Mogae wa Botswana ashinda tuzo

Ladslaus Modest

JF-Expert Member
Jun 27, 2008
635
20
Aliyekuwa rais wa Botswana, Festus Mogae, ameshinda tuzo yenye thamani ya dola za kimarekani milioni 5 itakayohamasisha utawala bora barani Afrika.

Bw Mogae aliachia madaraka mwezi Aprili baada ya kutumikia urais kwa vipindi viwili nchini humo.

Botswana ni moja ya nchi zenye utulivu mno kutoka bara la Afrika, haijawahi kuwa na mapinduzi na imekuwa na uchaguzi wa vyama vingi mara kwa mara tangu nchi hiyo kupata uhuru mwaka 1966.

Wakati wa kutangazwa zawadi hiyo, aliyekuwa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, Koffi Annan, amemsifia Bw Mogae kwa hatua yake ya kupambana na ugonjwa wa ukimwi uliokithiri nchini humo.

Tuzo ya Mo Ibrahim, ambayo ni tuzo yenye thamani ya juu kabisa duniani ilianzishwa na mjasiriamali wa masuala ya mawasiliano aliye raia wa Sudan, Mo Ibrahim.

Mbali na tuzo hiyo ya milioni 5, Bw Mogae pia atapokea dola za kimarekani 200,000 kwa mwaka mpaka maisha yake yatakapofikia hatima.

Botswana imejaaliwa na madini ya almasi, lakini ukilinganisha na nchi nyingine zenye utajiri wa aina hiyo barani Afrika madini hayo haikuwa chanzo cha mgogoro nchini humo.
Chanzo BBC


Ninatumaini kipindi kijacho zawadi hii itakuja Tanzania.
 
Mogae anastahili tuzo hii, aliachia madaraka miezi kadhaa kabla ya muda wake. try that with the Musevenis and Salmin Amours of Africa.

Botswana is an example to be emulated.
 
Nasikia na Mkapa alikuwemo kwenye kinyang'anyiro cha hiyo tuzo kwa mara ya pili tena..Tanzania sitarajii kama kuna Rais yeyote anayeweza kupata hiyo tuzo may be Mwl. Nyerere kama angekuwa hai hawa waliobakia wote hamna kitu!!
 
Hii ni zawadi nzuri sana kwa kiongozi aliyestaafu kwa heshima. Ila sidhani kama viongozi wetu wanaweza kutosheka nazo kwa vile wanaona ni tujisenti tu.

NB: Kama kuna thread inayoongelea jambo hili hili, naomba Mod uiunganishe kwa vile siku hizi ninaishi msituni.

Botswana's Mogae wins five-million-dollar African prize

LONDON (AFP) - Botswana's former president Festus Mogae was Monday named the winner of a five-million-dollar prize for good governance in Africa, winning praise for putting his country's mineral wealth to good use.

Announcing the Ibrahim Prize for Achievement in African Leadership in London's City Hall, former UN secretary-general Kofi Annan also praised Mogae's efforts in fighting AIDS in the southern African nation.

"President Mogae's outstanding leadership has ensured Botswana's continued stability and prosperity in the face of an HIV/AIDS pandemic which threatened the future of his country and people," Annan said.

"Botswana demonstrates how a country with natural resources can promote sustainable development with good governance, in a continent where too often mineral wealth has become a curse," Annan added.

Botswana is one of Africa's most stable countries, with a high credit rating and one of the best standards of living on the continent.

Annan also praised Mogae, who handed over power in April after a decade in office, for successfully diversifying Botswana's economy to reduce its dependence on diamonds -- it is the world's biggest producer of the gems.

Mogae has encouraged companies to mine large reserves of coal and open Botswana up to tourists to take advantage of the country's spectacular wildlife.

Guinea's former education minister Aicha Bah Diallo, a member of the prize committee, compared Botswana's progress with the decade-long civil war in another diamond-rich African country, Sierra Leone.

AFP: Botswana's Mogae wins five-million-dollar African prize
 
Tanzania hatutapata zawadi hii baada ya Kumkosa SAS kwenye Urais. Alioko madarakani na waliomtangulia (ukimwacha Mwalimu) wamejitengenezea wenyewe "ZAWADI" zao.
 
