Morogoro Enzi Hizo: Hii ndio Morogoro bwana!

Morogoro Enzi Hizo: Hii ndio Morogoro bwana!

Namimi hii hapa, niliishi Moro mwaka 1993/4, Eneo la Mazimbo, kipindi hicho ni Poli tu kuanzia Mazimbu Kanisa Katoliki hadi Daraja la treni Tinge tinge karibu na Kambi ya Wakimbizi ya Mazimbu. Asubuhi Lukobe Shamba, kulima mpunga, jioni kumwagilia bustani za babu pembezoni mwa mto Ngerengere. Nilijifunza kulima miwa, choroko na kuvua Dagaa uduvi. Tukiamka mimi na dada zangu ni kwenda Kupanga foleni ndani ya Kambi za wakimbizi wa South Africa kuchukua mbao za kuni za kupikia nyumbani. Wakati mwingine wasimamizi wa Wakimbizi (UNHR), utufungulia Makontena tuchukue nguo na viatu, tukifika nyumbani tunauza. Mjini kati Moro kwenda mpaka sikukuu, Sisi tulikua wapori pori tu uko Mazimbu.
huko lukobe sasa hivi ni town watu wamejenga balaa yaan moro imebadilika sana.
 
Hapo kwenye list ya kikosi cha Reli Moro mwongeze Mbui Yondani.Jamaa alikuwa hatari sana.Enzi hizo mpira tulisikilizia RTD.
 
Standard 7 Bungo primary 1995
1996-99 Kigurunyembe Secondary O-level
A-level 2000-2002 Forest Hill Secondary

Sent from my SM-J100H using JamiiForums mobile app
Forest Hills watoto wa pateli au sio nawewe ni mwarabu nini make ndo wamejaa pale!

Lol maeneo ya forest huko kichangani kilakala kote tulikua tunaenda kuchota maji pindi hostel morosec yakikatika hapo ndo tunapata muda wa kuzuruzaaa



Cc Smart911
 
Wavivu sana, wanapenda vigodoro,

Sema tu washukuru LAPF mfuko wa pension wamewajengea stand ya kisasa
Mzee Baba, nyinyi wapambanaji mbona bado hamna maendeleo!?. Hujasikia Bill Gates anasema "Siku zote wavivu ndio Wabunifu"?. Maana hupenda kutafuta njia rahisi sana ya kutatua tatizo ili wapate Muda wa kula bata.
 
Katika vyote mi nakumbuka sinema shani cinema na sapna. Alafu pale maeneo ya mlapakolo kulikuwa na muuza chips mmoja alikuwa anaitwa Peter, yule jamaa alikuwa anachoma mishikaki ya hatari sana ingawa baadae akapata mpinzani aitwae Kabele kama sijakosea
 
Katika vyote mi nakumbuka sinema shani cinema na sapna. Alafu pale maeneo ya mlapakolo kulikuwa na muuza chips mmoja alikuwa anaitwa Peter, yule jamaa alikuwa anachoma mishikaki ya hatari sana ingawa baadae akapata mpinzani aitwae Kabele kama sijakosea
sapna na shani cinema zilisha kufa zaman cjui kwa sasa hivi
 
Morogoro miaka ya 90 kulikuwa na radio moja tu
Kabla ya ujio wa radio Abood na radio Iman
hiyo radio ni,,,,,,
 
Back
Top Bottom