Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

dahh poleni wafiwa...na majeruhi mpate nafuu ya haraka...bila shaka hawa walikuwa wanawahi pasaka na kusugua visikino jijini ....
 
Lakini hii mikoa miwili ya Morogoro na Pwani vimelaaniwa au tatizo liko wapi? ajali za kutisha za mara kwa mara.
 
Poleni sana wafiwa na Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi~AMEN
 
Poleni wafiwa wote. Mungu azilaza roho za marehemu mahali pema peponi.amen
 
Yale maeneo sijui yanatatizo gani,ila nasikia Mindu kuna wanga sana kwa hiyo utakuta watoto wanajifunza uchawi wanauwa tu bila kujali chochote kile
Nadhani umefika wakati sasa wa serikali kutambuwa kuwa uchawi upo na unaumiza watu

pole kwa wafiwa ingawaje haitasaidia chochote kile
 
Tujuze zaidi mkuu, je basi lilikuwa linatoka wapi kwenda wapi

basi lilikuwa linatoka mby kwnd dar. Nipo na mmoja wa majeruhi anasema chanzo cha ajali baada ya lori
kuligonga basi ubavuni na kupinduka. Lori lilikuwa linakwepa kugongana uso kwa uso na gari lingine lililokuwa likitokea dsm!
 
basi lilikuwa linatoka mby kwnd dar. Nipo na mmoja wa majeruhi anasema chanzo cha ajali baada ya lori
kuligonga basi ubavuni na kupinduka. Lori lilikuwa linakwepa kugongana uso kwa uso na gari lingine lililokuwa likitokea dsm!
Mpe pole sana...
 
Watu 2 wamekufa na wengine 15 wamejeruhiwa baada ya bus la Al Said kugongana na lori eneo la Sangasanga Morogoro RADIO1 STEREO
 
Basi ilikuwa inatokea wap na lori pia limetokea wapi? Fafanua kwa faida ya wengi wetu Mkuu tafadhali.
 
Nipo hospitali ya mkoa wa morogoro, kwa mujibu wa dr anayemtibu jamaa yangu ni kuwa watu wawili ndio waliofariki, Mama na mtoto wake mdogo!
Ntaendelea kuwa-update!
 
Kuna mwana jamvi ameshaileta hapa jamvini na anasema ni watu 6 wewe unasema wawili, na amesema yuko pamaoja na majeruhi mmoja wao....
 
Lakini hii mikoa miwili ya Morogoro na Pwani vimelaaniwa au tatizo liko wapi? ajali za kutisha za mara kwa mara.

Mungu azilaze ROHO za marehemu mahali pema peponi na majeruhi wapone haraka.
Hakuna kulaaniwa hapa. Tatizo njia ni nyembamba mno na kuna milima hivyo kingo za barabara ni ndefu sana, likitokea tatizo huwewzi kujitetea. Magufuli akitaka kubomoa wanaleta siasa. Pia magari ni mengi mno kwani inatumiwa na nchi karibu sita Malawi, Zambia, Rwanda, burundi, DRC, Uganda. hivyo ilitakiwa kupewa kipaumbele na kupanuliwa lakini hilo halija fanyika
 
ajali hizi jamani?

kwa kweli madereva wetu si waangalifu.

masikini mama na mwana wamepotea hivi hivi tu!

poleni wafiwa
 
Kazi ya Mungu haina makosa.

Wala hairekebishwi na binadamu yeyote.

Bwana ametoa, Bwana ametwaa.

Sisi tuliwapenda, lakini yeye, amewapenda zaidi.

Shukuruni kwa kila jambo maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu.

Mungu, tunasema ahsante kwa kupenda kuwaua abiria hawa.
 
Kazi ya Mungu haina makosa.

Wala hairekebishwi na binadamu yeyote.

Bwana ametoa, Bwana ametwaa.

Sisi tuliwapenda, lakini yeye, amewapenda zaidi.

Shukuruni kwa kila jambo maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu.

Mungu, tunasema ahsante kwa kupenda kuwaua abiria hawa.

Sio kila ajali huwa ni mapenzi ya Mungu. Zingine huwa ni za uzembe wa madereva ulio wazi kabisa. Poleni wafiwa, na mliojeruhiwa Mungu awape nafuu ya haraka, amen.
 
Kuna mwana jamvi ameshaileta hapa jamvini na anasema ni watu 6 wewe unasema wawili, na amesema yuko pamaoja na majeruhi mmoja wao....

alifanya updates baada ya kupata taarifa rasmi kutoka moja ya hosptal alipo na jamaa yake kuwa ni wawili, mama na mtoto
 
Back
Top Bottom