Mnyika jimbo la Ubungo umeshalikosa

Mnyika jimbo la Ubungo umeshalikosa

Wewe jamaa unahitaji kuelimishwa. Kuna mambo umeyajaza kichwani mwako wakati hukutakiwa kuyaingiza humo.

Itafute ofisi ya Mbunge ili uelimishwe kazi za siasa na wanasiasa. Hiyo faida ya kuuza maji unayotaka Mbunge aipate wewe huihitaji? Kama wapiga kura ndiyo wa aina yako, basi nchi haitakaa ipate maendeleo.

William Lukuvi itabidi anunue malori 100 ili aweze kuwasaidia wananchi wa jimbo lake. Umeshusha Hadhi Ya Mbunge na vyema ukatengua kauli yako.
 
Kwa haya majibu ya washabiki wa chadema ndiyo maana watu wanaona bora waendelee kuchagua ccm tu.
 
Mleta mada kachakachuliwa akili na ccm. Aya subiria mnyika akuletee na ugali ndani wewe lala tuu usifanye kazi, alafu mnyika sio serekali serekali ya ccm ndio inayopanga bajeti iende wapi wape ukawa kura kwanza ndio umlaumu mnyika
 
Mkuu msamehe huyu ajuza sio kosa lake ni kosa la ccm kumnyima elimu na lishe bora

wewe jamaa unahitaji kuelimishwa. Kuna mambo umeyajaza kichwani mwako wakati hukutakiwa kuyaingiza humo. Itafute ofisi ya mbunge ili uelimishwe kazi za siasa na wanasiasa. Hiyo faida ya kuuza maji unayotaka mbunge aipate wewe huihitaji? Kama wapiga kura ndiyo wa aina yako, basi nchi haitakaa ipate maendeleo. William lukuvi itabidi anunue malori 100 ili aweze kuwasaidia wananchi wa jimbo lake. Umeshusha hadhi ya mbunge na vyema ukatengua kauli yako.
 
Mnyika ni mnunge wa Tanzania nzima sio ubungo tu

Toka uhuru maji yako wapi?? Ccm wameobgeza ubungo miaka50 huulixi maji mnyika afanye nin miaka4!!
 
kwa haya majibu ya washabiki wa chadema ndiyo maana watu wanaona bora waendelee kuchagua ccm tu.


wewe kapimwe akili.

Unaishi tanzania?
Unafatilia bunge?
Unafatilia siasa za tanzania?
Unajua mnyika ni upinzani?
Unafatiliaga bunge la bajeti?
Unajua mnyika ni nani kwenye serikali ya ccm?
Unaujua umuhimu wa kila binadamu kupata lishe bora?
Unajua umuhimu wa kuwa na elimu bora na sio bora elimu?

Je unavifahamu au unavyo vyote hivyo hapo juu?
 
Wanaotutesa ni serikali ya CCM, hivyo 2015 pigeni kura ya chuki nchi nzima dhidi ya CCM halafu muangalie kama maji hamtayapata. Tanzania ina zaidi ya 60% imezungukwa na maji, pia ardhini zaidi ya 75% kuna maji salama ya matumizi ya binadamu. tataizo la serikali hii ya ccm ni kufikiria kuiba tu badala ya maendeleo ya watu waliyoiweka madarakani.

Hivyo mtoa mada 2015 hatuangalii ubungo peke yake bali nchi nzima na tunaenda kuiangusha serikali ya ccm kupitia sanduku la kura.
 
ccm nawashauri jimbo la mnyika na tundu lisu wasisimamishe mtu(msindikizaji)
 
Wewe, Gongo la mboto gani maji ya chumvi yaliisha miaka ya tisini?

Hapa nilipo nmetoka kununua ndoo ya maji ya bomba kwa shilingi elfu moja.

Inaonesha upo bariadi mzee huijui dar.
 
Muheshimiwa wakati wa kampeni ya uchaguzi 2010 ulituahidi kuwa utamaliza kero ya maji Ubungo, tukakupa kura zetu. Tukakesha wote pale loyola kuhakikisha kura hazichakachuliwi, peoplez power tukalibeba na kulipindua gari la wizara ya mambo ya ndani wakati lilipolazimisha kuingia pale getini mimi Dar es salaam nimekuja mwaka 90 nilifikia Gongolamboto ambapo nakumbuka tulikuwa tunakunywa maji ya kisima na yenye chumvi.

