Mmoja auawa kwa risasi huko Tegeta

Mmoja auawa kwa risasi huko Tegeta

Hivi waziri mkuu aliagiza watu wapigwe mabomu, mijeledi, mateke ama risasi? Manake inawezekana hakueleweka vizuri
 
Kwa Mujibu wa ITV kipindi cha Hapa na Pale saa 12 leo jioni. Amepigwa risasi na watu wawili waliokimbia na boda boda.

Mtangazaji kasema ni mtu kutoka taasisi nyeti serikalini kutokana na kitambulisho chake mashuhuda walichokiona.

Ina maana alipopigwa cha kwanza kuokotwa ni Kitambulisho chake?
 
Dhuluma mbaya jamani au roho mbaya tuache jamani.
 
huu uhalifu wa kutumia boda boda naona unaonekana kuota mizizi sasa. vyombo vya dola vijipange kisawasawa. wale askari maarufu tigo wanawajibika ipasavyo?

wale wako bize kukamata magari yanayotanua...
 
Labda ni mmoja ya anayedhaniwa kuvujisha habari kwa CDM, wameamua kumshughulikia. Mwigulu or his family Next
 
Hivi waziri mkuu aliagiza watu wapigwe mabomu, mijeledi, mateke ama risasi? Manake inawezekana hakueleweka vizuri

Wapigwe tu, hata kama ni kwa Bomu la Nyuklia, alimradi lengo la kupiga litimie....
 
Hivi waziri mkuu aliagiza watu wapigwe mabomu, mijeledi, mateke ama risasi? Manake inawezekana hakueleweka vizuri

yeye alisema wapigwe tu... sasa na nini hapo hakusema, kuna siku tutasikia wanatandikwa na ndege za kivita kabisa
 
wapigwe tu wakikahidi na watapigwa du ingekuwa kspigwa kwenye mkutano wa Cdm ungesikia wamemua wenyewe Mh Jk mbona kasema nchi ni shwari jamaa juzi msasani kamwagiwa tindikali leo mwingine kapigwa risasi haya
 
Hivi waziri mkuu aliagiza
watu wapigwe mabomu, mijeledi, mateke ama risasi? Manake inawezekana
hakueleweka vizuri

AND I am sure kutokana na mkanganyiko ... tusubiri muendelezo ... TO BE CONTINUED ...! King Mzima lakini!
 
Mtu anapopata mauti cha kufichaficha ni nini
Huu ni udhaifu kuhusu suala la usalama
Vyombo vya Habari navyo vinazidi kujitia
aibu kila uchao,sasa kama waliona kitambulisho
kuna tatizo gani kusema sehemu anayofanyia
kazi.

Hii ni aibu kwa wana habari jueni hapa Tanzania
kila mtu ni muhimu kwa maendeleo ya Taifa.
 
kuna polisi elfu tatu wamehitimu leo,baadhi yao wanakuja dar kuweka heshima
 
Labda ni mmoja ya anayedhaniwa kuvujisha habari kwa CDM, wameamua kumshughulikia. Mwigulu or his family Next

Huyu ni wa pili mtu wa usalama kuuwawa ndani ya miezi mitatu. Mwingine aliuawawa huko huko ofisini kwao na kutupwa kisimani. Nakubaliana nawe huenda ni watu wa CDM wanaogundulika mmoja baada ya mmoja. na kama ni hivyo basi wengi wataondoka tu, kwani inadaiwa watu wa CDM wametanda sana huko UWT.
 
Back
Top Bottom