Tanzania hatutapata zawadi hii baada ya Kumkosa SAS kwenye Urais. Alioko madarakani na waliomtangulia (ukimwacha Mwalimu) wamejitengenezea wenyewe "ZAWADI" zao.

Wajitengenezee mara mbili? wameshajitengenezea tayarii.
 
Nakumbuka Museven alisema hiyo zawadi haitaki kwa sababu anauwezo wa kupata hizo hela akiendelea kuwa rais indefinitely! Wakimpa Mkapa wa TZ tutaandamana! Surprisingly anaweza kupata mwakani! Unajua Mogae alikosa last year, alikuwa wa pili baada ya Chissano na Mkapa alikuwa wa tatu!
 
KWA mwaka wa pili mfululizo, Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin William Mkapa, ameshindwa kutwaa tuzo ya utawala bora, yenye thamani ya mabilioni ya shilingi, inayotolewa na mmoja wa matajiri wakubwa duniani, Mo Ibrahim.

Tuzo hiyo iliyopewa jina la muasisi wake, Mo Ibrahim, ambayo ni kubwa kuliko zote kutolewa kwa mtu binafsi, imechukuliwa na rais mstaafu wa Botswana aliyeondoka madarakani Aprili mwaka huu, Festus Mogae (69), aliyeiongoza nchi yake hiyo ya kusini mwa Afrika kwa mafanikio makubwa kijamii, kiuchumi na kisiasa kwa miaka 10.

Ushindi huo wa Mogae unamfanya awe rais mstaafu wa pili kutwaa tuzo hiyo itakayomwezesha kuvuna kitita cha dola za Marekani milioni tano (karibu shilingi bilioni 6.5), baada ya mwaka jana kuchukuliwa na rais mstaafu wa Msumbiji, Joachim Chissano.

Mbali ya kutwaa kiasi hicho kikubwa cha fedha, Mogae kama ilivyokuwa kwa Chissano, atakuwa akipata kiasi kingine cha dola 200,000 (karibu shilingi milioni 260) kila mwaka kwa maisha yake yote.

Kabla ya Mogae kutangazwa kuwa ndiye mshindi wa tuzo hiyo jana jijini London, vyombo mbalimbali vya habari vya kimataifa vilikuwa vikimtaja Mkapa pamoja na viongozi wengine kadhaa wastaafu wa Afrika kuwa miongoni mwa watu waliokuwa wakipewa nafasi ya kushinda.

Kutajwa kwa Mkapa katika orodha ya viongozi wastaafu kwa mwaka huu, kumekuja mara ya pili, baada ya mwaka jana jina lake kuvuma hadi siku Chissano alipotangazwa kuwa mshindi.

Viongozi wengine ambao majina yao yamekuwa yakitajwa mara kwa mara kuwa walistahili kushinda tuzo hiyo ni pamoja na rais wa zamani wa Nigeria, Olusegun Obasanjo na mwenzake wa Sierra Leone, Tejan Kabbah.

Kabla na wakati wa utawala wa Mogae, Botswana imekuwa nchi yenye utulivu mkubwa wa kisiasa, ikiendeshwa chini ya mfumo wa vyama vingi tangu ilipopata uhuru mwaka 1966.

Akitangaza mshindi wa tuzo hiyo jijini London jana, Katibu Mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa (UN), Kofi Annan, alimwelezea Mogae kama mtu aliyekuwa mstari wa mbele katika kupambana na ugonjwa wa ukimwi, ambao umeitikisa nchi ya Botswana.

“Uongozi imara wa Mogae umehakikisha Botswana inaendelea na uthabiti wake wa kukabiliana na ugonjwa wa ukimwi ambao unatishia hali ya baadaye ya watu wa nchi hiyo,” alisema Annan.

Annan pia alimtaja Mogae kama mtu aliyekuwa akijaribu kutafuta njia nyingine ya kuimarisha uchumi wake mbali na kutegemea rasilimali ya dhahabu.

