Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Bai la Alsaedy lililokuwa likitokea mkoani Mbeya limepata ajali jioni hii katika eneo la kijiji cha Sangasanga mkoani morogoro na kuua watu kadhaa.Idadi kamili ya waliopoteza maisha bado haijajulikana lakini kwa walioshuhudia habari hiyo wanasema watu zaidi ya watano wamepoteza maisha hapohapo.
source:Abood radio
 
Endelea kutujuza kwa kirefu juu ya hii habari ya ajari, mwenye taarifa kamili.
 
Msafara wa wabunge wa chadema uliokuwa unaelekea jijini Mbeya umepata ajali mkoani Iringa.

Ajali hiyo ilitokana na lori la mizigo lililokuwa likijaribu kulipita lori lingine, jambo lililosababisha dereva wa gari la mbunge wa Kawe Mh Halima Mdee, kupunguza mwendo kwa ghafla na kugongwa na gari ya Mh. Grace Kiwelu, iliyokuwa nyuma yake na kupinduka.

Wabunge hao pamoja na wengine wawili wa kuteuliwa hawakujeruhiwa sana na wameendelea na safari, wakiwa na m/kiti wao Mh Mbowe kuelekea mikoa ya nyanda za juu kusini ambapo wamepanga kufanya maandamano na mikutano kwa siku 12.

Source;

Habari kwa ufupi, Radio Free Afrika saa 16:00pm leo.
 
asante kama wote wazima wa afya:israel::israel::israel: peoplzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzz
 
Kwa vile ni masuala ya ajali , hatuna budi kusema pole sana . Ila yaonyesha hiyo safari sio yenye heri na haina baraka za mungu
 
Kwa vile ni masuala ya ajali , hatuna budi kusema pole sana . Ila yaonyesha hiyo safari sio yenye heri na haina baraka za mungu

Nakusahihisha, sema ni kazi ya shetani asie watakia mema watu wa Mikoa ya nyanda za juu kusini na CDM kwa ujumla. Usithubutu kumhusisha Mungu kabisa.
 
kazi haisitishwi na ajali we must soldier on and concur our tz back, tupo pamoja wabunge wetu
 
Poleni sana. Tuombe iwe ni ajali tu na si mkono wa mtu maana hata yule Mwakyembe walitaka kumuondoa kinamna, Kolimba wakamkolimba kwa kutamka kwamba CCM imekosa mwelekeo.
 
Msafara wa wabunge wa chadema uliokuwa unaelekea jijini mbeya umepata ajali mkoani Iringa. Ajali hiyo ilitokana na lori la mizigo lililokuwa likijaribu kulipita lori lingine jambo lililosababisha dereva wa gari la mbunge wa kawe Mh Halima Mdee kupunguza mwendo kwa ghafla na kugongwa na gari ya Mh. Grace Kiwelu iliyokuwa nyuma yake na kupinduka. Wabunge hao pamoja na wengine wawili wa kuteuliwa hawakujeruhiwa sana na wameendelea na safari, wakiwa na m/kiti wao Mh Mbowe kuelekea mikoa ya nyanda za juu kusini ambapo wamepanga kufanya maandamano na mikutano kwa siku 12
source ni habari kwa ufupi, radio free afrika saa 16:00pm leo

Ahsante Yesu hakuna aliyepoteza uhai
 
Back
Top Bottom