Watu wawili wamekufa papo papo na wengine zaidi ya 70, wamejeruhiwa vibaya, baada ya basi walilokuwa wakisafiria kutoka Mugumu wilayani Serengeti, kuelekea wilayani Bunda, mkoani Mara kuacha njia na kuanguka.
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Mara, Mambo Masige, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo, iliyotokea jana majira ya saa 4:00 asubuhi, katika eneo la Chirige, mjini Bunda.
Ajali hiyo ililihusisha basi la kampuni ya A.M Coach aina ya Scania namba T. 740 AQD, mali ya Ahmed Mhamed, mkazi wa mjini Bunda.
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Dk. Rainer Kapinga, alisema watu wawili ambao wote ni wanawake walikufa papo hapo na kwamba majina yao bado hayajafahamika, na miili yao imehifadhiwa katika Hospitali ya DDH-Bunda.
Dk. Kapinga alisema majeruhi waliopokelewa hospitalini hapo ni zaidi ya 70, ambapo 12 kati yao ni watoto wadogo, na kwamba 30 ni wanawake na 40 ni wanaume.
Alisema majeruhi wengine watano wamepelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando jijini Mwanza, kutokana na hali zao kuwa mbaya.
Dk. Kapinga aliwataja baadhi ya majeruhi ambao wamepelekwa Bugando kuwa ni Fatuma Koleni, Anania Manyama na mwingine aliyetambuliwa kwa jina moja la Pendo.
Majeruhi ambao wamelazwa katika Hospitali ya DDH-Bunda ni Fatuma J. Wambura (9), Wambura J. (6) na Happy John, wakazi wa kisiwani Ghana, mkoani Kagera.
Wengine ni Stephen Henry (11) na Janet Henry (12), wote wakazi wa Kambarage mkoani Shinyanga, Guti Guti (7), mkazi wa Sanzate Bunda, Silora Chalres (4), Judith Charles (7) na Agripiner Charles (11), wakazi wa Mugumu Serengeti.
Wengine ni Lusia Julius (11, Mwanza), Neema Samwel (12, Mwanza), Grace Maunda (6) na Bahati Maunda (15 Mugumu), Chrisitina Magige (11, Mwanza) Daines Kunani (10, Mwanza), Pendo Suleimani (9, Mwanza) na Festo Amos (10, Busweru Mwanza).
Wengine ni Stephen William (8, Mugumu), Sesilia Alphan (16, Mwanza), Frenus Peter (14, mwanafunzi wa sekondari ya Maina), Robert Makindi (16, mwanafunzi wa Makoko Seminari), Horuman Amos (12, Busweru Mwanza) na Dominick Juma (18, Mugeta, Bunda) na Simon Joseph (18, Bariadi, Shinyanga).
Wengine ni Godfrey Rukaka (21), Tabu Chamriho (40), Chacha Aramali, Wambura Julius (20), Mgendi Stima, Igone Kihiri (32), Nyamhanga Mrimi (81), Mariamu Bira (20), Scholastika Mashauri (21), Mengi Sao (30), Grishon Namoni (22), Mango Maliganya (18), Bahati Guti (60), Mary Sumara (29) na Masatu Mang'ari (20), wote wakazi wa wilayani Bunda.
Wengine ni Mashaka Julius (22), Julius Masirori (52), Wambura Julius (20) na Martha Satuta (30), wakazi wa Isenyi wilayani Serengeti.
Wengine ni Hellena Mang'oa (19), Kichere Ngochoge (33), Asha Hassan (39), Theresia Rabani (46), Enos James (20), Samson James (23) na Emilliana Charles (27), ambao wote ni wakazi wa Mugumu wilayani Serengeti.
Wengine ni Buyugu Nchege (43, Sengerema), Agnes na Chacha Maseke (22, Igunga Tabora), Mkula Mashauri (25, Sengerema), Raphael Sakenge (75, Ngasamo Magu) na Christopher Malongo Bukani (62, Kwimba, Mwanza).
Wengine ni Daud Nomolomo (42, Sengerema Mwanza), Maico Ezekiah (35, Iramba, Singida), Nyambesa Sarora (30, Itembiri, Serengeti), Yohana Semakweli (33 Butimba Mwanza), Mary John (45, Kambarage Shinyanga) na Amos Makanga (30, Busweru, Mwanza).
Majina ya majeruhi wengine hayakupatikana mara moja kutokana na kuwa kwenye vyumba vya upasuaji.
Watu walioshuhudia ajali hiyo wamesema walishutukia gari hilo linakosa mwelekeo na kugonga nguzo ya umeme na kisha kupinduka, kabla ya kumpitia mwanamke mmoja aliyekuwa akitembea njiani na kufa papo hapo.
CHANZO: NIPASHE