Mwaka 2006, serikali ya Mogae ilianzisha sheria ya kudhibiti uuzwaji wa pombe na kupiga marufuku kinywaji hicho kuuzwa Jumapili baada ya takwimu kuhusisha ulevi na kuongezeka kwa maambukizi ya ukimwi.

Lakini hata hivyo Mogae ambaye aliachia madaraka kwa Seretse Khama, aliyewasili hapa nchini jana, alijikuta kwenye upinzani mkali baada ya sera yake ya kuwahamisha makundi ya watu wanaoishi porini katika nyumba zao za kijadi katika Jangwa la Kalahari.

Taarifa ya Mo Ibrahim ilieleza kuwa nchi nyingi za Afrika zilikuwa zimeimarika katika suala la utawala bora.

Lakini katika kielezo chake cha takwimu kilichochukuliwa tangu mwaka 2006, Mauritius imekuwa nchi inayoongoza kwa dhana ya utawala bora kati ya nchi 48 za Afrika na kwamba Liberia nayo ikichukua mkondo mzuri baada ya kuyumba miaka kadhaa iliyopita.

Nchi tano zilizotajwa kufanya vizuri katika utawala bora ni pamoja na Mauritius, Ushelisheli, Cape Verde, Botswana na Afrika Kusini.

Wakati nchi tano zilizofanya vibaya katika dhana nzima ya utawala bora ni pamoja na Angola iliyoshika nafasi ya 44, Sudan ya 45, Chad ya 46, Kongo ya 47 na mwisho kabisa ni Somalia ambayo imeshika ni ya 48.

Alipohojiwa jana na Idhaa ya Kiswahili ya BBC jinsi alivyoipokea tuzo hiyo, Rais huyo mstaafu wa Botswana alisema, anajisikia heshima kushinda tuzo hiyo hasa ikizingatiwa kuwa hiyo ni taasisi huru inayotumia jitihada zake yenyewe kufanya kazi hiyo.

Hata hivyo alisema yeye hakuanzisha utawala wa sheria na wa kidemokrasia nchini Botswana, bali alichokifanya ni kuimarisha kile alichokikuta.

Naye, Katibu Mkuu wa zamani wa uliokuwa Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU), Dk. Salim Ahmed Salim, alisema rais huyo alistahili kabisa kupata tuzo hiyo kwani alifanya kazi kubwa katika kunyanyua maisha ya wanawake na kuifanya Botswana kuwa moja kati ya nchi nne duniani, ambazo kuna uwiano sawa kati ya wanawake na wanaume katika elimu.

Vigezo ambavyo vinatumika kumpata mshindi wa tuzo hiyo ni kuendeleza misingi ya utawala bora, upiganiaji wa haki za binadamu na namna mhusika alivyoshiriki katika kuiletea nchi yake na Bara la Afrika maendeleo wakati akiwa madarakani.

Viongozi wengine waliochuana mwaka jana ni pamoja na Mathieu Kerekou (Benin), Azali Assoumani (Comoros), Domitien Ndayizeye (Burundi) na Henrique Rosa (Guinea Bissau).

Wengine ni Maaouya Ould Sid'Ahmed Taya (Mauritania), Joaquim Chissano (Msumbiji), Sam Nujoma (Namibia) Benjamin Mkapa (Tanzania), Abass Bonfoh (Togo), Gnassingbe Eyadema (Togo), Bakili Muluzi (Malawi) France-Albert Rene (Shelisheli) na Abdiqassim Salad Hassan (Somalia).

Chissano, mtu aliyekuwa akipewa nafasi kubwa ya kuchukua tuzo hiyo alikaa madarakani kwa miaka 19, na katika kipindi hicho akachukua hatua mbalimbali zilizosaidia kumjenga kisiasa kitaifa na kimataifa.

Miongoni mwa masuala yaliyomjengea umaarufu mkubwa ni pamoja na namna alivyoweza kumaliza vita ya wenyewe kwa wenyewe kati ya serikali yake na Chama cha upinzani cha Renamo kinachoongozwa na Alfonso Dhlakama.

