Mi naona tutafute sababu za kisayansi zaidi, hii habari ya kwamba hizi ajali na damu zinazomwagika ni kafara ya uchaguzi wa 2010 na kwamba wakuu wanapishana kuelekea bagaheart kuwaona wazee wawasafishie njia sidhani kama ina mantiki sana!!
Inaweza ikawa kweli..maana wanasiasa wetu wana mambo ya 'kiswahili' sana, lakini je tuta prove vipi? Ni wakati wa jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani, Tanroad, madereva na wamiliki wa vyombo vya usafiri na wadau wengine kuangalia kiundani vyanzo vya hizi ajali na kuja na majibu muafaka.