Melki the Storyteller
JF-Expert Member
- May 3, 2022
- 5,701
- 9,779
Ndo hivyo wakurugenzi.
Mwaka jana nilikuwa na nia kabisa ya kitaka kuoa kutokana na upole, unyenyekevu, heshima na adabu aliyokuwa nayo huyo binti licha ya uzuri na rangi yake
Mahari yenyewe haikuwa kubwa kiasi hicho, ni 300k tu. Niliitoa kiutani utani nikisindikizwa na ndugu pamoja na marafiki wenye hulka ambao wao tayari wamekwisha oa. Ndoa ilitakiwa iwe mwishoni mwa Januari. Lakini katikati ya Januari, mke mpya wa jirani yangu alimmwagia mumewe maji ya moto baada ya purukushani zilizotokea jioni hiyo. Chanzo eti ni fumanizi la kwenye simu
Baada ya hapo nilianza kupata tetesi za etu wanawake wapole na wakimya huwa wanatunza vinyongo, lakini siku wakiripuka, wanaweza kukuua huku wanacheka. Jumlisha zile kataa kataa ndoa za humu jukwaani na matukio kedekede. Hiyo siku sikulala usiku, nikaanza kutafakari namna ambavyo ninaenda kujitwisha mzigo mzito wa kumiliki kiumbe ambacho kimeumbwa na Mungu kwa akili na udongo mwingi sana, nikajikuta naona naingilia majukumu yasiyonihusu, nikaanza kukwepa
Nilitamani maneno na matarajio ya ndugu, jamaa na marafiki yapotee vinywani mwao lakini wapi. Ndugu wengine wenye shobo walinunua maandalizi madogo madogo bila kumsahau Mjomba Bwena ambaye alinunua tairi la gari ili aje anikabidhi kama zawadi kwenye harusi yangu ili nikamilishe vifaa vingine liwe gari kamili
Baada ya hapo nilisingizia kuwa nahitaji kusoma IT kwa ajili ya kazi zangu binafsi ili wanipatie muda. Nikahama hata pale nilipokuwepo. Siku nilipomuonesha dada yangu mahali nilipohamia, nikawa nimeyabananga. Wakwe wakaanza kutengeneza misururu. Sasa hivi wananisumbua eti nioe ili mdogo wake na mke wangu mtarajiwa aolewe maake keshapata bwana
Nimejaribu kuzungumza nao kwa mafumbo kuwaeleza kuwa sina wazo la kuoa, kama ni issue ya mahari mimi nishasamehe, lakini ndio kwanza wanatafsiri eti "Wiki ijayo mambo yatakuwa mwemwere mwemwere
Nifanye nini kuukimbia huu msala ndugu zanguni?
Mwaka jana nilikuwa na nia kabisa ya kitaka kuoa kutokana na upole, unyenyekevu, heshima na adabu aliyokuwa nayo huyo binti licha ya uzuri na rangi yake
Mahari yenyewe haikuwa kubwa kiasi hicho, ni 300k tu. Niliitoa kiutani utani nikisindikizwa na ndugu pamoja na marafiki wenye hulka ambao wao tayari wamekwisha oa. Ndoa ilitakiwa iwe mwishoni mwa Januari. Lakini katikati ya Januari, mke mpya wa jirani yangu alimmwagia mumewe maji ya moto baada ya purukushani zilizotokea jioni hiyo. Chanzo eti ni fumanizi la kwenye simu
Baada ya hapo nilianza kupata tetesi za etu wanawake wapole na wakimya huwa wanatunza vinyongo, lakini siku wakiripuka, wanaweza kukuua huku wanacheka. Jumlisha zile kataa kataa ndoa za humu jukwaani na matukio kedekede. Hiyo siku sikulala usiku, nikaanza kutafakari namna ambavyo ninaenda kujitwisha mzigo mzito wa kumiliki kiumbe ambacho kimeumbwa na Mungu kwa akili na udongo mwingi sana, nikajikuta naona naingilia majukumu yasiyonihusu, nikaanza kukwepa
Nilitamani maneno na matarajio ya ndugu, jamaa na marafiki yapotee vinywani mwao lakini wapi. Ndugu wengine wenye shobo walinunua maandalizi madogo madogo bila kumsahau Mjomba Bwena ambaye alinunua tairi la gari ili aje anikabidhi kama zawadi kwenye harusi yangu ili nikamilishe vifaa vingine liwe gari kamili
Baada ya hapo nilisingizia kuwa nahitaji kusoma IT kwa ajili ya kazi zangu binafsi ili wanipatie muda. Nikahama hata pale nilipokuwepo. Siku nilipomuonesha dada yangu mahali nilipohamia, nikawa nimeyabananga. Wakwe wakaanza kutengeneza misururu. Sasa hivi wananisumbua eti nioe ili mdogo wake na mke wangu mtarajiwa aolewe maake keshapata bwana
Nimejaribu kuzungumza nao kwa mafumbo kuwaeleza kuwa sina wazo la kuoa, kama ni issue ya mahari mimi nishasamehe, lakini ndio kwanza wanatafsiri eti "Wiki ijayo mambo yatakuwa mwemwere mwemwere
Nifanye nini kuukimbia huu msala ndugu zanguni?