Mtu Asiyejulikana
JF-Expert Member
- Sep 11, 2017
- 1,694
- 3,982
Ukimsikiliza Lema haongei kwa bahati mbaya. Anachoongea na anachofanya sasa ni kufitinisha Wanachama na Chama Cha CHADEMA. Alianza na kusema waendesha Boda boda wamelaaniwa. Hivyo, hata kula zao hahitaji.
Sasa anasema wasajili line za simu wafukuzwe makwao maana hawana wanachofanya. Lakini hazungumzii wezi, mafisadi, majambazi, matapeli, malaya n.k hawa amewaacha tu wawe huru katika speech zake.
Alipewa mikakati alipotaka kurudi TZ kama ambavyo yeye mwenyewe alidokeza. Arudi ila aunge mkono juhudi ili naye ale mema ya nchi, kama wenzie
Mwaka 2025 chadema hawatakuwa na la kuzungumzia. CCM kwa sasa imemaliza kila jambo. Hakuna ufisadi, miradi inaenda poa. Wanasiasa hawatekwi. Wanafanya issues zao bila tatizo. Hivyo hakutakuwa na haja ha upinzani. Kila kitu kimeenda sawa kama ambavyo kilitakiwa.
Tunawazika Chadema. Maana hawana hoja tena. Hata suala la Katiba Mpya sasa naona anayekomaa ni Maria Sarungi tu. Wanachadema wameshasahau. Wamenyimwa hoja kwa sasa. Hata sera zao wanashindwa zitangaza. Tunakoenda hakutakuwa na hoja kabisa ya upinzani.
Sasa anasema wasajili line za simu wafukuzwe makwao maana hawana wanachofanya. Lakini hazungumzii wezi, mafisadi, majambazi, matapeli, malaya n.k hawa amewaacha tu wawe huru katika speech zake.
Alipewa mikakati alipotaka kurudi TZ kama ambavyo yeye mwenyewe alidokeza. Arudi ila aunge mkono juhudi ili naye ale mema ya nchi, kama wenzie
Mwaka 2025 chadema hawatakuwa na la kuzungumzia. CCM kwa sasa imemaliza kila jambo. Hakuna ufisadi, miradi inaenda poa. Wanasiasa hawatekwi. Wanafanya issues zao bila tatizo. Hivyo hakutakuwa na haja ha upinzani. Kila kitu kimeenda sawa kama ambavyo kilitakiwa.
Tunawazika Chadema. Maana hawana hoja tena. Hata suala la Katiba Mpya sasa naona anayekomaa ni Maria Sarungi tu. Wanachadema wameshasahau. Wamenyimwa hoja kwa sasa. Hata sera zao wanashindwa zitangaza. Tunakoenda hakutakuwa na hoja kabisa ya upinzani.