Mnyika jimbo la Ubungo umeshalikosa

Mnyika jimbo la Ubungo umeshalikosa

umeugusa ukweli wa rohoni na ndiyo maana nina jakamoyo sana nikiona wanasema hawatampa eti sababu ya maji lkn amini usiamini....................na wameshau kwamba maji hayajakauka wakati wa Mnyika, tatizo la maji Kimara lina umri sawa na Jimbo lenyewe

Mnyika atashinda kwa kishindo,hiyo haina ubishi,bila Mnyika Ubungo ilikuwa ni jehanum Mnyika katufungua macho.Hatutaki wabunge ambao hawana msaada kwetu.Mnyika For Ubungo
 
Kete ya Maji Ubungo akina Mnyika imewapa credity kubwa sana watu wanajivunia Mnyika.Waulize wamama wa Ubungo watakwambia kuhusu Mnyika
 
Gongolamboto kuna maji?....mnyika anafanya kazi sana...tumekuwa tumkimsikia akipiga kelele kuhusu maji ubungo...lk serikali ya ccm haitaki kupeleka huduma hiyo sio ubungo tu.ni Tanzania. nzima. Soln...2015 husiichague CCM....chagua ukawa....allafu..ndipo uje kumuhoji mnyka
 
Nani unafikiri ukimchagua atakupa maji?

Nadhani wakimchagua Mbunge wa ccm watapata maji. Kwani serekali itaundwa Na ccm, nao hawatamtupa Mbunge wao. Na watamsaaidia kutafautisha kipindi cha Utawala wa CDM jimboni na wakwao. So the choice has to be the ruling party.
 
Muheshimiwa wakati wa kampeni ya uchaguzi 2010 ulituahidi kuwa utamaliza kero ya maji Ubungo, tukakupa kura zetu. Tukakesha wote pale loyola kuhakikisha kura hazichakachuliwi, peoplez power tukalibeba na kulipindua gari la wizara ya mambo ya ndani wakati lilipolazimisha kuingia pale getini mimi Dar es salaam nimekuja mwaka 90 nilifikia Gongolamboto ambapo nakumbuka tulikuwa tunakunywa maji ya kisima na yenye chumvi.

Niliendelea kunywa maji ya chumvi mpaka mwisho wa miaka ya tisini ndiyo ilikuwa mwisho wa kunywa maji ya chumvi..leo karne ya 21 miaka 50 ya uhuru kwa mara ya kwanza na kunywa maji ya chumvi. Kweli tunasifu juhudi zako za kufichua maovu huko bungeni lakini kura zetu sahau. Umeshindwa kusoma alama za nyakati kwamba wakuu wamekuundia zengwe Ubungo pasipatikane maji ili uonekane hufanyi chochote. Ungeweza hata kuleta maji ya kununua kwenye malori tunge appriciate uwajibikaji wako sasa huku maji hakuna hata ya kununua hakuna. Ukipata ubunge 2015 walahi natembea uchi. "maana tumechoka sasa"

Kumbe unalifahamu hilo la kumletea zengwe unalalamika nini hata wewe ukipewa ubunge leo hutaweza kuwatimizia wapigakura wako yoto,nakushauri usikate tamaa Peoplessssss
 
Nadhani wakimchagua Mbunge wa ccm watapata maji. Kwani serekali itaundwa Na ccm, nao hawatamtupa Mbunge wao. Na watamsaaidia kutafautisha kipindi cha Utawala wa CDM jimboni na wakwao. So the choice has to be the ruling party.

Kama hiyo ndo sababu basi jimbo la Ubungo lingekuwa linatiririka maji mpaka yanamwagika.Hivi unajua shida waliyokuwa wanapata wanaubungo kabla ya Mnyika? Unajua wewe kweli.Ubungo ipo chini ya CCM toka Uhuru halafu useme leo CCM itarahisisha upatikanaji wa maji,you must be joking
 
watu wa jimbo la ubungo punguzeni uoga. Unganeni muandamane kwenda makao makuu ya wizara ya maji yalipo hapo ubungo kwa lengo la kumwambia magembe na makala waamue moja, la kufungulia maji au wawape ruhusa ya kulitoboa bomba linalopita jimboni kwenu ili mjichotee bila malipo.
Mnyika mtamwonea bure kwani aliipeleka hoja binafsi ya kuitaka serikali iseme ni lini jiji la Dar litapata maji ya uhakika lakini ccm waliipoka hoja ile na kuifanya ya kitaifa.
Kukosa kwenu maji ni mbinu za ccm kumdhoofisha Mnyika kwani ni mwiba unaowachoma sana bungeni hata Makinda anamwogopa. Si ndiye aliyemwita mkulu dhaifu?. Dogo ni jembe acheni kumharibia, give him another chance na kayapasueni bomba mkinge maji ili magembe aumie kwa hatua mlizochukua.