Aidha, katika kipindi chake cha urais, Chissano, anatajwa kuwa rais aliyeweza kusimamia vyema rekodi ya kukuza uchumi wa taifa lake, sambamba na kuheshimu haki za binadamu.

Wakati Chissano akiweka rekodi hizo, Mkapa analaumiwa kwa kushindwa kumaliza mgogoro wa kisiasa uliodumu kwa zaidi ya miaka 10 Zanzibar, ingawa amekuwa akisifiwa kwa kukuza uchumi wa Tanzania.

Mo ambaye ndiye mwanzilishi wa Kampuni ya simu nya Celtel, alitangaza azima ya kuanzisha tuzo hiyo mwaka jana kwa matarajio ya kuongeza uwezo wa Bara la Afrika kujitegemea na ili siku moja watu wake waishi bila ya kutegemea misaada.

“Tunahitaji kuondoa rushwa, tunahitaji kuboresha utawala, tunahitaji kuwa na afya na baadaye hatutahitaji misaada,” alisema Ibrahim.
 
Baadhi ya watu walitoa maoni yao juu ya Mr Clean alivyo kosa hii tuzo.
Wakimpa Mkapa hii tuzo itakuwa hawa jamaa hawako makini mtu ameua watu kibao zanzibar na kunyanyasa wapinzani na democrasia isikue katika awamu yake halafu wampe?
Nawapongeza sana majaji wa huu mfuko sasa naanza amini wako makini na kazi wanayo fanya.

Papa Gee,
Na kati ya Arusha.

na Papa Gee, Arusha, - 21.10.08 @ 08:50 | #49403

Hongera morgae. Wengine wa kupewa ni Mwanawasa, kagame, mbeki. Kuffor wa Ghana. Lakini Brother Che nkapa mweke pembeni pamoja na JK, kurunzinza, kabila, kibaki, museveni, msweti II, santos, mwinyi, omar wa sudan. Mumbarak wote hawa hatufai kupewa

na Al Hasan Mwinyi, Tz, - 21.10.08 @ 08:57 | #49404

Mkapa mmemnyima Tuzo wenyewe kwa kumwandika kama fisadi

na jomba, moro, - 21.10.08 @ 09:00 | #49405

mimi nashangaa sana kwa mtu kama mkapa na huyu eyadema kufikiliwa kupewa tuzo kama hizi ni maajabu matupu. viongozi hawa ni wala rushwa wakubwa na wanaongoza kwa kuvunja haki za binadamu, kudidimiza demokrasia na uhuru wa vyombo vya habari. huyu Eyadema ninamfahamu tu kwa mauhaji makubwa yaliondesha nchini kwake chini ya utawala wake. nitamwelezea zaidi Benjamini Mkapa wa Tanzania maana ndiye ninayemfamu vizuri huyu ni kiongozi mla rushwa mkubwa na siku zote ndani ya utawala alikuwa akiwazima watu wote waliokuwa wakijaribu expose rushwa mfano mzuri ni swala la GEN. ulimwengu alipojaribu ku expose ndani ya utawala alishambuliwa. Mkapa alivunja haki za binadamu kwa kutuma vijana wake Zanzibar mara baada ya uchaguzi na kuuwa watu wasiokuwa na hatia, watu wale waliuawa kwa kuamua kutumia haki yao ya kidemokrasia kwa kuandamana na Mkapa aliamuru watu wale adhabu yao kuwa ni kifo. kuhusu uchumi mkapa alitekeleza sera ya uwekezaji kwa kutumia cheo chake cha urais kujiuzia kiwanda cha coal kwa bei karibu na bure na pia kuingiiza nchi katika mikataba ambayo imelitumbukiza taifa letu katika makubwa kwa tamaa yao ya kupenda rushwa na kuweka maslai ya taifa pembeni. Benjamin Mkapa kwa mtazamo wangu mimi kama mtanzania niliyeishi ndani ya utawala wa miaka 10 hafai hata kufikiriwa kutunukiwa kikombe licha ya hayo mamilioni ya dola. Benjamini mkapa angekuwa anaishi katika nchi zenye utawala wakueshimu sheria angekuwa jela kwa kutumia ofisi vibaya na kushiriki katika ulaji wa rushwa wa kupindukia.
ushauri wangu kwa vyombo hivi vya nje, please kabla hamjamfikiria kumpa mtu tuzo lolote nendeni kwenye nchi usika mkaongee na hao aliwaongoza ili kupata maoni na siyo kusoma vitabu au majarida feki wanayoandika kuhusu kukua kwa uchumi au kuleta demokrasia.

