Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

watakuwa wamewapeleka hospital marehemu mungu awalaze mahali pema pepon
 
wanajf nimeskia punde kuwa ajali ya basi la hood kutoka mbeya limegongana na lory la mohamed interprise na vyombo vyote vimeteketea kwa moto,pia abiria wanne wameteketea akiwemo dereva wa lory. mwenye news zaidiatujuze,source . matukio rfa
Hii itakuwa ile ya juzi pale Mikumi!
 
Pole sana kwa waliopatwa na maswahibu..

Bajaji na Pikipiki ni "MAJENEZA YANAYOTEMBEA"
 
Pole sana kwa waliopatwa na maswahibu..Bajaji na Pikipiki ni "MAJENEZA YANAYOTEMBEA"
Mkuu! Ni kweli kbs! MUNGU tupe rehema yako u2linde bila ya kuchoka kama siku zote. Wafiwa wote poleni! Bwana ametoa na ametwaa! Jina lake lihimidiwe!
 
duh, jamaa lazma alikua mbali!! hii habari sio ya juzi?
Yaelekea huyu Best alikuwa usingizini tangu majuzi halafu kakurupuka bila shaka kakutana na kipindi cha magazeti na ndiyo akaona labda WanaJF wote walikuwa fofofo kama yeye. Kweli washikaji wengine ni mizigo humu na cjui walikaribishwaje.
 
Pole sana kwa waliopatwa na maswahibu..Bajaji na Pikipiki ni "MAJENEZA YANAYOTEMBEA"
Ni kweli majeneza yatembeayo lakini kwa akina sisi yanatusaidia kwa usafiri tuwaombee wenzetu waliotangulia kwa usafiri huo nasi tunafuata
 
Kuna ajali mbaya sana imetokea hapa eneo la posta mjini ifakara, baada ya lori kukosa muelekeo na kuangukia watu, inasemekana zaidi ya watu kumi wamepoteza maisha“Updates”
 
RIP watu msiokuwa na hatia na mliokuwa mmelundikana barabarani kwa kukosa kazi.
 
RIP watu msiokuwa na hatia na mliokuwa mmelundikana barabarani kwa kukosa kazi.
inawezekana watu walikuwa kazini .. wengi wanaokuwa pembezonimwa barabara si wanauza vitumbua na miguu ya kuku? ndio ajira zetu hizi bra
 
Rip watu,af we unaesema walilundikana bila kazi acha kuropoka umejuaje mazingira yenyewe yalikuwaje?kama ni gulio? Imbecile!
 
Kuna ajali mbaya sana imetokea hapa eneo la posta mjini ifakara, baada ya lori kukosa muelekeo na kuangukia watu, inasemekana zaidi ya watu kumi wamepoteza maisha

Mimi nilisema tangu zamani na kushambuliwa hapa hii serikali inayoongozwa na Fisadi papa ambayo haioni umuhimu wa kujenga barabara kwenda na wakati, (hii ni pamoja na kuweka signs, ku-check magari yanayokuwa barabarani) pamoja na kuwa na wataalam wa highway code utawamaliza Watanzania na kuendelea kusaga meno hadi pale watakapoweza kuondoa uvundo na uozo kwenye hii system. Sishangai na ajali bado zitakuja kwa kasi ya radi. Hivi kweli barabara za enzi ya wakati wa Uhuru ambazo zilipanuliwa na kuwekwa lami i.e two way ndizo tunaita highway?

BTW Hivi Majembe Auctions ndio wenye dhamana ya kukagua magari? Niliwahi kuuliza kama wana wataalam waliobobea kwenye nyanja hiyo.
 
Back
Top Bottom