Mkaruka
JF-Expert Member
- Feb 5, 2013
- 19,932
- 34,916
Salaam JF ! Kiukweli sisi kama wananchi tunaokaa Katika JIMBO LA UBUNGO tunasema kwamba....."Mnyika ni mbunge tuliyemwamini na kumchagua kwa KURA lukuki tukitarajia huo ndio mwisho wa matatizo yetu hususani MAJI ,yaliyodumu kwa takribani miaka 53 sasa!Tunasema kwamba UMETUANGUSHA sana!!Jimbo lililokupa ubunge umelisahau na kutwishwa majukumu mazito ya chama.Tumekuwa tukikusikia ukitukanana na viongozi wenzio wa kisiasa mikutanoni.Hivi hili ndilo tulilokutuma?Chama ni bora kuliko sisi?Wanasema hukusanyi KODI na hivyo huwezi kuleta maji na kama ni hivyo ni kwanini ulituahidi?Why Tusiendelee kumchagua yuleyule aliyekuwepo amma hata mtu mwingine,chama kingine ila wewe?.Kwasababu ya yote hayo tunasema tunashukuru sana kwa utumishi wako na tunakushauri URUDI SHULE.Ahsante..... IBRAHIM MGAYA Mkazi Kimara!!