Niliendelea kunywa maji ya chumvi mpaka mwisho wa miaka ya tisini ndiyo ilikuwa mwisho wa kunywa maji ya chumvi..leo karne ya 21 miaka 50 ya uhuru kwa mara ya kwanza na kunywa maji ya chumvi. Kweli tunasifu juhudi zako za kufichua maovu huko bungeni lakini kura zetu sahau. Umeshindwa kusoma alama za nyakati kwamba wakuu wamekuundia zengwe Ubungo pasipatikane maji ili uonekane hufanyi chochote. Ungeweza hata kuleta maji ya kununua kwenye malori tunge appriciate uwajibikaji wako sasa huku maji hakuna hata ya kununua hakuna. Ukipata ubunge 2015 walahi natembea uchi. "maana tumechoka sasa"

Wewe anza maandalizi ya matembezi yako ukiwa uchi,lakini isije ikawa akili zinaanza kuruka hivyo kuhalalisha kusalula kwako.Mnyika atashinda jimbo la ubungo 2015 period.
 
Mleta mada kama kweli unataka kumshutumu mbunge wako kwa haki basi ni vyema ukajifunza ili ujue majukumu ya mbunge na wajibu wake. Pia uwe mfuatiliaji wa mbunge wako anapokuwa bungeni. Mnyika huwa anapigia kelele swala la maji hapo Ubungo, utekelazaji wa serikali ndio tatizo.

Unaposema mbunge aanze kubeba maji awaletee..hapo sasa umewaza kwa kiwango kidogo sana cha kufikiri maana mbunge hastahili kuyafanya matatizo ya watu wake kuwa mtaji wa biashara. Na kama ulitaka awaletee bure..hili nalo linaonyesha ufinyu wa uelewa wa mambo.

kubwabwaja bungeni sio hoja!...., tunataka kuoma matokeo ya makelele yake kwenye Kero ya maji

Kiukweli katika swala maji Mnyika ameprove failure!

Ni vema akampisha mtu mwingine kwenye hicho kiti!
 
wewe kapimwe akili.

Unaishi tanzania?
Unafatilia bunge?
Unafatilia siasa za tanzania?
Unajua mnyika ni upinzani?
Unafatiliaga bunge la bajeti?
Unajua mnyika ni nani kwenye serikali ya ccm?
Unaujua umuhimu wa kila binadamu kupata lishe bora?
Unajua umuhimu wa kuwa na elimu bora na sio bora elimu?

Je unavifahamu au unavyo vyote hivyo hapo juu?

Duh! Sijui hata kilichokufanya utapike matapishi yote hayo.

Ndiyo maana mie huwa sioni kama mnatofauti na wale wanaoshabiki mafisadi(ccm) maana wote bado hamjajitambua,mmeweka mbele sana ushabiki wa vyama.
 
Watu wako busy na vyama vyao bhana, we unawaleta kero zako za maji nani atakusikiliza.

We unakuwa kama mgeni wa siasa za bongo.
 
Mmi naona ungeanza sas ili itakpofika wakati huo uwe umeshazoea. na waliotuongoza toka tunapata Uhuru utawachukulia hatuagani maan hakuna walichokufanyia au ni mnyika
 
Yaani tena atapata kura nyingi kuliko wakati ule,,, maana sasa hata zile kura za CUF atazipata kwa maana ni ukawa.... Yaani 2015 atashinda kwa kishindo ikiwezekana hata kampeni asipige!!!
 
Naomba nikusaidie, kazi ya mbunge ni kuwasemea watanzania kazi ambayo imefanywa vizuri mno na mnyika kushinda wabunge wote wa ccm, kazi ya serikali na kuwapelekea huduma kama hiyo ya maji kazi ambayo serikali yako ya ccm imeshindwa kufikia viwango.
muheshimiwa wakati wa kampeni ya uchaguzi 2010 ulituahidi kuwa utamaliza kero ya maji ubungo, tukakupa kura zetu. Tukakesha wote pale loyola kuhakikisha kura hazichakachuliwi, peoplez power tukalibeba na kulipindua gari la wizara ya mambo ya ndani wakati lilipolazimisha kuingia pale getini mimi dar es salaam nimekuja mwaka 90 nilifikia gongolamboto ambapo nakumbuka tulikuwa tunakunywa maji ya kisima na yenye chumvi.

Niliendelea kunywa maji ya chumvi mpaka mwisho wa miaka ya tisini ndiyo ilikuwa mwisho wa kunywa maji ya chumvi..leo karne ya 21 miaka 50 ya uhuru kwa mara ya kwanza na kunywa maji ya chumvi. Kweli tunasifu juhudi zako za kufichua maovu huko bungeni lakini kura zetu sahau. Umeshindwa kusoma alama za nyakati kwamba wakuu wamekuundia zengwe ubungo pasipatikane maji ili uonekane hufanyi chochote. Ungeweza hata kuleta maji ya kununua kwenye malori tunge appriciate uwajibikaji wako sasa huku maji hakuna hata ya kununua hakuna. Ukipata ubunge 2015 walahi natembea uchi. "maana tumechoka sasa"
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom