Mtanzanias
JF-Expert Member
- Jul 30, 2021
- 1,747
- 3,723
Tunategemea mechi nzuri sana na yenye ushindani mkali leo hii kwakuwa zinakutana timu ambazo zote ziko vizuri kiufundi na zikiwa na wachezaji bora kwenye vikosi vyao, Monastir walimfunga yanga goli 2 kule Tunisia na aina ya magoli ambayo walifunga ni mipira ya kutengwa (set pieces), ni eneo ambalo yanga watakuwa wamelianyia kazi vya kutosha na sidhani kama watafanya tena makosa ya kuruhusu mipira ya namna ile.
Ushindi kwa yanga leo hii ni kitu kisichoepukika ni sawa na maji usipoyanywa utayaoga, Yanga kwa sasa wanayo timu bora, benchi bora la ufundi na wanajiamini sana.
Yanga kupata matokeo kwenye uwanja wowote ule hapa afrika sio story tena kutokana na confidence waliyonayo kwa sasa.
Kwa maana iyo Monastir wajiandae kukutana na yanga tofauti na ile waliyocheza nayo mechi ya kwanza. Ni mechi dume na nzuri sana na ni kipimo tosha kitakachoonyesha ubora wa kikosi cha yanga walichotengeneza kwa sasa ambacho kinawafanya wasiwe na stress wala wasiwasi wanapocheza mechi yoyote ile iwe ndani ya nchi ama nje ya nchi.
Nauona ushindi wa yanga aijalishi magoli mangapi bali watasonga mbele na nawaona wakifika nusu fainali kwa mara ya kwanza katika historia.
Ushindi kwa yanga leo hii ni kitu kisichoepukika ni sawa na maji usipoyanywa utayaoga, Yanga kwa sasa wanayo timu bora, benchi bora la ufundi na wanajiamini sana.
Yanga kupata matokeo kwenye uwanja wowote ule hapa afrika sio story tena kutokana na confidence waliyonayo kwa sasa.
Kwa maana iyo Monastir wajiandae kukutana na yanga tofauti na ile waliyocheza nayo mechi ya kwanza. Ni mechi dume na nzuri sana na ni kipimo tosha kitakachoonyesha ubora wa kikosi cha yanga walichotengeneza kwa sasa ambacho kinawafanya wasiwe na stress wala wasiwasi wanapocheza mechi yoyote ile iwe ndani ya nchi ama nje ya nchi.
Nauona ushindi wa yanga aijalishi magoli mangapi bali watasonga mbele na nawaona wakifika nusu fainali kwa mara ya kwanza katika historia.