Mnyika tafadhali soma hii

Unaposema uongo tafuta unaofanana na uhalisia hata kama mtu humpendi, kwani inaonesha dhahiri ya kwamba umetunga!!
 
Kitu kimoja ninacho kipenda chuo kikuu cha HAVARD wanaamini juu ya utafiti na ndo maana kuna bango kubwa unapoingia chuoni hapo linalo someka hivi...VERITAS. Na wemeendelea pia kwenye logo yao. Hivo mtoa mada tuwekee ushaidi we need verification. Kama huna hili jukwaa si la majungu na madudu madudu!!!!!
 
Jamani mimi naomba watu wenye upeo mdogo unaofanana na vyeo vya akina tambwe hizza wapishe mapema, pia wewe unayewaambia watu wametumwa acha upofu wa maono,sio kila jambo ni lazima liwe zuri kwa chadema, yaani unanishangaza sana,kila jambo linaloikosoa cdm unasema wametumwa wewe sio mwanachadema kabisaaa,hata ukiwa na kadi basi ww ni wenye uono mfupi na hutafanikiwa katika haya...sikia kila jambo na ujenge hoja.
 
Kipindi cha daladala hakirushwi na ITV bali ni TBC1.Kwa hiyo hata habari yako ni ya uongo kuanzia taarifa ya tv ..husika

Hapa umekosea wameisha hama TBC kipindi sana ...kaka kuwa makini kabla ujapost na wewe ni mpotoshaji!!
 
Kama kuna mtu anafahamu kilichosemwa kwa ukamilifu wake kwenye kipindi cha Daladala kilichotajwa pamoja na Clouds TV tafadhali naomba anijulishe kupitia johnmnyika@gmail.com au aandike hapa ili nikirejea Tanzania niweze kuchukua hatua. Siku njema

JJ
Mnyika achana na upuuzu huu tushugulikie kero zetu! sisi wakazi wa MISUMI karibu na PANDE hatuna maji, barabara ya kutokea MADALE haipitiki na pia umeme hatuna. Tushugulikie please ili ikifika 2015 tuone kuna kazi hata sisi wa MBEZI MISUMI UMETUJALI!!1
 
Mimi siwapendi CDM ila pia sipendi hii tabia ya kuzushia watu hata kidogo.

Uliyeandika haya njoo utupe majibu baada ya kujibiwa na haswa uliposema kuwa asome , amesoma na amejibu sasa unapotelea wapi
kama hutokuja tutakusomea Albadir ijumaa ijayo.
 
Juzi nikiwa natizama kipindi cha daladala kinachorushwa na itv kila siku saa moja jioni.kuna tetesi mh. J.mnyika umechukua ela kutoka kwa magari ya maji taka ili yaendelee kumwaga maji taka hayo katika mabwawa ya kiwanda cha urafiki yaliyopo mabibo.je tuhuma hizi zina ukweli?tujulishe wapiga kura wako wa mabibo.

Mbona yote unayosikia husemi humu? Mbaya zaidi siyo hoja yako umesikia na sisi tumesikia. Pateni muda wa kutafakari kabla hatua ya pili haijachukuliwa mnaonekana wazushi!
 
Tangu lini mnyika kawa mkurugenzi wa Kinondoni. Hii ni kazi ya serikali. Mnatupotezea muda.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom