Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mie ndio usafiri wangu NAMBARI ONE lakini sasa naona umefika muda wa kutafuta mbadala. Poleni sana abiria.
 
Hii kampuni ni hatari sana, likianza kuanguka moja basi tusikilizie tu yatafika hadi kumi, hii si sawa jeshi la polisi muwe makini msisubiri madhara mengine bora msimamishe huduma ya usafirishaji kwa hii kampuni japo kwa muda
 
Mungu utuhurumie na kutuepusha na hili janga la ajali. Mungu uzilaze roho za marehem mahali pema peponi.. Amen.
 
Mabasi mengine mikosi mitupu.
Msipande magari yenye majina yenye maagano na mapepo.
Watu wenye utajiri wa majini makafara damu ni sehemu ya maagano na ibada zao.
 
Duh!hili ni balaa kubwa,poleni sana majeruhi na wafiwa wote!!
 
Ni kweli nchi yetu watu wanakufa kwenye ajali za barabarani kama mzaha tuu, Ufumbuzi unaonekana haupo?? Jambo ambalo siamini kabisa kwamba limeshindikana!! Suluhisho ni moja tu kuwe na Mamlaka inayothibiti madereva wote na usimamizi wa vyombo vyote vya moto vitumiavyo barabara.Ni rahisi sana endapo udereva utafanywa taaluma na siyo kazi baki tuu,
 
Kuna watu wanakalia ofisi wakijiita wathibiti ajali na majanga lakini hakuna chochote wanachofanya. Maisha ya watanzania yanapotea hivi hivi kwa uzembe wa watu..sijui kwa nini utaratibu usiwekwa wa kuwawajibisha pia wamiliki wa vyombo vya usafiri sambamba na madetreva wao pale ajali zinapotokea? (Corporate Liability) ili kuwafanya wamiliki wawe na makini katika kuwasimamia madereva na kuweka vyombo vilivyo salama barabarani?
 
Kuna ajali mbaya imetokea eneo la Buguruni Al Hamza. Bus(Dcm) la Mbagala likiwa linaelekea Ubungo, limepigwa na tela la lori na kutumbukia mtaroni. Abiria wengi wameumia na wanakimbizwa hospital. Nimeshuhudia maiti wawili wakiondolewa eneo la tukio.
Tatizo DCM hayana breki! Anyway naona siku hizi ajali kila siku hazingoji december!Poleni majeruhi ugueni pole. o
 
pole sana kwa wafiwa, na kwa walio jeruhiwa mungu awaponye.
 
Back
Top Bottom