Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Basi la kampuni ya new force likitokea mbeya kwenda dar limepata ajali maeneo ya wanging'ombe mkoani iringa na kuua watu 4 na wengine kujeruhiwa vibaya.source TBC1,mwenye habari zaidi atujuze.
 
Jamani natoa wito kwa kila mtu kwa dini yake tuliombee Taifa letu maana hizi ajali ni too much sasa
 
Hivi hii nchi ina serikali kweli? How can ajali ua watu leo, kesho, jana, juzi, and serikali haichukui hatua zozote kukabili hali?
 
Kama serikali haitatenga bajeti kufanya upanuzi wa barabara, tutakwisha. Barabara zetu ni nyembamba sana hivyo kosa dogo tu kwishna. Na maeneo yale ukiongeza wabeba ulanzi kwa baiskeli taabu tupu
 
Magufuli akisema tupanue barabara mnasema ana KIBURI,M BABE,sasa mnalia nini ? Msemakweli ktk nchi hii hatakiwi labda aje YESU.
 
Nimewahi panda hili basi la New Force nikitokea Mbeya mwezi wa 10 mwaka jana kwa kifupi hili ni haya ni mabasi ya hovyo kabisa hakuna huduma nzuri kwa mteja lugha chafu nja mwendo wao ni wahovyohovyo mabasi ni mabovu na yanamilikiwa na mwekezaji wa kichina mwenye gereji itwaayo Double Stars iko pale shekilango.

Nikiwa saafarini gari liliharibika dereva na konda wake wakapotea bila kurudi mi nikaondoka na begi langu mizigo mingine nikaiacha nilikuja ambiwa gari lilifika ubungo saa nane usiku na nilipofuatilia mizigo yangu haikupatikana hadi leo na polisi ubungo walishindwa kunisaidia kifupi mwekezaji anawalea. Kwa kweli ni gari bovu engine nyuma moshi unaiingia ndani ya gari live tabu tupu.
 
Mungu aziweke roho za marehemu mahala pema peponi, na sisi marehemu watarajiwa atunusuru na ajali za barabarani
 
Hivi hii nchi ina serikali kweli? How can ajali ua watu leo, kesho, jana, juzi, and serikali haichukui hatua zozote kukabili hali?

apo ikumbukwe kuwa si zaidi ya miaka 10 tu tangu serikali ianzishe ule mradi wa matajiri wa Kufunga Speed gavana!
 
na mabasi ya yanaenda spidi sana jamani yaani mtu unawaza hapa kikitokea kitu mbele tumekwisha
 
Kuna ajali imetokea Morogoro maeneo ya Bwawa la Mindu karibu na njia panda ya chuo kikuu cha Mzumbe, watu 6 wamefariki dunia baada ya basi la al saed linalofanya safari kati ya mbeya na dar kupinduka.
Ntawajuza zaidi.
 
Kuna ajali imetokea Morogoro maeneo ya Bwawa la Mindu karibu na njia panda ya chuo kikuu cha Mzumbe, watu 6 wamefariki dunia baada ya basi la al saed linalofanya safari kati ya mbeya na dar kupinduka.
Ntawajuza zaidi.
Tujuze zaidi mkuu, je basi lilikuwa linatoka wapi kwenda wapi
 
Back
Top Bottom