Mnyika jimbo la Ubungo umeshalikosa

Mnyika jimbo la Ubungo umeshalikosa

Du! Mbona mnahasira sana na mbunge wenu tulieni dawa iingie nani aliwatuma kuchagua maharage ya mbeya.
 
Swala la maji dar siyo ubungo pekeyake, ni dar karibia yote. Huko Gongo la mboto alipopataja au Ukonga nzima haina maji ya bomba... Hapa tukubaliane tatizo ni serikali yetu, uliza wilaya au majimbo yote ya dar yana maji, au wewe shida yako ipi kwa mh Mnyika? ??
Mnyika alisema ataleta maji imekuwaje mbona mnakimbia hoja?
 
Maji yamemshinda sasa amehamia kwenye katiba..anatapatapa..atatukoma tunausongo nae yule tumbili we mwache tu![/QUOTE
Hayo yote msingi wake ni katiba, katiba ikiwa mbaya escrow utaendelea kuziona.
 
vijana wa mabibo hostel tunasubiri dirisha la kuandikisha wapiga kura lifunguliwe tukajiandikeshe tukurudishe bungeni mbunge wetu kipenzi, tunauona mchango wako na hata ccm wanajua, ndo mana nape ana tapatapa hataki kurud tena ubungo
 
mvua za december zinapokaribia kunyesha anga huwa na mawingu sana,
wakati huo kuna watu huwa wanaweweseka sana njiani na kuongea wenyewe ovyo
mleta hii mada ni mhanga wa aya mawingu ya mvua.
tafadhali mshikeni huyo asije akakanyaga nyanya za watu akawatia hasara wajasiliamali wetu,
(mawingu, kichaa, mvua)
 
Pole sana ndugu sisi wananchi wa ubungo kwakweli tunajifunia kua na mbunge wa aina ya mnyika ambae haangalii masilahi ya ubungo pekee bali masilahi ya taifa kwa ujumla.Mnyika ni chaguo la mungu kijana huyu ameyatoa maisha yake hadi kuamua kusoma evening class kwaajili ya mabadiliko ya nchi hii kwakweli,hao watawala wanambania kuleta maendeleo ubungo hasa ya maji ambayo ndio kero kubwa ya maji sababu za kisiasa kwani wao kikubwa wanacho jali ni idadi ya uwakilishi bungeni na si maendeleo kwa taifa kwa ujumla wake,watu kariba ya mnyika ni wana
apinduzi ambao serikari yoyote yenye kuendekeza vitendo vya kifisadi hawapendi kumsapoti kisiasa hasa maendeleo jimboni kwake au kwa wapiga kura ili asionekane yeye ni mtu safi,nachelea kusema kwamba mimi kama mwananchi wa ubungo tena kimara namsapoti sana mnyika kuwa sio tu mbunge bali hata waziri au Raisi kabisa.

tatizo watu wenye uelewa kama wewe na wachache hapa tz
 
Hebu acheni kudeka....

Huko kigamboni hawawahi kuwa na maji toka enzi za mkoloni lakini hawajawahi kumghasi mbunge wao mtandaoni
 
yaani mimi (mlete mada ) siongelei kwa ushabiki wa chama nazungumzia ahadi alizozitoa huyu mheeshimiwa mpaka tuka mpa kura zetu, tukakesha naye pale loyola, tukalivunja vunja gari la wizara ya mambo ya ndani kwa imani kuwa lilikuwa limejakuharibu matokeo.....leo ni mwezi wa pili ubungo tunanunua maji ndoo sh 1000 tena hapa mtaani kwetu kuna tajiri mmoja ndio analeta kwenye malori...vinginevyo utatumia ya chumvi sasa kama huyu tajiri wa hapa mtaani pamoja na kwamba anatuuzia maji lakini amekuwa msaada mkubwa sana yeye sio mwanasiasa Mnyika mwenye jimbo lako umeshindwa kweli kutafuta lori kumi za maji hata ukawa unatuuzia kwa sh 500 kwanza utapata faida pili utatuletea ahueni kwenye hili swala la maji, mchango wako bungeni ni mkubwa lakini jimboni hamna anayekuelewa...unahangaika na mambo makubwa mara katiba mara ufisadi wakati jimboni hamna
maji...watakuuua bure..kuwa mbunifu nunua malori kumi ya maji pitisha mitaani uzia wananchi kwa bei nafuu kidogo kwanza utapata faida kisha watu tunaweza kurudisha imani.
 
