Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

mimi nashangaa sana ajari za mabomu zilijirudia na hakuna hatua zozote zilizochukuliwa na leo hii ajali zimejirudia tena hakuna hatua zinazochukuliwa huu ni uzembe wa hali ya juu sana kwa abiria na wasimamizi au washika dau wa usalama barabarani
RIP brodas and sistos!
Hizi ajali zote za wiki hili ni 100% uzembe!
Poleni ndugu wa wafiwa, maana hakuna la ziada tunachoweza kuwaambieni zaidi ya hilo.
 
Ni kweli, hiyo ajari imetokea saa 4 usiku wa kuamukia leo. Haya magari (maroli)mabovu yanayoruhusiwa kutembea kwenye hizi barabara nyembamba inaonekana ndiyo yanasababisha ajari kwa kiasi kikubwa.

Sikubaliani na wazo hili. Ajali zinasababiushwa kwa kiasi kikubwa na uzembe wa madereva.
Nimeshasafiri sana na nimenusurika mara kadhaa na ajali ambazo zinaonekana dhahiri ni uzembe wa madereva.
 
watu kumi na watatu wamekufa na wengne kumi na watatu wamejeruhiwa baada ya basi walilokuwa wanasafiria aina ya coaster lililokuwa linatokea moro kuja dar kugoganga na lori aina ya fuso maeneo ya kibaha,source tymz fm
mwenyezi mungu awape moyo wa uvumilivu.
 
Accidents, drivers are to blame! Wengi waendeshao Fuso za michanga na mizigo hawakuwahi kupata ABC kuhusu driving as a 'profession', wanaona kwenda kwenye Veta ni upotezaji wa muda. Kumbe kule wangejifunza mengi hasa hasa discipline ya barabarani. Matokeo yake utamkuta driver anaendesha kwa ushabiki wa abiria.
 
tufanye nini sasa maana kila siku ajali mara mabomu mala majambazi mala pikipiki yaani mikosimikosi sijui hata wakubwa huwa wanaliona hili!na wanalichukuliaje??
Inasikitisha sana...lakini
malori mengi ni mabovu
yanaharibika na kuegeshwa hovyohovyo
hakuna ishara wala taa zaidi ya majani ambayo usiku hayaonekani vema
mwendo kasi
ulevi
traffic wanakula rushwa
abiria wengi hawaelewi somo,ikitokea mmoja anamlalamikia dereva basi wengine watampinga au kwa uoga na ignorance watakaa kimya
Jamani mambo haya mpaka lini???
 
tuandamane
attachment.php
 
Inasikitisha!!! jamani malori mabovu yanayopaki njiani bila kuweka tahadhari!!
 
RIP ...hii idadi ya 13 imekaaje wazee? Ile ya 5 Star marehemu ni 13, na hii marehemu ni 13..majeruhi ni 13....13, 13....!!is there anytng behind the digit 13???
 
Madereva wazembe wanapoteza maisha yetu.

Kuna umuhimu wa mamlaka husika kuliona hili na kulivalia njuga.
Kwa kweli hawa madereva wapimwe akili na uwezo wao wa kumudu barabara kabla ya kupewa magari, pia umri wa kuendesha masafa uangaliwe hawa vijan bange nyingi
 
Pamoja na kuwaombea marehemu na waliojeruhiwa, wakati umefika sasa kama taifa kutafuta suluhisho la kudumu la ajali. Inavyoonekana, kila tunalobuni wala halileti nafuu... speed gavana hazitumiki tena (sina hakika kama zingetumika ipasavyo matokeo yake yangekuwa nini), mabasi yasiendeshwe usiku, bado haifuatiliwi (ajali hii imetokea saa 4 usiku), trafiki wamegeuka kuwa wala rushwa barabarani (wakiwa wakali madereva wanalalamika sana). Tufanye nini sasa?
 
Habari za uhakika kutoka mkoani Morogoro zilizotua katika mtandao huu hivi sasa zinadai kuwa abiria zaidi ya 40 wamenusurika kifo baada ya basi la kampuni ya Upendo ambalo walikuwa wakisafiria kutoka Dar es Salaam kwenda Njombe mkoani Iringa kupinduka eneo la Mikumi mkoani Morogoro

Hii ni ajali ya nne kutoka mkoani kwa kipindi kifupi cha mwezi mmoja baada ya ajali ya wasanii wa 5 star leo bado mzimu wa ajali umeendelea kuuandama mkoa wa Morogoro.

Taarifa hizo za uhakika ambazo zimepata kuthibitishwa na jeshi la polisi mkoa wa Morogoro zinadai kuwa hakuna aliyepoteza ,maisha katika ajali hiyo japo undani zaidi waajali hiyo utaupata hivi punde.
 
mimi nilikuwa nyuma ya basi hilo nikiwa na basi la Sumry...basi hilo lilianza kuyumba ghafla na baada ya hapo likapoteza uelekeo kabisa na kupinduka likageuka kule lilikotoka(daslam)...hata sisi almanusura tulivae basi hilo na leo yalikuwa ni msururu wa mabasi kama sita hivi.kwa hiyoo ni Mungu tu amesaidia.....

ki ukweli hakuna aliyepoteza maisha kwenye ila watu wamejeruhiwa vibaya sana...kuna mtot mmoja wa kiume miaka 13 amevinjika miguu yote miwili na mguu wa kushot ndi unaning'inia mfupa uko nje.....lakini ule wa kulia umeondka kabisa....mimi binafsi ndiye niliyembeba mtoto yule kumtoa chini ya gari na ilibidi kubadili nguo pale maana nilitapakaa damu sana wakati tunawatoa wale majeruhi

wale majeruhi walichukuliwa kwenda hosp morogoro...lakini katika hali ya kushangaza kuna gari la serikali lilipita pale na kukuta njia imefungwa na dreva wa gari hilo akaombwa kubeba baadhi ya majeruhi ..kwa kiburi chake akagoma na kuliondoa gari kiasi kwamba kidogo asababishe ajali nyingine ya kugonga watu.....kwa kuwa njia ilikuwa imefungwa hakufika popote.....akasimama ndipo watu wakajaa pale na kutoa upepo tairi zote na kutoboa matairi...........



 
Mhm, sijui ndo yale makafara ya serikali niliyosikia kipindi cha nyuma?...
 
Tuzidi kuuomba atunusuru jamani,ajali zimekuwa nyingi sana.EEE MWENYEZI MUNGU TUHURUMIE.
 
Mhm, sijui ndo yale makafara ya serikali niliyosikia kipindi cha nyuma?...
Lakini wale walinzi waalio ongezwa kwa mkuu na yule bingwa wa utabiri si nao huwa wanakula ?mmmmmmmmhhhh!!sitaki kuamini kua chakula chao ndio hicho.

Poleni wote mlio nusurika siku moja Bwana atawaaibisha wote waendao kinyume na mapenzi yake.
 
Tatizo ni serikali ya CCM na TANROADS Watanzania watendelea kufa kwa hizi ajali koko hadi pale tutakapoweza kupata akili ya kuwaondoa mafedhuli wanaokwapua fedha za walipa kodi kwa maslahi yao binafsi.
 
Back
Top Bottom