Naunga mkono hoja yako mkuu,Mnyika kama Kiongozi ameshafanya sehemu yake,kilichobaki ni kwa Wananchi kuchukua hatua kuishinikiza serikali itende!!

Mnyika ni mjakazi tu wa wakazi wa Ubungo,tumemtuma na salamu amezifikisha,sasa unapomtuma mtu halafu ambaye umemtuma Kwake asipofanya maagizo yako huyu ndiyo ww unatakiwa kumchukulia hatua!! Kumchukulia hatua "Messenger " ni aidha kukosa Hekima au Woga tu
 
yaani mimi (mlete mada ) siongelei kwa ushabiki wa chama nazungumzia ahadi alizozitoa huyu mheeshimiwa mpaka tuka mpa kura zetu, tukakesha naye pale loyola, tukalivunja vunja gari la wizara ya mambo ya ndani kwa imani kuwa lilikuwa limejakuharibu matokeo.....leo ni mwezi wa pili ubungo tunanunua maji ndoo sh 1000 tena hapa mtaani kwetu kuna tajiri mmoja ndio analeta kwenye malori...vinginevyo utatumia ya chumvi sasa kama huyu tajiri wa hapa mtaani pamoja na kwamba anatuuzia maji lakini amekuwa msaada mkubwa sana yeye sio mwanasiasa Mnyika mwenye jimbo lako umeshindwa kweli kutafuta lori kumi za maji hata ukawa unatuuzia kwa sh 500 kwanza utapata faida pili utatuletea ahueni kwenye hili swala la maji, mchango wako bungeni ni mkubwa lakini jimboni hamna anayekuelewa...unahangaika na mambo makubwa mara katiba mara ufisadi wakati jimboni hamna
maji...watakuuua bure..kuwa mbunifu nunua malori kumi ya maji pitisha mitaani uzia wananchi kwa bei nafuu kidogo kwanza utapata faida kisha watu tunaweza kurudisha imani.

Naona unamfundisha maisha Mh.nani kakwambia ana hela ya kununua Lori kumi?
 
wacheni kumpa tumaini mnyika, nimefanya kautafiti hasa kwa wanawake wamesema hawampi

huku ubungo wanaochota maji ni mabeki tatu na vijana wa mikokoteni. unazungumzia wsnawake wapi?
 
[h=3]MAELEZO NA HOJA BINAFSI YA KUPENDEKEZA BUNGE LIJADILI NA KUPITISHA MAAZIMIO YA HATUA ZA HARAKA ZA KUBORESHA UPATIKANAJI WA MAJI SAFI NA USHUGHULIKIAJI WA MAJI TAKA KATIKA JIJI LA DAR ES SALAAM KWA MUJIBU WA KANUNI YA 54 FASILI YA (1) YA KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE TOLEO LA MWAKA 2007.............................................
Maji ni uhai, hivyo matatizo ya upatikanaji wa maji safi na ushughulikiaji wa maji taka katika Jiji la Dar es salaam na nchini kwa ujumla kama hatua za haraka zisipochukuliwa yatageuka kuwa janga la taifa. Katika kila watanzania katika Jiji la Dar es Salaam na nchini; kwa wastani mmoja hapati huduma ya maji safi na salama na hali ni mbaya zaidi kuhusu ushughulikiaji wa maji taka.

hata kama hakufanikisha lakini nia na dhati alikuwa nayo, nitaungana na wewe katika kutetea kiti chako 2015.[/h]
 
Ubungo tumesha mkabidhi mnyika ata akisimamisha jiwe akaliandika mnyika linapita bila kupigwa
 
Muheshimiwa wakati wa kampeni ya uchaguzi 2010 ulituahidi kuwa utamaliza kero ya maji Ubungo, tukakupa kura zetu. Tukakesha wote pale loyola kuhakikisha kura hazichakachuliwi, peoplez power tukalibeba na kulipindua gari la wizara ya mambo ya ndani wakati lilipolazimisha kuingia pale getini mimi Dar es salaam nimekuja mwaka 90 nilifikia Gongolamboto ambapo nakumbuka tulikuwa tunakunywa maji ya kisima na yenye chumvi.