na nick, Tanzania, - 21.10.08 @ 09:44 | #49421

Mkapa haitaji hizo zawadi. alikwisha jilipa mwenyewe mara kadhaa hizo. Katika himaya ya yamafisadi kila mmoja anajilipa kadriya madaraka yake. Mo asipoteze wakati wake kuanagalia Afrika Mashariki. Huku kazi moja tu! Kukupua kila nafasi inapotokea. Huku Wizi ni halali.

na Mchora, Kibaha, - 21.10.08 @ 09:45 | #49422

Katika jukwaa la siasa Mkapa hapaswi kufikiriwa kupewa zawadi ila kufikishwa mahakamani.Mkapa ndio chanzo cha ufisadi Tanzania.Kikishika chama ambacho kinajali Watanzania lazima Mkapa na JK waende Lupango.

na OLE LETIPIPI, TANZANIA, - 21.10.08 @ 09:55 | #49426


Benjamin Mkapa ktk utawala alitumia kila nafasi aliyonayo kudidimiza demokrasia ndani ya nchi kwa kulitumia jeshi la polisi kukandamiza demekrasia na pia kutumia swala la usalama kama EXCUSE ya kuwanyima wapinzani haki yao ya kikatiba ya kukusanyana na kutoa maoni yao. Benjamini mkapa alikuwa adui mkubwa wa demokrasia .
kuhusu uhuru wavyombo vya habari ndani ya utawala wake alifungia magazeti likiwemo majira na mengineyo kwa kuandika habari ambazo akuzipenda.
aliakikisha waandishi wote ambao wanamkosoa wanachukuliwa hatua mfano mzuri ni General Ulimwengu wa RAI.
KWAHIYO BENJAMIN MKAPA HAFAI kufikiriwa kupewa TUZO yeyote ile nje na ndani ya Tanzania ambapo ametuibia pesa chungu nzima kwa kutumia makampuni ya kutoka south afrika kukusanya mapato kwa kumtumia mwanae Nicholous Mkapa.

na nick, Tanzania, - 21.10.08 @ 10:03 | #49433

Jamani hii ni Taasisi huru kama kweli tunataka maoni yetu yazingatia, basi kama una ushahidi hata wa kimazingira ukimtumuhumu rais yeyote mfano Mkapa unaweza kutuma tuhuma hizo ktk taasisi hiyo na wao huzifuatilia kwa kufanya uchunguzi kwa njia wanazozifahamu. Tukifanya hivyo tutakuwa tumetimiza wajibu wetu.

1. Kwa mfano Mkapa tunamtuhumu kwa kuviza demokrasia na pia kuua wananachi kule Pemba wasio na hatia.
2. Kujiuzia mgodi wetu wa makaa ya mawe wa kiwira kwa bei ya kutupwa
3. Mkitaba mibovu ya wawekezaji ambayo hadi leo inatutesa kiuchumi.
4. Kula pesa yetu ya kupambana na malaria aliyochangiwa na Mariah Cariah

Hizi zote ni tuhuma mimi nilizituma huko kwenye taaisis ya MO Ibrahimu huenda ndio maana hakupata hiyo tuzo

na Ron, Tz, - 21.10.08 @ 10:07 | #49436

Hebu acheni hizo bwana, tatizo Watanzania mnakariri, kuambiwa Mkapa ana kosa flani basi mnafuta mazuri yote aliyoyafanya!! huu ni unafiki wa chura..ambaye ukimwangalia kwa nyuma huonekana amekaa na ukimwangalia kwa mbele ni kama amesimama! sasa nyie haueleweki, 2005 mlivaa tshirt za ccm na kumbeba huyu bwana mdogo kikwete..leo amekuwa mzito baada ya kula misosi ya ikulu mnahaha kumtua anashindikana, acha awavunje shingo!

