Dr. Mariposa
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 4,636
- 15,247
Guys ninaandika haraka haraka maana nampepea bwana harusi mtarajiwa amezimia baada ya kukataliwa kuoa binti mzuri wa kizanzibar,
Huyu jamaa baada ya kuposa na kulipa mahari yote akapata mualiko maalum wa kuonana na familia ya wakwe zake watarajiwa na kupata chakula cha mchana pamoja, nilimwambia kua akipewa samaki ale kiduchu tu ila chonde chonde asimgeuze,
Basi bwana na mie nilikua mmoja wa wapambe wa bwana harusi mtarajiwa kama mjuavyo tamaduni ni kua wanawake hukaa sehemu yao na wanaume hukaa sehemu yao lakini wakati tunaachana akakae upande wa wanaume nikamkumbusha tena "huku Zenji ukiwa ukweni samaki hagaezwi" akasema nisikonde "chill, i got this...." hayo ndio maneno ya mwisho kunambia kabla hajazimia 😭😭😭😭
Huyu bwana akapewa bonge la samaki unajua samaki wa kupaka weweeee, jamaa akapagawa akasahau onyo nililompa akaanza kumgegedua samaki upande wa kwanza ukaisha akamgeuza na kuendelea kumfakamia kwa fujo huku akijiramba vidole daah!🥺 hapo hapo baba wa bibi harusi akasimama kwa hasira na kuanza kumfokea sana kwanini kamgeuza yule samaki, akasema ndoa haipo tena mahari yake amtume mshenga wake akaifate kesho asubuhi sana na kuondoka huku akirusha rusha mikono, taharuki ikatokea jamaa tunamuuliza vipi hajajibu akadondoka na kuzimia......
Nitaendelea kuwapa updates ila ndio hivyo mkija Zanzibar kuoa chonde chonde msimgeuze samaki.
Huyu jamaa baada ya kuposa na kulipa mahari yote akapata mualiko maalum wa kuonana na familia ya wakwe zake watarajiwa na kupata chakula cha mchana pamoja, nilimwambia kua akipewa samaki ale kiduchu tu ila chonde chonde asimgeuze,
Basi bwana na mie nilikua mmoja wa wapambe wa bwana harusi mtarajiwa kama mjuavyo tamaduni ni kua wanawake hukaa sehemu yao na wanaume hukaa sehemu yao lakini wakati tunaachana akakae upande wa wanaume nikamkumbusha tena "huku Zenji ukiwa ukweni samaki hagaezwi" akasema nisikonde "chill, i got this...." hayo ndio maneno ya mwisho kunambia kabla hajazimia 😭😭😭😭
Huyu bwana akapewa bonge la samaki unajua samaki wa kupaka weweeee, jamaa akapagawa akasahau onyo nililompa akaanza kumgegedua samaki upande wa kwanza ukaisha akamgeuza na kuendelea kumfakamia kwa fujo huku akijiramba vidole daah!🥺 hapo hapo baba wa bibi harusi akasimama kwa hasira na kuanza kumfokea sana kwanini kamgeuza yule samaki, akasema ndoa haipo tena mahari yake amtume mshenga wake akaifate kesho asubuhi sana na kuondoka huku akirusha rusha mikono, taharuki ikatokea jamaa tunamuuliza vipi hajajibu akadondoka na kuzimia......
Nitaendelea kuwapa updates ila ndio hivyo mkija Zanzibar kuoa chonde chonde msimgeuze samaki.