Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

poleni majeruhi, poleni wafiwa, marehemu wapumzike kwa amani amina
:rip:
 
Kuna mtu kaniambia kwenye hiace amepona dereva tu na dereva wa ngorika ndiyo ametolewa mida hii tangu saa moja naye inasemekana hali yake ni mbaya sana...
 
its really bad.ndo tumemuingiza mmoja wa majeruhi theater,a young girl of 25 with massive internal bleeding.we are going to open her up and try to arrest the bleeding ila therre is little chance she wil survive.muombeeni kwa mungu jamani
 
Hakuna mtu ambae alikuwa hajui kuwa Ngorika ipo siku litauwa,nadhani hata police na vyombo vingine vya barabarani vilikuwa vinasubiri tu siku.ngorika ni kampuni ya mabasi ambayo tangu enzi ilikuwa inasifika kwa speed kali barabarani nahata baadhi ya askari wanajua hilo na walikuwa hata wakidiriki kusifia mwendo wa yale mabasi.binafsi nilishaapa kutopanda lile basi milele baada ya kuona jinsi linavyoenda na hata ukiangalia wahudumu wa bus lile kuanzia conductor hadi dereva ni mirungi tu kwa kwenda mbele,kwa ufupi ni mabasi ambayo yanaonekana matatizo yake yameanzia kwa tajiri wao.
nashauri waziri husika na viongozi wa jeshi la police usalama barabarani wajiuzulu kwa hili.maana tumeshachoka na ajali kila siku.
Ni kweli uliyo yasema Gorika hukimbia sana linalotoka dar hufika Arusha saa saba na kutoka Arusha mpka dar ni wastani wa km 660...hivyo hukimbia wastani 94kph pata picha bado halijasimama kwenye kwenye vituo mbalimbali....
 
Jamani poleni sana.

Mimi nasema ukweli sisi wote kama wahusika wa tatizo hili wananchi, serikali na taasisi zote zinazohuiska hatujalipatia ufumbuzi janga hili.

Njia nzuri ya kupata ufumbuzi wa kudumu wa tatizo ni kuanza na kukubali kuwa hatujapata ufumbuzi. Tukatae propaganada wanazokuja nazo kina wakuu wa traffic kila kukicha kuwa leo tumepata dawa hii kesho ile na ajali zinaendelea kupoteza wapendwa wetu - kukubali kushindwa siyo afande mpinga, fanya hivyo na uombe msaada iitishwe mijadala ya kitaifa ili amkundi mbalimbali yajadili na kutoa mawazo juu ya jinsi ya kuondoa janga hili.
Ni mawazo yangu nasema kwa uchungu.
 
Mfanyakazi mwenzetu amefiwa na baba yake
yey alikuwa kwenye Hiace
Poleni sana wafiwa wote
Mungu awaponye majeruhi wote
Dereva wa Ngorika amefariki
 
Jamani poleni sana.

Mimi nasema ukweli sisi wote kama wahusika wa tatizo hili wananchi, serikali na taasisi zote zinazohuiska hatujalipatia ufumbuzi janga hili.

Njia nzuri ya kupata ufumbuzi wa kudumu wa tatizo ni kuanza na kukubali kuwa hatujapata ufumbuzi. Tukatae propaganada wanazokuja nazo kina wakuu wa traffic kila kukicha kuwa leo tumepata dawa hii kesho ile na ajali zinaendelea kupoteza wapendwa wetu - kukubali kushindwa siyo afande mpinga, fanya hivyo na uombe msaada iitishwe mijadala ya kitaifa ili amkundi mbalimbali yajadili na kutoa mawazo juu ya jinsi ya kuondoa janga hili.
Ni mawazo yangu nasema kwa uchungu.
Abiria ndiyo tatizo kuu mkuu huo ndiyo ukweli....Ngorika inajulikana kwa mwendo kasi lakini watu ndiyo huligombania unategemea nini.....
 
mradi wa speed governor ulikwisha na sasa waliagizwa wote kujiunga na Car track system ambayo inatumia GPS...
 
Hii nayo inahitaji Kikombe cha babu kuponyesha maisha ya watu? Serikali lazima iwe serious sasa na usafiri wa barabarani kwani ajali ni nyingi muno. Mpaka lini? Huu ni uzembe wa madereva wenyewe na watendaji wa serikali.
 
Tuache kulaumu na kunung'unika, tutakufuru mipango ya Mungu ya ajali, kazi ya Mungu haina makosa.
 
Mfanyakazi mwenzetu amefiwa na baba yake
yey alikuwa kwenye Hiace
Poleni sana wafiwa wote
Mungu awaponye majeruhi wote
Dereva wa Ngorika amefariki
Pole sana mkuu, Nasikia dereva angeweza kupona kama wangechukua uamzi wa kumuokoa mapema kuliko kusubilia gari la kuja kunyanyua basi...
 
Dah! Na mimi nilisikia redioni, nafika kazini mfanyakazi mwenzangu analia ndugu yake amefariki katika ngorika. Inasikitisha sana.
 
kuna taarifa kuwa waliokuwa kwenye Hiace wamekufa wote. daladala ilikuwa ikielekea A mjini
 
Tuache kulaumu na kunung'unika, tutakufuru mipango ya Mungu ya ajali, kazi ya Mungu haina makosa.

Taso, nachelea kukubaliana na wewe. Kazi ya Mungu iwe namna hii brabara za Tanzania tu? Mbona barabara za nchi zingine haiko hivi? Tusikwepe ukweli wa uzembe wetu kwa kumtaja Mungu. The fact is, kuna uzembe mkubwa sana katika sekta nzima ya usafirishaji Tanzania na sijui lini tutaamka na kuchukua hatua.
 
Tuache kulaumu na kunung'unika, tutakufuru mipango ya Mungu ya ajali, kazi ya Mungu haina makosa.
Matukio kama haya yapo kwa ajili ya utukufu na uwepo wa Mungu. Lakini mungu hachangui watu wakutokewa na matukio ila watu wenyewe kulingana na mazingira na akili zao. Ajali ipo tangi zamani kama njia mojawapo ya kutoa roho ya binadamu, lakini huwezi kuniambia mungu anamnywesha pombe dereva na kumuamru aendeshe gari ili apate ajali. NO. Dereva aliyelewa yy mwenyewe kajisababishia ajali kwa uzembe na wala siyo mungu wala kazi yake. Tusimsingizie mungu. Mungu katupa uchanguzi wa mema na mambaya, moto na maji, kifo na uzima, etc.
 
Tunawapeni pole wote ambao malengo na mipango yao ya maisha imesitishwa ghafla. Pia poleni sana mliopoteza baba, mama , kaka na dada zetu Mungu atawapa matumaini mapya kwani ingekuwa iko ndani ya uwezo wetu tunge rudisha nyuma mshale wa saa.
 
kwa mwendo wa Ng'orika huwa najisemeaga siku likila mzinga atakayetoka salama amshukuru mungu wake manake speed yake si mchezo
 
Poleni wafiwa. Nawaombea majeruhi wapone haraka. Basi za Ngorika zinafahamika kwa mwendo kasi kuanzia kwa abiria wanaopanda hayo mabasi,askari wa usalama barabarani na mamlaka nyingine husika za serikali zinazosimamia usafiri wa abiria! Lakini pia madreva wa Hiace za Arusha wanajulikana kwa uendeshaji hovyo barabarani. Ukitaka jua ujinga wao kaa pale traffic lights za Sanawari.
 
Back
Top Bottom