha mtu kuamini na polisi wamefanya kosa kubwa sana. Acha Mungu ajitetee mwenyewe. Kwanza hili kwa Mungu siyo issue kubwa kama binadamu mnafiki anavyotaka ionekana. Mbona wapo watu kama kina Paulo walimhujumu Mungu lakini baada wakaja badalika?
 
Bora ashughulikiwe na serikali
Mungu mwenyewe akimshughulikia hata SEKUNDE NYINGI.
Anakauka.
Unafikiri Mungu ana akili mbovu namna hiyo? Wanafiki wakubwa nyie wanadamu. Mtu kama yule sheikh papuchi anabanjua kama hana akili nzuri halafu leo anakuja ''kumwamurisha'' Mungu aue kiumbe chake! Kwani Mungu yeye haoni? Au mnafikiri Mungu ni kama serikali inayoogopa kuhojiwa?
 
Mungu nae ana HASIRA.
Akichukia inawezekana tusiamke kesho.
Acha Afundishwe.
Kuwa hii dunia na pumzi si Yetu.
Mtu anatukaniwa BABA yake anachukia sembuse kutukaniwa Mungu?.
Unafikiri Mungu ana akili mbovu namna hiyo? Wanafiki wakubwa nyie wanadamu. Mtu kama yule sheikh papuchi anabanjua kama hana akili nzuri halafu leo anakuja ''kumwamurisha'' Mungu aue kiumbe chake! Kwani Mungu yeye haoni? Au mnafikiri Mungu ni kama serikali inayoogopa kuhojiwa?
 
Mungu nae ana HASIRA.
Akichukia inawezekana tusiamke kesho.
Acha Afundishwe.
Kuwa hii dunia na pumzi si Yetu.
Mtu anatukaniwa BABA yake anachukia sembuse kutukaniwa Mungu?.
Hivi unajua duniani kuna mamilioni ya watu ambao hawaamini kuwa kuna Mungu na Mungu hata siku moja hajawahi kuwaadhibu? Kwa nini mnataka kumfundisha Mungu kazi?
 
Kama haina dini basi iruhusu watu kukashifu imani ya wengine?

Hujaelewa kitu, kiazi! Inawezaje kuruhusu kukashifu wakati kutoa kashfa au dhihaka ni kosa?? Wakisema haina dini hawana maana mtu aseme chochote juu ya imani ya mtu mwingine. Ina maana maamuzi yake hayataathiriwa na imani moja na si nyingine katika kushughulikia mambo ya kisheria. Kama ukiua mtu, huwezi ukasema mahakama ikuachie huru kwa sababu ulikuwa unamtoa mtu huyo kama dhabihu kwa mungu wako!!

Inabidi tutoe na mifano ili vilaza waelewe!!
 
Back
Top Bottom