Mmoja auawa kwa risasi huko Tegeta

Mmoja auawa kwa risasi huko Tegeta

Zak Malang

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2008
Posts
5,404
Reaction score
242
Kwa Mujibu wa ITV kipindi cha Hapa na Pale saa 12 leo jioni. Amepigwa risasi na watu wawili waliokimbia na boda boda.

Mtangazaji kasema ni mtu kutoka taasisi nyeti serikalini kutokana na kitambulisho chake mashuhuda walichokiona.

==============
UPDATE:
==============

Mwanaume mmoja ambaye hakujulikana jina lake mara moja, muda mfupi uliopita ameuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana eneo la Tegeta jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, wauaji ni wanaume wawili waliokuwa katika pikipiki maarufu kama 'Bodaboda'.

Marehemu alikuwa akishuka katika gari lake aina ya Toyota Mark II yenye namba za usajili T 508 ADY ndipo alipopigwa risasi kadhaa.

Global Publishers
 
Kwa nini unadhani ni TISS? Ni kwa sababu ya mambo ya kazi au Mambo binafsi??
 
Dar er salaam mda siyo mrefu itakuwa siyo sehemu salama ya kuishi. Umafia unazidi kuongezeka
 
Kapigwa mtu wao hapo ndipo tutajua ufanisi wa vyombo vyetu,watafanya kila mbinu kupata ukweli.ila angekuwa kauwawa kwenye mkutano wa CHADEMA zingeanza danadana.
 
Kwa Mujibu wa ITV kipindi cha Hapa na Pale saa 12 leo jioni. Amepigwa risasi na watu wawili waliokimbia na boda boda.

Mtangazaji kasema ni mtu kutoka taasisi nyeti serikalini kutokana na kitambulisho chake mashuhuda walichokiona.

Kuwa na kitambulisho sio lazima awe ni wa hiyo taasisi. Inahitajika uchunguzi zaidi
 
Ni nani huyo mtu nyeti?
Kama ni wa Tiss sometimes hao wanauwana wenyewe kwa wenyewe, eti kwa sababu za kiusalama!
 
biashara ya boda boda ina faida na hasara zake
zamani ukiona unafuatwa na pikipiki lazima unashtuka
siku hizi ukiona pikipiki utadhani ni bodaboda yuko kazini kumbe wauaji au majambazi.
tutakwisha wengi.....ueni mafisaid tuachieni watu wema
 
Kwa Mujibu wa ITV
kipindi cha Hapa na Pale saa 12 leo jioni. Amepigwa risasi na watu
wawili waliokimbia na boda boda.

Mtangazaji kasema ni mtu kutoka taasisi nyeti serikalini kutokana na
kitambulisho chake mashuhuda walichokiona.

huu uhalifu wa kutumia boda boda naona unaonekana kuota mizizi sasa. vyombo vya dola vijipange kisawasawa. wale askari maarufu tigo wanawajibika ipasavyo?
 
Tanzania sehemu pekee unapoweza kufanya lolote na wala asiwepo wa kukutafuta wala hata kusumbua akili yake.
Hivi sasa ukifanya tukio tu lazima chadema au sisiem ndio wanatajwa na sio mhalifu mwenyewe.....ngoja siku wakija ikulu sijui mtasemaje
 
Wananchi laleni, nchi iko salama. Hiyo ni maandalizi ya kutoa nishani zilizotukuka kwa wakuu wetu wa Jeshi la Polisi. Si unajua yakitokea matukio ya namna hiyo ndiyo huwa hupanda vyeo?
 
Ni nani huyo mtu nyeti?
Kama ni wa Tiss sometimes hao wanauwana wenyewe kwa wenyewe, eti kwa sababu za kiusalama!

Yanaendelea ya Kamanda Barlow na yule wa moshi/Arusha waliedai ni Jambazi
 
Kapigwa mtu wao hapo ndipo tutajua ufanisi wa vyombo vyetu,watafanya kila mbinu kupata ukweli.ila angekuwa kauwawa kwenye mkutano wa CHADEMA zingeanza danadana.

Ni kweli, si unakumbuka ya Barow.
 
siku hizi neno idara nyeti na vigogo vinazidi kukaribiana na maana za uswahilini
 
Back
Top Bottom