Tuzo Ndg. Yeriko Nyerere itupe funzo kuthamini 'big brains' wa ndani ya nchi

Rabbon

JF-Expert Member
Apr 16, 2022
15,103
22,547
Salaam, Shalom!!

Nchi yetu imeng'ara tena katika bara la Afrika baada ya kijana Mahiri, ndugu Yeriko Nyerere kutuletea Tuzo Bora kabisa ya uandishi Bora wa vitabu kwa Afrika nzima.

Tuzo hiyo imetolewa na Taasisi iitwayo, ZIKOMO AFRICA AWARDS yenye maskani yake nchini Zambia iliyotokewa November 2023, Yericko Nyerere akiwa mtanzania pekee aliyechaguliwa kushiriki.

Tuzo hiyo imekuja miaka 6 baada ya kitabu alichoandika ndugu yetu Yeriko Nyerere juu ya Ujasusi wa kidola na kiuchumi.

Ujasusi kidola katika Usalama kama nchi tupo vizuri, Hilo halipingiki, ila Ujasusi kiuchumi, naona Bado tunasuasua. Ikiwa kitabu hiki kingesomwa na wataalamu wetu wa Uchumi Kwa kipindi Cha miaka 6 iliyopita na kifanyiwa KAZI, naamini tusingekuwa hapa tulipo.

Yaani ndugu Philip Mpango na ndugu Mwigulu nchemba, wangechukua haraka ushauri na madini katika kitabu cha mtanzania mwenzetu, tusingekuwa Bado tunafanya na kupita njia tunayopitia kiuchumi.

Tungesoma kitabu hiki kisawa sawa, tusingekubali kukodisha Bandari zetu kwa wageni, kuuza misitu na madini kiholela.

Najua hatujachelewa, tunaandika Katiba mpya, pia tunaelekea Uchaguzi, vyama vinaandaa Ilani zao Kwa mwaka 2025-2030, chonde chonde, msiache kuchungulia kitabu hiki Hasa kuhusu Ujasusi wa kiuchumi, kuona namna gani mtatoa dira nzuri kuhakikisha raslimali zetu zinatunufaisha na kututajirisha Watanzania.

NB: Roho mbaya haijengi, linapokuja suala la Maslahi mapana ya nchi, tuwe kitu kimoja bila kujali, Yeriko Nyerere ametoka CHADEMA au la, Tanzania kwanza.

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo Tanzania 🇹🇿.

Aamen.

Cc: Yericko Nyerere.
 
Kitabu kisomwe na wataalamu wa uchumi tungekuwa mbali???

Hivi wachagga wanasoma kitabu gani Cha uchumi?
Mtu anaandika kitabu Cha ujasusi wa uchumi wa academia !
Kuna kina mangi wako Dar es salaam stock exchange wanakimbiza ni Hatari ,hao ndio wafanye review ya hicho kitabu Kisha watushauri.
Mentorship mentorship mentorship
Huu ndio ujasusi wa kichagga.
Sio watu wa academia kupromote legacy ya mwalimu eti Yericko na kitabu chake na hata kiduka hajawahi miliki.
Good read though 🥴
 
Kongole kwako ndugu Yericko Nyerere.

Mungu akubariki, na Nchi ikutumie ipasavyo Kwa faida ya wananchi.
 
Salaam, Shalom!!

Nchi yetu imeng'ara tena katika bara la Afrika baada ya kijana Mahiri, ndugu Yeriko Nyerere kutuletea Tuzo Bora kabisa ya uandishi Bora wa vitabu Kwa Afrika nzima.

Tuzo hiyo imekuja miaka 6 baada ya kitabu alichoandika ndugu yetu Yeriko Nyerere juu ya Ujasusi wa kidola na kiuchumi.

Ujasusi kidola katika Usalama kama nchi tupo vizuri, Hilo halipingiki, ila Ujasusi kiuchumi, naona Bado tunasuasua. Ikiwa kitabu hiki kingesomwa na wataalamu wetu wa Uchumi Kwa kipindi Cha miaka 6 iliyopita na kifanyiwa KAZI, naamini tusingekuwa hapa tulipo.

