Salaam, Shalom!!
Nchi yetu imeng'ara tena katika bara la Afrika baada ya kijana Mahiri, ndugu Yeriko Nyerere kutuletea Tuzo Bora kabisa ya uandishi Bora wa vitabu kwa Afrika nzima.
Tuzo hiyo imetolewa na Taasisi iitwayo, ZIKOMO AFRICA AWARDS yenye maskani yake nchini Zambia iliyotokewa November 2023, Yericko Nyerere akiwa mtanzania pekee aliyechaguliwa kushiriki.
Tuzo hiyo imekuja miaka 6 baada ya kitabu alichoandika ndugu yetu Yeriko Nyerere juu ya Ujasusi wa kidola na kiuchumi.
Ujasusi kidola katika Usalama kama nchi tupo vizuri, Hilo halipingiki, ila Ujasusi kiuchumi, naona Bado tunasuasua. Ikiwa kitabu hiki kingesomwa na wataalamu wetu wa Uchumi Kwa kipindi Cha miaka 6 iliyopita na kifanyiwa KAZI, naamini tusingekuwa hapa tulipo.
Yaani ndugu Philip Mpango na ndugu Mwigulu nchemba, wangechukua haraka ushauri na madini katika kitabu cha mtanzania mwenzetu, tusingekuwa Bado tunafanya na kupita njia tunayopitia kiuchumi.
Tungesoma kitabu hiki kisawa sawa, tusingekubali kukodisha Bandari zetu kwa wageni, kuuza misitu na madini kiholela.
Najua hatujachelewa, tunaandika Katiba mpya, pia tunaelekea Uchaguzi, vyama vinaandaa Ilani zao Kwa mwaka 2025-2030, chonde chonde, msiache kuchungulia kitabu hiki Hasa kuhusu Ujasusi wa kiuchumi, kuona namna gani mtatoa dira nzuri kuhakikisha raslimali zetu zinatunufaisha na kututajirisha Watanzania.
NB: Roho mbaya haijengi, linapokuja suala la Maslahi mapana ya nchi, tuwe kitu kimoja bila kujali, Yeriko Nyerere ametoka CHADEMA au la, Tanzania kwanza.
Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo Tanzania 🇹🇿.
Aamen.
Cc: Yericko Nyerere.
Nchi yetu imeng'ara tena katika bara la Afrika baada ya kijana Mahiri, ndugu Yeriko Nyerere kutuletea Tuzo Bora kabisa ya uandishi Bora wa vitabu kwa Afrika nzima.
Tuzo hiyo imetolewa na Taasisi iitwayo, ZIKOMO AFRICA AWARDS yenye maskani yake nchini Zambia iliyotokewa November 2023, Yericko Nyerere akiwa mtanzania pekee aliyechaguliwa kushiriki.
Tuzo hiyo imekuja miaka 6 baada ya kitabu alichoandika ndugu yetu Yeriko Nyerere juu ya Ujasusi wa kidola na kiuchumi.
Ujasusi kidola katika Usalama kama nchi tupo vizuri, Hilo halipingiki, ila Ujasusi kiuchumi, naona Bado tunasuasua. Ikiwa kitabu hiki kingesomwa na wataalamu wetu wa Uchumi Kwa kipindi Cha miaka 6 iliyopita na kifanyiwa KAZI, naamini tusingekuwa hapa tulipo.
Yaani ndugu Philip Mpango na ndugu Mwigulu nchemba, wangechukua haraka ushauri na madini katika kitabu cha mtanzania mwenzetu, tusingekuwa Bado tunafanya na kupita njia tunayopitia kiuchumi.
Tungesoma kitabu hiki kisawa sawa, tusingekubali kukodisha Bandari zetu kwa wageni, kuuza misitu na madini kiholela.
Najua hatujachelewa, tunaandika Katiba mpya, pia tunaelekea Uchaguzi, vyama vinaandaa Ilani zao Kwa mwaka 2025-2030, chonde chonde, msiache kuchungulia kitabu hiki Hasa kuhusu Ujasusi wa kiuchumi, kuona namna gani mtatoa dira nzuri kuhakikisha raslimali zetu zinatunufaisha na kututajirisha Watanzania.
NB: Roho mbaya haijengi, linapokuja suala la Maslahi mapana ya nchi, tuwe kitu kimoja bila kujali, Yeriko Nyerere ametoka CHADEMA au la, Tanzania kwanza.
Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo Tanzania 🇹🇿.
Aamen.
Cc: Yericko Nyerere.