Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Reset In Peace! Na wale wote waliopata majeraha MUNGU akawatie nguvu na mpone mapema tuendelee na ujenzi wa taifa le2 lililomilikiwa na mapapa wachache wasio na huruma hata kidogo kwa wanainchi wao.
 
Vehicle check list hutumika kuhakikisha kuwa kabla haujaondosha gari yako, umeikagua na kujiridhisha kuwa ni salama.
Swali: Madereva wa mabasi/ daladala (magari ya abiria) wanatumia hizo check list?
Kwa nini Traffic Police wasianzishe hiyo (kama haipo), ili hata kama dereva atajaza jaza tu halafu ikatokea tatizo ambalo litaonekana ni la muda mrefu awe sued na kama hakujaza kwa maana kwamba hakukagua awe sued pia!

Tatizo linakuja kwenye RUSHWA!
Duh, huwa nikifika hapo tu naishiwa nguvu!
 
Sadly, haya mashindano ya ajali yanaonekana kupamba moto kati ya Hood, Abood na Sumry. Niliwahi kushauri huko nyuma kuwa kama mmliki (kwa maana ya kampuni) inapata ajali mara kwa mara basi ifungiwe mpaka pale serikali itapojiridhisha kuwa kampuni hiyo inafuata kanuni zote za usalama barabarani ikiwa ni pamoja na ubora wa mabasi yenyewe, uwezo na nidhamu ya madereva wao.

Lakini kwa kuongeza (and very practicle) wamiliki wa mabasi haya matatu: Hood, Abood na Sumry, WAAPIZWE kwa vitabu vya dini zao kwamba iwapo wanatumia/watatumia 'science ya kimazingira' kuendesha na kuleta ufanisi kwenye biashara zao basi mungu awapumzishe. Waapizwe!

RIP na poleni wafiwa na wale wote mliopata ajali pamoja na ndugu,jamaa na marafiki wa wahanga wote.
 
Nchi mpaka gari ya "rais" inatoka tairi, itakua basi la abiria.
Poleni majeruhi, Mwenyezi Mungu atawajalia mpate nafuu haraka
RIP mliotangulia.
 
lilikua linakwenda wapi??au ni ile ya mbeya??hood nae ana mkosi sasa hata mwezi haujaisha lile lililoungua mikumi...mungu awalaze pema marehem na awafariji wafiwa ,,,,,amen
 
Kumekuwa na mfulilizo wa baadhi ya mabasi kupata ajai mara kwa mara. Jioni hii nimepigiwa sim na rafiki yangu aliyesafiri leo kuwa kumetokea ajali mbaya ya basi la Hood maeneo ya Mikumi. Ila sikupata details zingine. Kama kuna mwenye taarifa please tujuzeni. Kulikoni Hood? Kuna nini nyuma ya pazia hili?
 
IMG_4808.jpg

MKOA wa Morogoro unaendelea kuandamwa na mzimu wa ajali,ambapo usiku wa kuamkia leo ajali nyingine mbaya iliyoyahusisha maroli mawili, Scania lenye namba za usajili T 830 BFZ na Canter yenye namba za usajili T 845 BSD kutokea maeneo ya Fulwe, Mikese mkoani hapa baada ya maroli hayo kugongana uso kwa uso na kusababisha watu watano kufariki dunia papohapo na majeruhi mmoja ambaye amelazwa katika hospitali ya mkoa wa Morogoro.

Mwandishi wetu alifika eneo la tukio na kuyakuta maroli hayo yakiwa yameharibika vibaya huku madereva wote wakiwa ni miongoni mwa watu waliopoteza maisha.​

Zifuatzao ni picha zaidi za tukio hilo:

IMG_4795.jpg


IMG_4809.jpg



IMG_4803.jpg





IMG_4807.jpg

IMG_4811.jpg

DUNSTAN SHEKIDELE, MOROGO



 
dah,nilikutana na hii ajali! yaani lori moja lilikuwa limebakia vipisi vya ushahidi! mungu awalaze pema, maskini tz!
 
Mungu awalaze marehemu pema peponi...
Chanzo cha ajali kichunguzwe ili kupunguza matukio kama haya kutokea tena..
 
RIP marehemu wote,na wale waliojereuhiwa tunawaombea wapone haraka.
 
ulegelege wa..............ndo matokeo yake
kwa kweli barabara ya chalinze moro ni nzuri
lakini kona nyingi,miti mingi barabarani usiku giza totoro,hakuana alama za kutosha
the same to moro dom na moro iringa!
 
nimeishuhudia ajali hii,canter ilikuwa inaovateki gari ikashindwa kumaliza,mbele ilikuwa inakuja scania wakakutana macho kwa uso,
 
Jamani nimepigiwa simu kuna ajali mbaya imetokea minaki lori limelalia
dalaldala watu watano wameshatolewa maiti na wengine wamelaliwa
juhudi za polisi kunasua waliobakia ama maiti watarajiwa bado zinaendelea
kama una ndug ajarudi mpaka usiku huu na yuko mitaa ya kisarawe msanga
embu jaribu kucheki nae kwa kubofya kama jamaa awajamsaidia kumzimia
basi asiache kwenda kushukuru mungu siku ya kesho jamani....
Poleni wafiwa na majjeruhi 20 wameshatolewa hali zao sio nzuri sana
 
Back
Top Bottom