Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Hii ndio miezi yao ya kutoa kafara,next week utasikia hood
 
Hii ndio miezi yao ya kutoa kafara,next week utasikia hood
kuna tetesi kuwa ni matajiri wa mabasi wanafanyiziana ili kunyang'anyana abiria. Baada ya Abood kufanya ajali majuzi, abiria wote wamehama, hivyo lazima yaliyobakia nayo yafanye ajali ili uwanja wa ushindani uwe sawa!.
 
Ni kweli jamaa wawili wamefariki watumishi wa Jeshi la Magereza kwa majina mmoja ni RAJABU alikuwa mhasibu wa mkoa wa Pwani. Walikuwa wanatoka Kibaha wanaenda Wami Vijana kwa ajili ya shughuli za kikazi ndipo walipokutana na ajali hiyo ambayo ilikuwa uso kwa uso. Dereva wa gari amepona lakini aliyekuwa msindikizaji na huyo ofisa wametangulia mbele ya haki. Mungu awalaze mahali pema peponi. Ameen.

Marehemu Rajabu alisoma CBE Dar 2001-2002 Diploma in Accountancy baadae UDSM 2003 - 2006 B. Com in Accounting.
 
Mungu awapokee na kuwapumzisha peponi. Awarehemu makosa yao.
 
Habari tulizozipata punde zinasema basi AM lililokuwa likitoka Serengeti kwenda Bunda limepata ajali.Watu wawili wamekufa na wengine hamsini wamejeruhiwa.
 
Mungu awarehemu marehemu. Majerui Mungu awaepushe na vilema vya kudumu. Inauma sana hasa pale ambapo tutaambiwa kuwa ni uzembe wa Dereva au Mmiliki.
 
Habari tulizozipata punde zinasema basi AM lililokuwa likitoka Serengeti kwenda Bunda limepata ajali.Watu wawili wamekufa na wengine hamsini wamejeruhiwa.

Ajali imetokea sehemu gani?
 
  • Basi la AM Coach lililokuwa linatoka Serengeti kwenda Bunda limepata ajali. Watu 2 wamekufa na 50 wamejeruhiwa.
Source: Home
 
WATU wawili wamekufa papo hapo na wengine 70 kujeruhiwa vibaya baada ya basi walilokuwa wakisafiria kutoka Mugumu wilayani Serengeti kwenda wilayani Bunda kuacha njia na kupinduka.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Mara, Mambo Masige, amesema ajali hiyo ilitokea jana saa 4:00 asubuhi, katika eneo la Chirige mjini Bunda.

Ajali hiyo imelihusisha basi la kampuni ya A.M Coach, aina ya Scania, lenye namba za usajili T. 740 AQD, mali ya Ahmed Mhamed, mkazi wa mjini Bunda.

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Dk. Rainer Kapinga alisema waliokufa papo hapo ni
wanawake lakini majina yao hayajafahamika na miili yao imehifadhiwa katika Hospitali ya teule ya Bunda.

Dk. Kapinga alisema majeruhi waliopokelewa hospitalini hapo ni 70 wanawake wakiwa ni 30 na wanaume 40 na kati yao, watoto wadogo wakiwa 12.

Majeruhi wengine watano wamepelekwa katika hospitali ya rufaa ya Bugando jijini Mwanza, kutokana na hali zao kuwa mbaya.

Dk. Kapina aliwataja baadhi ya majeruhi ambao wamepelekwa Bugando kuwa ni Fatuma Koleni, Anania Manyama na mwingine aliyetambuliwa kwa jina moja tu la Pendo.

Aliwataja majeruhi ambao wamelazwa katika hospitali ya Bunda kuwa ni Fatuma Wambura (9), Wambura J. (6) na Happy Jonh, wakazi wa kisiwani Ghana, mkoani Kagera.

Wengine ni Stephen Henry (11) na Janet Henry (12), wote wakazi wa Kambarage mkoani Shinyanga, Guti Guti (7), mkazi wa Sanzate Bunda, Silora Charles (4), Judith Charles (7) na Agripiner Charles (11), wakazi wa Mugumu Serengeti.

Wengine ambao ni wakazi wa Mwanza na umri kwenye mabano ni Lusia Julius (11), Neema Samwel (12), Grace Maunda (6) na Bahati Maunda (15), Christina Magige (11), Daines Kunani (10), Pendo Suleimani (9) na Festo Amos (10) mkazi wa Busweru Mwanza.

Wengine ni Stephen William (8, Mugumu), Sesilia Alphan (16, Mwanza), Frenus Peter (14, mwanafunzi wa sekondari ya Maina), Robert Makindi (16, mwanafunzi wa Makoko Seminari), Horuman Amos (12, Busweru Mwanza) na Dominick Juma (18, Mugeta Bunda) na Simon Joseph (18, Bariadi Shinyanga).

Wengine ni Godfrey Rukaka (21), Tabu Chamriho (40), Chacha Aramali, Wambura Julius (20), Mgendi Stima, Igone Kihiri (32), Nyamhanga Mrimi (81), Mariamu Bira (20), Scholastika Mashauri (21), Mengi Sao (30), Grishon Namoni (22), Mango Maliganya (18), Bahati Guti (60), Mary Sumara (29) na Masatu Mang'ari (20), wote wakazi wa wilayani Bunda.

Wengine ni Mashaka Julius (22), Julius Masirori (52), Wambura Julius (20) na Martha Satuta (30), ambao wote ni wakazi wa Isenyi wilayani Serengeti. Wengine ni Hellena Mang'oa (19), Kichere Ngochoge (33), Asha Hassan (39), Theresia Rabani (46), Enos James (20), Samson James (23) na Emilliana Charles (27), ambao wote ni wakazi wa Mugumu wilayani Serengeti.

Wengine na umri na makao yao kwenye mabano ni pamoja na Buyugu Nchege (43, Sengerema), Chacha Maseke (22, Igunga Tabora), Mkula Mashauri (25, Sengerema), Raphael Sakenge (75, Ngasamo Magu) na Christopher Malongo Bukani (62, Kwimba Mwanza).

Wengine ni Daud Nomolomo (42, Sengerema Mwanza), Michael Ezekiah (35, Iramba Singida), Nyambesa Sarora (30, Itembiri Serengeti), Yohana Semakweli (33 Butimba Mwanza), Mary John (45, Kambarage Shinyanga) na Amos Makanga (30, Busweru Mwanza).

Majina ya majeruhi wengine hayakupatikana mara moja kutokana na kuwa kwenye vyumba vya upasuaji.
HabariLeo | Wawili wafa katika ajali, 70 waliojeruhiwa watajwa
 
Kuna ajali imetokea katika stand kuu arusha ilyohusisha bus la kampala coach. Watu watatu anaofiwa kuwa wamekufa.

Gari ilo lilikuwa nina rudi nyuma ili kupaki, ila dreva alishinda kulimudu na kipitiliza ukingo na kugonga na kukanyaga watu waliokuwa wana pita na waliokuwa wanafanya biashara - Wamachinga.

Tutazidi kuwapa habari
 
Mkuu asante kwa taarifa. Ila mkuu avatar imeniua macho sioni tena
 
R.I.P.
Arusha imekuwaje ndg zangu?
Anyway, Good will stand!
 
Bad news...
Tutafuatilia...
Sitoi RIP maana haijathibitishwa kama wamefariki!
 
Kilichotekea ni mtu ambaye nadhani konda, alirudisha gari nyuma, akagonga kibao fulani, baada kugoga akashtuaka, badala ya kushika break, akaongeza mafuta ndo gari likarudi nyuma kwa kasi na kugonga watu.
 
Kilichotekea ni mtu ambaye nadhani konda, alirudisha gari nyuma, akagonga kibao fulani, baada kugoga akashtuaka, badala ya kushika break, akaongeza mafuta ndo gari likarudi nyuma kwa kasi na kugonga watu.


Thanks, endelea kutuhabarisha mkuu.
 
Kilichotekea ni mtu ambaye nadhani konda, alirudisha gari nyuma, akagonga kibao fulani, baada kugoga akashtuaka, badala ya kushika break, akaongeza mafuta ndo gari likarudi nyuma kwa kasi na kugonga watu.

Stendi ya Arusha haina utaratibu kabisa imejaa mawakala, wapiga debe polisi na machinga.
 
Back
Top Bottom