Niliendelea kunywa maji ya chumvi mpaka mwisho wa miaka ya tisini ndiyo ilikuwa mwisho wa kunywa maji ya chumvi..leo karne ya 21 miaka 50 ya uhuru kwa mara ya kwanza na kunywa maji ya chumvi. Kweli tunasifu juhudi zako za kufichua maovu huko bungeni lakini kura zetu sahau. Umeshindwa kusoma alama za nyakati kwamba wakuu wamekuundia zengwe Ubungo pasipatikane maji ili uonekane hufanyi chochote. Ungeweza hata kuleta maji ya kununua kwenye malori tunge appriciate uwajibikaji wako sasa huku maji hakuna hata ya kununua hakuna. Ukipata ubunge 2015 walahi natembea uchi. "maana tumechoka sasa"

Tutaanza kufichua mabilioni yaliyotengwa kwa ajili ya maji yanavyotumika vibaya.

Kwanza kuna pesa za MCA (Milennium Challenge AccounT) kama ambavyo mradi unajieleza kwenye website ya serikali.
attachment.php


Hizi ilipewa wizara ya fedha moja kwa moja. Je, Mnyika atafute nyingine na kuanza project mpya?

Alipopelekwa hoja yake binafsi ya kufuatilia mradi huu, Waziri alimzima, wote tunakumbuka.

Waziri mwenyewe alituambia kuwa kuna fedha hii kwenye bajeti ya 2012/13 Namnukuu hapa

Serikali yatenga mabilioni kugharimia maji.WIZARA ya Maji jana iliwasilisha makadirio yake ya matumizi kwa mwaka 20012/2013 bungeni ambayo yanaonyesha kuwa imetenga Sh465.756 bilioni kwa ajili ya miradi ya maendeleo.Akiwasilisha bajeti hiyo, Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe alisema kati ya fedha hizo, Sh140.015 bilioni ni za ndani na Sh325.740 ni fedha kutoka nje.
Profesa Maghembe alisema kwa ujumla wake, wizara yake inakusudia kutumia Sh485.898 bilioni, kati ya hizo matumizi ya kawaida ni Sh20.142 bilioni.
Alisema miongoni mwa kazi ambazo wizara hiyo imepanga kuzitekeleza ni pamoja na maeneo yanayofaa kuchimba visima virefu na kusimamia uchimbaji kwa maeneo 630 katika sehemu mbalimbali nchini.
"Mwaka 2012/2013, kupitia Bajeti ya Serikali, Sh51.9 bilioni kutoka mfuko wa pamoja zimepangwa kugharimia ujenzi wa miundombinu ya maji, kujenga uwezo wa watekelezaji wa programu, uhamasishaji, kutoa elimu ya usafi na mazingira, ufuatiliaji na kulipa wataalamu washauri kwa ajili ya usimamizi wa makandarasi," alisema Profesa Maghembe na kuongeza:
"Kiwango hicho cha fedha kilichotengwa ni sehemu ya Sh81.8 bilioni ya mchango wa Serikali na ahadi ya Washirika wa Maendeleo."
Alisema Serikali inaendelea kutekeleza Mpango wa Dharura wa Kuboresha Huduma ya Maji katika Jiji la Dar es Salaam na Miji ya Kibaha na Bagamoyo ambao unalenga kuongeza uwezo wa uzalishaji wa maji kutoka mita za ujazo 300,000 kwa siku hadi mita za ujazo 710,000 siku ifikapo 2014.
Profesa Maghembe alisema mpango huo unatekelezwa kwa ushirikiano baina ya Serikali ya Tanzania na Shirika la Marekani la Changamoto za Milenia (MCC), Serikali ya Norway, Serikali ya India na washirika wengine wa maendeleo kupitia Mfuko wa Pamoja wa Maji.
"Utekelezaji wa Mpango huo ulianza rasmi Februari 2011 na umepangwa kukamilika Desemba 2014 na utagharimu Sh653.9 bilioni," alisema Profesa Maghembe.
Watanzania tumekuwa wajinga. Mahali ambapo uzembe uko wazi tu, tunaleta siasa eti kuadhibu upinzania.

