Mnaopinga uondoaji wa maduka ya dawa maeneo ya hospitali mnaujua ukweli?

COARTEM

JF-Expert Member
Nov 26, 2013
3,598
3,644
Lengo la serikali kuruhusu maduka hayo kuwepo maeneo ya hospitali lilikuwa zuri tu. Waliagizwa kuuza dawa kwa bei nafuu na maduka hayo yafunguliwe saa 24 kila siku. Lakini baada ya maduka hayo kuanza kufanya kazi, kuna watendaji wa serikali wasiokuwa waaminifu walianza kuweka maslahi yao kwenye maduka hayo. Wenye maduka hayo wakaanza kukiuka maelekezo ya serikali na kufanya mambo wanayo yajuwa wao. Bei za dawa zilipandishwa maradufu kuliko hata maduka ya dawa yaliyo mbali na hospitali.

Mfano
  1. Dawa inayouzwa hospitali Tshs 800/= ( maduka pembeni mwa hospitali wanauza Tshs 4000/=) wakati maduka yaliyo mbali kidogo just mwendo wa dk 10 wao wanauza dawa hiyoTshs 1000/= hadi 1500/=.
  2. Dawa inayouzwa hospitali Tshs 5000/= ( maduka pembeni mwa hospitali wanauza Tshs 35,000/=) wakati maduka yaliyo mbali kidogo just mwendo wa dk 10 wao wanauza dawa hiyoTshs 15,000/= hadi 20,000/=.
  3. Dawa inayouzwa hospitali Tshs 1000/= ( maduka pembeni mwa hospitali wanauza Tshs 5000/=) wakati maduka yaliyo mbali kidogo just mwendo wa dk 10 wao wanauza dawa hiyoTshs 2000/= hadi 2500/=.
  4. Maduka hayo hayafunguliwi saa 24 kama ilivyokubaliwa, lugha za watoa huduma ni mbovu kama zilivyo za watoa huduma wa ndani ya hospitali. Ukitaka kuamini nilicho kiandika nenda Hospitali ya Mkoa Morogoro kwenye lile duka la nje ya geti kuu la hospitali hiyo utaelewa hiki nilicho kiandika. Lile duka nje ya geti la Hospitali ya mkoa Morogoro ni zaidi ya wezi. Nunua dawa ndani ya hospitali hiyo kisha nenda kanunue dawa hiyo hiyo kwenye hilo duka nje ya geti maweeee......utalia.
Nawaambia wana JF hayo maduka yananuka harufu ya unyonyaji kwa mgonjwa, kuna CHAIN ya ULAJI kwenye maduka hayo ambayo inawahusisha watumishi wenye vyeo vikubwa serikalini. Mh Rais MAGUFULI piga kazi watu watakuelewa tu mbele ya safari. Nchi ilioza hii jamani.

NAUNGA MKONO AGIZO LA SERIKALI KUFUNGA MADUKA HAYO PEMBENI MWA HOSPITALI ZA UMMA!

Agizo liko hapa Maduka yote ya dawa nje ya hospitali za Serikali marufuku
 
Support kubwa mtoa thread unayoyasema ndio Hali halisi , tuendelee kumpa big up Mheshimiwa Dr JPM
 
Issue sio bei.Wakuu wanadai hizo dawa ni za humo ndani zinaibiwa. Kama ni za wizi maana yake bei ingekuwa chini sana.Makes no sense
 
Ndugu wale watu si wezi bali ni wafanyabiashara wanaohitaji ushindani. Kimsingi kinachotakiwa ni kuongeza maduka nje ili ushindani uwepo. Kuwaita wezi ni kutowatendea haki. Wakifunga hayo maduka madawa yatapatikana wapi? Waliopoteza kazi nani atawaajiri? Kwani wanauza biashara haramu. Serikali iandae utaratibu wake na si kuwavuruga wafanyabiashara.
 
Mkuu kwanini yafungwe kama yapo kihalali na ni biashara za watu na kodi wanalipa na serikali inaingiza kipato?
Tatizo lipo kwenye hospitali zetu tu,kwani iwapo serikali itafanya jitihada hizo dawa zipatikane hapo hospitali kwa tsh.800 kuna mtu atatamani kwenda nje kununua dawa hizo hizo kwa tsh.1000 au 2000?
Cha muhimu ni serikali kuongeza bajeti ya wizara ya afya na waisimamie kwa ukaribu kuondoa urasimu katika hosptali zetu.
 
Watoe kwani lazima wajenge nje ya hospital wakapeleke huko mbali wasituzingue na ole wao serikali nayo isiweke dawa hospitalini moto wake...
 
Issue sio bei.Wakuu wanadai hizo dawa ni za humo ndani zinaibiwa. Kama ni za wizi maana yake bei ingekuwa chini sana.