Ila hii imezidi sasa daaah....mwezi mmoja sasa no maji. Mnatutakia nini jamani?
 
Hukumbuki hata yule anayeongoza kwa uongo serikali mwaka 2012 bungeni alisema(william lukuvi) alimpa saluti kwamba kati ya watu anaowakubali wanaotumia akili bungeni ni pamoja na mnyika ? Leo ww tu unaye kesha barabarani na kofia ya kijani umchukie mnyika inawezekana ww ni chizzi……

Tumia akili yako vizuri..lukuvi anaishi jimbo la mnyika? Lukuvi anateseka na shida ya maji kama sisi?..nakwambia hivi mnyika harudi tena bungeni abaki huko huko huku asikanyage tena tutamsulubu vibaya sana..anashinda kwenye vyombo vya habari tu wakati sisi hatuna maji? Anamuwakilisha nani bungeni?
 
muheshimiwa wakati wa kampeni ya uchaguzi 2010 ulituahidi kuwa utamaliza kero ya maji ubungo, tukakupa kura zetu, tukakesha wote Mpale loyola kuhakikisha kura hazichakachuliwi, peoplez power tukalibeba na kulipindua gari la wizara ya mambo ya ndani wakati lilipolazimisha kuingia pale getini mimi Dar es salaam nimekuja mwaka 90 nilifikia gongo la mboto ambapo nakumbuka tulikuwa tunakunywa maji ya kisima na yenye chumvi, niliendelea kunywa maji ya chumvi mpaka mwisho wa miaka ya tisini ndiyo ilikuwa mwisho wa kunywa maji ya chumvi..leo karne ya 21 miaka 50 ya uhuru kwa maraya kwanza nakunywa maji ya chumvi....kweli tunasifu juhudi zako za kufichua maovu huko bungeni lakini kura zetu sahau....umeshindwa kusoma alama za nyakati kwamba wakuu wamekuundia zengwe ubungo pasipatikane maji ili uonekane hufanyi chochote......ungeweza hata kuleta maji ya kununua kwenye malori tunge appriciate uwajibikaji wako sasa huku maji hakuna hata ya kununua hakuna .....ukipata ubunge 2015 walahi natembea uchi......"maana tumechoka sasa"
Mtoa mada yaelekea katumwa na iptl hana jipya na sisi hatuko tayari kupoteza jimbo.
 
Maji yamemshinda sasa amehamia kwenye katiba..anatapatapa..atatukoma tunausongo nae yule tumbili we mwache tu!

watu wa jimbo la ubungo punguzeni uoga. Unganeni muandamane kwenda makao makuu ya wizara ya maji yalipo hapo ubungo kwa lengo la kumwambia magembe na makala waamue moja, la kufungulia maji au wawape ruhusa ya kulitoboa bomba linalopita jimboni kwenu ili mjichotee bila malipo.
Mnyika mtamwonea bure kwani aliipeleka hoja binafsi ya kuitaka serikali iseme ni lini jiji la Dar litapata maji ya uhakika lakini ccm waliipoka hoja ile na kuifanya ya kitaifa.
Kukosa kwenu maji ni mbinu za ccm kumdhoofisha Mnyika kwani ni mwiba unaowachoma sana bungeni hata Makinda anamwogopa. Si ndiye aliyemwita mkulu dhaifu?. Dogo ni jembe acheni kumharibia, give him another chance na kayapasueni bomba mkinge maji ili magembe aumie kwa hatua mlizochukua.
 
watu wa jimbo la ubungo punguzeni uoga. Unganeni muandamane kwenda makao makuu ya wizara ya maji yalipo hapo ubungo kwa lengo la kumwambia magembe na makala waamue moja, la kufungulia maji au wawape ruhusa ya kulitoboa bomba linalopita jimboni kwenu ili mjichotee bila malipo.
Mnyika mtamwonea bure kwani aliipeleka hoja binafsi ya kuitaka serikali iseme ni lini jiji la Dar litapata maji ya uhakika lakini ccm waliipoka hoja ile na kuifanya ya kitaifa.
Kukosa kwenu maji ni mbinu za ccm kumdhoofisha Mnyika kwani ni mwiba unaowachoma sana bungeni hata Makinda anamwogopa. Si ndiye aliyemwita mkulu dhaifu?. Dogo ni jembe acheni kumharibia, give him another chance na kayapasueni bomba mkinge maji ili magembe aumie kwa hatua mlizochukua.

Wazo zuri sana hili mkuu....yakiitishwa haya maandamano sitakosa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom