Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Dah poleni sana wafiwa, na majeruhi pia, mkuu T B hautakiwi kupita unatakiwa angalau utoe msaada kwa majeruhi, ila ahsante kwa taarifa
 
Pale mahali ni pabaya kwa ule mteremko wa zaidi ya kilometa 1,malori wana tabia wa "kutikisa gea"(kwenda free ili kuibia mafuta).
Magari yenye mzigo yanaishia kuwashinda na hatimaye kuparamia mengine.
 
pole sana wanakunduchi..
Mungu zilaze roho za marehemu mahali pema
peponi...
Amen!!
 
Ni kweli...daladala,Bodaboda,Malori mawili na Toyota Starlet ambayo watu wote wanne waliokuwemo wamefariki... moja ya ma-lorry lilikuwa limesheheni bia nyingi ambazo wakazi wa Kunduchi machimbo wamejikuta wamepata bia za bure na baadhi yao wameonekana wakiwa wamelewa chakariiiii... na Miili ya waliokuwa kwenye Starlet ilizamika kupelekwa kwenye Garage iliyo Kunduchi Mbuyuni ili iweze kutolewa ni ajali ya kutisha sana... sababu ni Trafiki Police zaidi ya 20 hivi waliosimamisha magari ovyo ovyo... na hii si mara ya kwanza.... Trafiki police hao waliponea chupuchupu kuuawa na wananchi wenye hasira kali... walikimbizwa na Mawe na chupa za bia huku wakimwacha,Trafiki kike aliyepigwa mawe na kuja kuokolewa na wanajeshi wa Jeshi lililopo jirani na eneo hilo... watu nane wamedhibitishwa kupoteza maisha...
 
Duh tutapataje kupona?
Ee MUNGU Tusaidie.
 
Mungu azilaze pema roho za marehemu na awatie nguvu katika kipindi hiki kigumu.
 
tunazidi kupoteza nguvu kazi muhimu saana tu RIP marehemu wote na POLENI wafiwa huu ni wakati mgumu sana kwenu
 
Thanks for info. Taarifa kama hizi ni muhimu sana kwa role ya jf 'be the first to know'.
RIP waliopoteza maisha,
poleni wafiwa.
 
May God rest their souls in eternal peace~AMEN!
 
Nasikia chanzo ni trafiki.......Walisimamisha gari ghafla
imekuwa ni kawaida yao kusimamisha magari maeneo hayo haswa siku za jumamosi... Eneo hilo ni tambarare kabisa ni kati ya mita 200 hadi 300 kutoka njia ya IPTL na njia ya kuingia JKT Quarry... Trafiki inabidi wawajibike kwa hili... Kwani WAMEKUWA KAMA MATEJA... Wanakamata gari moja kabla ya kumaliza walilolikamata wanakamata mengine matano hadi sita... kila Trafiki... sasa wale waliopaki wakiona jamaa wana-behave kama MATEJA wanaondoka ghafla huku wale ambao hawajapigwa Mkono akiongeza kasi... kwa ufupi ndilo lilisosababisha ajali ya leo... VERY SAD.
 
Back
Top Bottom