Issue ni vyote viwili vinafanyika, na bei inakuwa kubwa sababu kwanza mleta dawa toka idara ya serikali anaiuza kwa dukani pembeni ya hospitali (saa ingine duka humilikiwa na mtumishi wa hospitali husika, halafu muuzaji dukani naye anaweka cha juu kwa hiyo mwisho wa siku victim anakuwa mgonjwa anayekuja nunua dawa hapo kwa maagizo au maelekezo toka ndani ya hospitali husika
 
Mleta mada upeo wako ni mdogo sana. Unabahatisha mambo hapa.

UHALISIA.
1/Sio kweli kuwa serikali ndio iliweka utaratibu wa maduka ya dawa kuwa karibu na hospitali. Wamiliki wa maduka ya dawa ndio waliamua kuyaleta maduka ya dawa karibu na hospitali. Kifupi wamiliki wa maduka walisogeza huduma na biashara zao karibu na wateja wao(Wagonjwa).

2/Sio kweli kabisa kuwa serikali iliweka utaratibu wa maduka hayo yafanye biashara masaa 24 au yauze dawa kwa bei ya chini. Ukweli ni kwamba serikali hausiki kabisa na uendeshaji wa maduka ya dawa binafsi nje ya hospitali.

3/Eneo lolote nje ya hospitali ni eneo binafsi, kuna kila biashara zinafanywa nje ya hospitali za serikali. Kama Hoteli, Bar, Guest, Migahawa, Vituo vya mafuta, banki, Maduka ya Dawa nk. Wamiliki wa maeneo hayo wamejenga majengo ili watu kuweza kupangisha kwa shughuli mbalimbali ikiwemo biashara, Ofisi, Nyumba za ibada nk. Kodi zake zinakuwa ghali zaidi kwa sababu ni Eneo lenye biashara zaidi.

4/Maduka ya Dawa ni biashara huria, kila mtu anapanga bei yake ya kuuzia kwa sababu kila mmiliki wa duka la Dawa anauza kulingana na faida inayotaka. Sio kweli kabisa kuwa maduka ya dawa nje ya hospitali yanauza dawa kwa bei ghali. Uchunguzi wangu nimegundua tofauti kabisa. Dawa zinauzwa ghali wakati tu upatikanaje wake unapokuwa haba.
 
suala si kuondoa hayo maduka, kwan hata wakiuzia mbali na hapo, kama dawa kwenye hospitali za serikali hakuna... na hakuna anayefatilia utaratibu waliopewa hao wauza madawa! Hakutakuwa na msaada wowote

suala ni kwa nchi nzima, wauza madawa watakaokiuka utaratibu wafungiwe kibali! Muhimu ni utekelezaj na ufatiliaji!

Ahsante
Jigo
 
Issue sio bei.Wakuu wanadai hizo dawa ni za humo ndani zinaibiwa. Kama ni za wizi maana yake bei ingekuwa chini sana.Makes no sense
Umewahi kuuguliwa na kwenda kununua dawa kwenye hayo maduka? Mkuu hayo maduka siyo msaada hata kidogo
 
Mleta mada upeo wako ni mdogo sana. Unabahatisha mambo hapa.UHALISIA.1/Sio kweli kuwa serikali ndio iliweka utaratibu wa maduka ya dawa kuwa karibu na hospitali. Wamiliki wa maduka ya dawa ndio waliamua kuyaleta maduka ya dawa karibu na hospitali. Kifupi wamiliki wa maduka walisogeza huduma na biashara zao karibu na wateja wao(Wagonjwa).2/Sio kweli kabisa kuwa serikali iliweka utaratibu wa maduka hayo yafanye biashara masaa 24 au yauze dawa kwa bei ya chini. Ukweli ni kwamba serikali hausiki kabisa na uendeshaji wa maduka ya dawa binafsi nje ya hospitali.3/Eneo lolote nje ya hospitali ni eneo binafsi, kuna kila biashara zinafanywa nje ya hospitali za serikali. Kama Hoteli, Bar, Guest, Migahawa, Vituo vya mafuta, banki, Maduka ya Dawa nk. Wamiliki wa maeneo hayo wamejenga majengo ili watu kuweza kupangisha kwa shughuli mbalimbali ikiwemo biashara, Ofisi, Nyumba za ibada nk. Kodi zake zinakuwa ghali zaidi kwa sababu ni Eneo lenye biashara zaidi.4/Maduka ya Dawa ni biashara huria, kila mtu anapanga bei yake ya kuuzia kwa sababu kila mmiliki wa duka la Dawa anauza kulingana na faida inayotaka. Sio kweli kabisa kuwa maduka ya dawa nje ya hospitali yanauza dawa kwa bei ghali. Uchunguzi wangu nimegundua tofauti kabisa. Dawa zinauzwa ghali wakati tu upatikanaje wake unapokuwa haba.
Wewe utakuwa mtoto wa Mringo bila shaka.
 
govt works on pepar ebu ambatanisha document ambayo serikali iliruhsu maduka kwa makubaliano yafanye kazi saa24 na kuuza dawa kwa bei nafuu
 
Back
Top Bottom