TANZIA Mohamed Raza afariki dunia. Ni mfanyabiashara, mwanasiasa na mdau mkubwa wa michezo Zanzibar

Sol de Mayo

JF-Expert Member
Sep 10, 2016
6,330
5,934
Mohammed  Raza afariki dunia.jpg

Mfanyabiashara maarufu wa Zanzibar na Mwanasiasa ambaye aliwahi kuwa Mwakilishi Jimbo la Uzini Mkoa wa Kusini Unguja, Mohamed Raza amefariki leo hii wakati alipokuwa akipatiwa matibabu, Allah amrehemu ndugu yetu huyu, na amuingize katika pepo.

Itakumbukwa May 09,2023 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Mwinyi alimtembelea Mohamed Raza baada ya kulazwa Hospitalini Jijini Dar es Salaam.

Allah amjaalie kauli thabit huyu ndugu yetu, Aamiin.

=======

Aliyekuwa muwakilishi jimbo la Mkunazini kupitia Chama cha Mapinduzi(CCM), Mohamed Raza ameaga dunia leo Juni 08, 2023 wakati akitibiwa jijini Dar es Salaam. Mohamed Raza Hassanali Dharamsi alizaliwa Julai 18, 1962 eneo la Mkunazini, ni mfanyabiashara maarufu visiwani Zanzibar.

Raza alizaliwa Zanzibar kwa wazazi wenye asili ya kihindi na alisoma shule ya Shaaban Robert iliyopo Upanga, Dar es Salaam mwaka 1977 mpaka 1980.

Alichaguliwa kwa mara ya kwanza mwaka 2012 kuliwakilisha jimbo la Uzini, nafasi ambayo ameweza kuihudumu kwa zaidi ya miaka 10. Februari mosi zilisambaa taarifa za kifo chake ambazo zilikanushwa na mwandishi maarufu wa Zanzibar, Farouk Karim na kusema anaumwa lakini alikuwa mzima.

Baada ya kuhitimu kidato cha nne shule ya Shaaban Robert, Raza aliingia kwenye biashara kwa kuungwa mkono na jamii ya Kishia kupitia jamii ya wahindi ya Ithhia Zanzibar na kuibuka kwake na fursa za kibiashara kukisaidiwa na mfanyabiashara maarufu Zanzibar, Naushad Mohamed Suleiman. Uhusiano wa wawili hao ulikuja kuyumba 2016 kutokana na kutoaminiana.
 
Mfanyabiashara maarufu wa Zanzibar na Mwanasiasa aliyewahi kuwa Mwakilishi wa Jimbo la Uzini, Mkoa wa Kusini Unguja, Mohamed Raza amefariki dunia leo Juni 8, 2023 Saa tano asubuhi katika Hospital ya Aga Khan, jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu.

Taarifa za msiba huo ambazo zimethibitishwa na mmoja wa wanafamilia aliyejitambulisha kwa jina la Mohammed Ibrahim Raza, maziko yake yanafanyika Saa 11 jioni katika makaburi ya Kisutu, Dar es Salaam.

“Ni kweli ndugu yetu aametutoka tunategemea kumpumzisha kwenye nyumba yake ya milele katika makaburi ya Kisutu leo saa 11 jioni,” amesema Mohamed.

Mei 9, 2023, Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi alifika katika Hospitali ya Aga Khan alikokuwa amelazwa kwa lengo la kumjulia hali.
 
HHuyu

Mfanyabiashara maarufu wa Zanzibar na Mwanasiasa ambaye aliwahi kuwa Mwakilishi Jimbo la Uzini Mkoa wa Kusini Unguja, Mohamed Raza amefariki leo hii wakati alipokuwa akipatiwa matibabu, Allah amrehemu ndugu yetu huyu, na amuingize katika pepo.

Itakumbukwa May 09,2023 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Mwinyi alimtembelea Mohamed Raza baada ya kulazwa Hospitalini Jijini Dar es Salaam.

Allah amjaalie kauli thabit huyu ndugu yetu, Aamiin.

=======

Muwakilishi jimbo la Mkunazini kupitia Chama cha Mapinduzi(CCM), Mohamed Raza ameaga dunia leo wakati akitibiwa jijini Dar es Salaam. Mohamed Raza Hassanali Dharamsi alizaliwa Julai 18, 1962 eneo la Mkunazini, ni mfanyabiashara maarufu visiwani Zanzibar na mpaka anafariki leo Juni 08, 2023 alikuwa bado ana dhamana ya uwakilishi wa Mkunazini kwenye baraza la wawakilishi Zanzibar.

Raza alizaliwa Zanzibar kwa wazazi wenye asili ya kihindi na alisoma shule ya Shaaban Robert iliyopo Upanga, Dar es Salaam mwaka 1977 mpaka 1980.

Alichaguliwa kwa mara ya kwanza mwaka 2012 kuliwakilisha jimbo la Uzini, nafasi ambayo ameweza kuihudumu kwa zaidi ya miaka 10. Februari mosi zilisambaa taarifa za kifo chake ambazo zilikanushwa na mwandishi maarufu wa Zanzibar, Farouk Karim na kusema anaumwa lakini alikuwa mzima.

Baada ya kuhitimu kidato cha nne shule ya Shaaban Robert, Raza aliingia kwenye biashara kwa kuungwa mkono na jamii ya Kishia kupitia jamii ya wahindi ya Ithhia Zanzibar na kuibuka kwake na fursa za kibiashara kukisaidiwa na mfanyabiashara maarufu Zanzibar, Naushad Mohamed Suleiman. Uhusiano wa wawili hao ulikuja kuyumba 2016 kutokana na kutoaminiana.
Huyu inasemekana alikuwa anajihusisha mapenzi ya kisodoma wakati wa utawala wa komandoo
 
Back
Top Bottom