So hapo Tundu Lissu anakiri kweli kuwa alikuwa anahamasisha uasi, ila dhidi ya mfumo kandamizi.....Je huo mfumo unapimwaje kuwa ni kandamizi? Maana ukienda Marekani Kuna wanaharakati wanaona nchi Yao Ina mfumo kandamizi, ukienda China pia wapo wanaiona nchi Yao Ina mfumo kandamizi, Urusi, Kenya, Rwanda, n.k
Mifumo kandamizi na isiyo kandamizi inapimwa kwa kutumia nini?
Je kama mfumo ni kandamizi kweli, kufanya uasi anaoumaanisha Lissu (riots, sabotage, n.k) linakuwa suluhisho halali kwa sababu Nyerere alisema? Tunatakiwa kuchukua maneno ya wanasiasa au viongozi kama kuhalalisha jambo hata kama litahatarisha amani na usalama wa nchi?
Mfano Magufuli alishawahi kusema wafungwa wafanyishwe kazi kama punda, wapigwe mateke, Inakuwa ni kauli sahihi kwa sababu kiongozi mkubwa alisema?