Yaani ndugu Philip Mpango na ndugu Mwigulu nchemba, wangechukua haraka ushauri na madini katika kitabu Cha mtanzania mwenzetu, tusingekuwa Bado tunafanya na kupita njia tunayopitia kiuchumi.

Tungesoma kitabu hiki kisawa sawa, tusingekubali kukodisha Bandari zetu Kwa wageni, kuuza misitu na madini kiholela.

Najua hatujachelewa, tunaelekea Uchaguzi, vyama vinaandaa Ilani zao Kwa mwaka 2025-2030, chonde chonde, msiache kuchungulia kitabu hiki Hasa kuhusu Ujasusi wa kiuchumi,kuona namna Gani mtatoa dira nzuri kuhakikisha raslimali zetu zinatunufaisha na kututajirisha Watanzania.

NB; Roho mbaya haijengi, linapokuja suala la Maslahi mapana ya nchi, tuwe kitu kimoja bila kujali, Yeriko Nyerere ametoka CHADEMA au la.

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿.

Aamen
Wewe kenge ni miongoni mwa watu wapuuzi msiopenda kujisomea hata magazeti kama Mtanzania au Rai. Hiyo title ya kitabu isikutishe. Alichofanya Yeriko ni copy & paste ya makala za watu na kuziweka kwenye kitabu. Hakuna kitu alichotunga pale. Kwa waliosoma makala za Mzee Joseph Mihangwa wataona jinsi Yeriko alivyokopi makala nyingi za yule mzee na kuziweka kwenye kitabu chake bila ku-acknowledge. Kibaya zaidi amecopy kama zilivyo hadi nukta. Hata story za Habib Anga the Bold baadhi ziko kwenye hicho kitabu.

Kitabu chake ni cha hadithi na mchango wake ni kuburudisha tu wananchi. Yeriko angepewa tuzo ya mjasiriamali aliyetumia makala za watu kujiandikia kitabu na kuuza hila wahusika kunufaika.
 
Kitabu kisomwe na wataalamu wa uchumi tungekuwa mbali???

Hivi wachagga wanasoma kitabu gani Cha uchumi?
Mzanaki aliyekulia ktk pensheni ya Babu yake Leo anaandika kitabu Cha ujasusi wa uchumi wa academia !
Kuna kina mangi wako Dar es salaam stock exchange wanakimbiza ni Hatari ,hao ndio wafanye review ya hicho kitabu Kisha watushauri.
Mentorship mentorship mentorship
Huu ndio ujasusi wa kichagga.
Sio watu wa academia kupromote legacy ya mwalimu eti Yericko na kitabu chake na hata kiduka hajawahi miliki.
Good read though 🥴
Kwamba Yericko ni Mzanaki???

Nyie ndio mnajua Yericko ni mtoto wa Nyerere.

Huyo jamaa atawapeli mpaka siku atawafira.

Kweli fake it till you make it.
 
Wewe kenge ni miongoni mwa watu wapuuzi msiopenda kujisomea hata magazeti kama Mtanzania au Rai. Hiyo title ya kitabu isikutishe. Alichofanya Yeriko ni copy & paste ya makala za watu na kuziweka kwenye kitabu. Hakuna kitu alichotunga pale. Kwa waliosoma makala za Mzee Joseph Mihangwa wataona jinsi Yeriko alivyokopi makala nyingi za yule mzee na kuziweka kwenye kitabu chake bila ku-acknowledge. Kibaya zaidi amecopy kama zilivyo hadi nukta. Hata story za Habib Anga the Bold baadhi ziko kwenye hicho kitabu.

Kitabu chake ni cha hadithi na mchango wake ni kuburudisha tu wananchi. Yeriko angepewa tuzo ya mjasiriamali aliyetumia makala za watu kujiandikia kitabu na kuuza hila wahusika kunufaika.
Tuonyeshe copy ya kitabu Cha Yericko Nyerere ulichosoma na kugundua amecopy na kupaste.

Ama Kweli, Nabii hakubaliki nyumbani kwao!!
 
Kwamba Yericko ni Mzanaki???

Nyie ndio mnajua Yericko ni mtoto wa Nyerere.

Huyo jamaa atawapeli mpaka siku atawafira.

Kweli fake it till you make it.
Akiwa mtanzania pekee inatosha.

Tupendane Watanzania.
 
Back
Top Bottom