Crashwise
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 22,227
- 8,760
Kushindwa kwa kiongozi kuna weza kukawa na sababu nyingi..Mosi nimekwambia chadema hatukuwekeza nguvu mikoa ya pwani hivyo hatukuwa na misingi, pili kutoa kiongozi Mwanza akaongoze Mtwara hili halija kaa vizuri sana ukumbuke chama chetu hakijajitoshereza muda mwingi watu wanafanya kazi za siasa kwa kujitolea zaidi sasa ukimwambie atoke mwanza aende Mtwara maana yake nini? naona tu tuendelee kutumia viongozi wa maeneo husika siamini kabisa kuwa mtwara au kusini hakuna mtu anae faa kuongoza kanda hizo bali naamini ama hawajafanya mafunzo ya kutosha kitu ambacho baada ya kuzinduliwa mafunzo yatafanyika kuanzia juu mapaka matawi maana sitegemei tena kuwa ccm watapiga marufuku siasa mikoa hiyo...Haya ndo maelezo yanayotakiwa nashangaa kuna watu wengine badala ya kuleta hoja wanaanza kashifa za kijinga... sijui ni lini watakuja kukubali kwamba haiwezekani wakati wote watu wawe na mawazo yanayofanana na pale unapotoa mawazo tofauti na wao unaanza kukashifiwa!
Tukija upande wa Mtwara, kama umenisoma visuri hakuna popote nilipoitaja Mtwara lakini nimezungumzia Kusini kwa ujumla! Tena, pamoja na ile hoja ambayo tuliijadili kwa kina na wewe mara ya kwanza, kuna siku nilizungumzia ni watu wa aina gani wanapaswa kutia nguvu mikoa ya Kusini na maeneo yale ambayo uungwaji mkono bado ni mdogo! Kwangu mimi bado naamini kwamba kuna baadhi ya watu wana influence kubwa kuliko wengine... na kwamba, bado naamini watu kama akina Mnyika wenye ushawawishi wanaweza kuwekeza nguvu zao huko bila kuathiri utendaji wa kila siku wa Makao Makuu! Hoja ikiwa kwamba, viongozi wa CHADEMA Kanda ya Kusini tayari wameshashindwa kazi kwahiyo, wala hapakuwa na ubaya wowote wa Kanda sawa na hiyo kuongozwa na Wa-CHADEMA wengine wenye influence hata kama sio wakazi wa huko! Huwezi kumchukua mtu ambae ameshindwa kueneza chama over the past 10 years halafu tena unampa Ukurugenzi wa Kanda au kitu kinachofanana na hicho coz' hapo awali alishindwa si kwa sababu hapakuwa na kanda bali ni incompetent!
mangine tuendelee kuvumiliana.....