kama watanzania hatutakiwi kumbeza Mkapa hivi, amefanya makubwa mengi ukimlinganisha na waliomtangulia na huyu kijana aliyemfuata, hivi mnajua hata hizi barabara na majengo yote muhimu yanayomalizika sasa hivi nchini yalianzishwa katika kipindi cha Mkapa, huyu Kiwete wenu anapumulia kwenye mgongo wa huyo Mzee.

Hebu tuwe tunatoa hoja za msingi sio kufuata mkumbo bila kujua mtokapo na muendako.

After all kupata tuzo sio lazima, inawezekana alijitahidi kufanya vizuri lakini wenzie walifanya vizuri zaidi..! kwani ni ugomvi, au kawambia ameumia! jifunzeni kujenga hoja sio mnabwabwata kama bata paratatatatatata..!

na Rodney Moses, DSM,TZ, - 21.10.08 @ 10:36 | #49449

Ndugu Ron umefanya jambo la busara sana, Huyu Nyoka Cobra Mkapa anastahili kupewa zawadi ya kuwa KEKO tu na wauwaji wenzake . Namalizia kwa Kumwomba Bwana Mungu Amani iwe nawe.Shukrani

na kisisina, zimbabwe, - 21.10.08 @ 10:42 | #49453
 
hii award ina mapungufu makubwa sana... kama alikosa mwaka jana iweje awe tena kwenye kuiwania? hii award haitakiwi kuotolewa kila mwaka maana mwisho wa siku watakuwa wameisha marais bora naitaenda kwa ambae hafai. inatakiwa itolewe labda kila baada ya miaka mitatu ili tuwe tumepata wastaafu wapya.... na ikiwezekana mara nyingine mshindi akosekane
 
Nakumbuka Museven alisema hiyo zawadi haitaki kwa sababu anauwezo wa kupata hizo hela akiendelea kuwa rais indefinitely! Wakimpa Mkapa wa TZ tutaandamana! Surprisingly anaweza kupata mwakani! Unajua Mogae alikosa last year, alikuwa wa pili baada ya Chissano na Mkapa alikuwa wa tatu!

Mogae alikuwa hajastaafu mwaka jana.Mkapa mwakani hatakuwemo kwenye kinyang'anyiro hiki.
 
The fact Mkapa amekuwa akitajwa tajwa na kukosa kwa points chache hii inathibitisha alikuwa kiongozi mzuri.

Kwa kadiri mambo yanavyo unfold Tanzania hivi sasa kidogo kidogo Mkapa atapata heshima anayostahili.

Kweli nabii hakubaliki kwao!
 
Kwa kadiri mambo ynavyo unfold Tanzania hivi sasa kidogo kidogo Mkapa atapata heshima anayostahili.

Mkuu Masatu,

Heshima mbele, hivi unafikiri aliwaachia Mtandao kwa bahati mbaya? Hapana alijua kuwa yataishia kua haya yanayo-unfold sasa na jina lake halitakuja kufunikwa kisiasa, kama vile Mwalimu alipomuachia Mwinyi, au?
 
of all the people benjamini mkapa? GOD IS GREAT, kwendelea kutajwa kwake si kwa bahati mbaya, kwani hata hiyo taasisi inataka kujua nini maoni ya watanznia dhidi ya bokasaa wao mkapa
 
The fact Mkapa amekuwa akitajwa tajwa na kukosa kwa points chache hii inathibitisha alikuwa kiongozi mzuri.

Kwa kadiri mambo yanavyo unfold Tanzania hivi sasa kidogo kidogo Mkapa atapata heshima anayostahili.

Kweli nabii hakubaliki kwao!

Masatu, najua wewe ni mpiga debe mzuri tu wa Serikali za CCM lakini inapofika suala la uzalendo/utaifa ningekuomba uweke mbali mapenzi yako kwa Vyama na kutanguliza utaifa. Kwa yote mabaya Mkapa aliyofanya yaweza kuwa mapungufu ya kibinadamu maana hakuna aliye mkamilifu, lakini inapofika kuwa implicated kwenye hujuma ya kujiuzia Kiwira Coal Mine (wizi) kwa bei chee hapo inakuwa ngumu kusema kuwa huo ni upungufu wa kibanadamu maana hiyo ni hujuma kwa Uchumi wa Taifa na Watanzania.

Nikuulize swali; Je, Mkapa amekanusha hiyo tuhuma ya kujiuzia KCL na kama amekanusha hivi ni kweli kuwa KWL si mali yake? Kama angejiuzia kwa bei ya soko (kitu ambacho ni kinyume cha maadali ya uongozi) tungeweza kusema kuwa bado alikuwa kiongozi mzuri. Tena unakumbuka mauaji ya Pemba Zanzibar baada ya Uchaguzi wa 2000? Unajua kuhusu uchaguzi wa Zanzibar ulivyoendeshwa na hata kupigiwa kelele na Waangalizi wa Kimataifa na wa ndani kuwa haukukidhi matakwa ya kuwa Uchaguzi huru na wa Haki? Uongozi bora wa Mkapa uko wapi hapo? Kwenye kuruhusu kuchotwa kwa mabilioni ya EPA kugharamia kampeni za CCM?

Pili, hata hivyo sitashangaa siku akija kupata hiyo tuzo maana kwa kawaida wanaotoa hiyo tuzo si Watanzania na uzoefu unaonyesha kuwa ni Wafadhili na Watu wa nje ndiyo huwasifia viongozi wetu (hawawajui sana) nao viongozi wetu hulenga kujionyesha kwa watu wa nje kuwa wao ni viongozi bora ili kuwapendeza hao Wafadhili wao.
 
Mkapa akosa tena mabilioni

na Mwandishi Wetu
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

Please delete
 
pamoja na propaganda zote bado MZEE BEN ni kifaa katika historia ya utawala wenye mafanikio hapa nchini. kuingia kwake kwenye kinyanganyiro hicho na kutajwa kama mshindani makini kwa kirefu na vyombo mbali mbali ni historia na alama ya mafanikio kwake kama kiongozi na taifa aliloliongoza.

Mzee Ben rekodi yake ni ya kujivunia, ushahidi upo machoni mwa jamii makini. barabara, shule, huduma za serikali, economic reforms, revenue growth....

media zetu badooooooooo....au uchambuzi dhaifuuuuu.
chuki za kisiasa kwa huyu mzee zimebackfire mapemaaaaa,
 
Ukiangalia utendaji kazi wa mzee Ben mtakubaliana na mimi kuwa JK hatii mguu hata 1/3 jamaa amemwacha mbalia kabisa..Naona jamaa ataanza kujivunia kwa kumaliza kujenga daraja la Ruvu.Barabara nyingi alizo mwachia Mzee Ben mpaka kesho hazijakamilika.
Kweli Ben nakubali alikuwa kichwa katika utendaji aliye mwangusha na kumponza ni mke wake tu.
Kwa nini jamaa asimrudishe Magufuli kwenye miundo mbinu kama alivyo fanya Ben?Au naye kambi ya Sumaye?
 
ZAWADI ambazo zinatolewa na Mo Ibrahim, muanzilishi wa Celtel zina maana nyingine ambayo haisemwi sana.

Nayo sio nyingine ni kwamba sisi waafrika Mashariki ni wababishaji, wagandamizaji na wasanii wa demokrasia na maendeleo ya kweli ya watu wetu.

Kwa maneno mengine kushindwa kupata zawadi hiyo ni kwamba viongozi wetu ni wabovu; rushwa iko juu; haki ina walakini; na uwazi na ukweli hamna kabisa.

Lakini hili ni jambo la kuhuzunisha sana maana kwa kweli tuna mazingira mazuri tu ya kushinda zawadi hiyo ili mradi tuache ukora, ubinafsi, ubabe na uchama unaozidi kipimo!
 
Back
Top Bottom