Mimi ntaanza kulikuza hili, nahisi kuna uchafu kama wa EPA na ESCROW.

Kwa nini Maghembe alizima hoja binafsi ya Mnyika?

Kwa nini team Lumumba inaitumia hii kama propaganda ya kumchafua Mnyika?

attachment.php

attachment.php


Tatizo si kuwa pesa hakuna, tatizo zimetumikaje?

Baada ya Escrow mnaonaje tulikuze hili limtikise Maghembe?

Kwa kweli Mnyika anachukiwa na CCM kwa jinsi anavyohoji mambo
 

Attachments

  • maji ruvu chini.PNG
    maji ruvu chini.PNG
    26.2 KB · Views: 2,132
  • maji ruvu-chini.PNG
    maji ruvu-chini.PNG
    30.3 KB · Views: 2,079
Nadhani wakimchagua Mbunge wa ccm watapata maji. Kwani serekali itaundwa Na ccm, nao hawatamtupa Mbunge wao. Na watamsaaidia kutafautisha kipindi cha Utawala wa CDM jimboni na wakwao. So the choice has to be the ruling party.

Mbona Tabata tunae Makongoro mahanga wa CCM lakini hatujui kama dar kuna maji yasiyo ya chumvi....
 
Muheshimiwa wakati wa kampeni ya uchaguzi 2010 ulituahidi kuwa utamaliza kero ya maji Ubungo, tukakupa kura zetu. Tukakesha wote pale loyola kuhakikisha kura hazichakachuliwi, peoplez power tukalibeba na kulipindua gari la wizara ya mambo ya ndani wakati lilipolazimisha kuingia pale getini mimi Dar es salaam nimekuja mwaka 90 nilifikia Gongolamboto ambapo nakumbuka tulikuwa tunakunywa maji ya kisima na yenye chumvi.

Niliendelea kunywa maji ya chumvi mpaka mwisho wa miaka ya tisini ndiyo ilikuwa mwisho wa kunywa maji ya chumvi..leo karne ya 21 miaka 50 ya uhuru kwa mara ya kwanza na kunywa maji ya chumvi. Kweli tunasifu juhudi zako za kufichua maovu huko bungeni lakini kura zetu sahau. Umeshindwa kusoma alama za nyakati kwamba wakuu wamekuundia zengwe Ubungo pasipatikane maji ili uonekane hufanyi chochote. Ungeweza hata kuleta maji ya kununua kwenye malori tunge appriciate uwajibikaji wako sasa huku maji hakuna hata ya kununua hakuna. Ukipata ubunge 2015 walahi natembea uchi. "maana tumechoka sasa"


Yulambiwa kigoma itakuwa kama dubai

fly over kila kona

kilimo kwanza kiko wapi???

na vile vile mwenyekiti wenu alikuja kwa kasi zaidi nguvu mpya na ari mpya hahahahahaahahah

kaambulia richmond na escrow ila sijui kama........................

nadhani umeelewa
 
Tutaanza kufichua mabilioni yaliyotengwa kwa ajili ya maji yanavyotumika vibaya.

Kwanza kuna pesa za MCA (Milennium Challenge AccounT) kama ambavyo mradi unajieleza kwenye website ya serikali.
attachment.php


Hizi ilipewa wizara ya fedha moja kwa moja. Je, Mnyika atafute nyingine na kuanza project mpya?

Alipopelekwa hoja yake binafsi ya kufuatilia mradi huu, Waziri alimzima, wote tunakumbuka.

Waziri mwenyewe alituambia kuwa kuna fedha hii kwenye bajeti ya 2012/13 Namnukuu hapa

Watanzania tumekuwa wajinga. Mahali ambapo uzembe uko wazi tu, tunaleta siasa eti kuadhibu upinzania.

Mimi ntaanza kulikuza hili, nahisi kuna uchafu kama wa EPA na ESCROW.

Kwa nini Maghembe alizima hoja binafsi ya Mnyika?

Kwa nini team Lumumba inaitumia hii kama propaganda ya kumchafua Mnyika?

attachment.php

attachment.php


Tatizo si kuwa pesa hakuna, tatizo zimetumikaje?

Baada ya Escrow mnaonaje tulikuze hili limtikise Maghembe?

Kwa kweli Mnyika anachukiwa na CCM kwa jinsi anavyohoji mambo



lipua magamba 100 ni sawa na chadema 1
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom