Mdau, Hili kweli ni Tatizo kubwa kwa Taifa letu, kwanza nguvukazi kubwa inapotea,Pili resources zetu ni Haba hasa madawa na hospitals.
Ajali za magari zinaongezeka kutokana na sababu kubwa moja. Siku hizi chanzo kikubwa cha kusafirisha mizigo na abiria ni barabara, Miaka ya nyuma Reli za TRC na TAZARA zilitumika sana, pia Meli za Shirika la Reli. Kwa sasa barabara zetu zime jaa misururu ya magari makubwa yame beba Macontainer,na Mizigo mingine kama Carterpillar za migodi na ujenzi wa barabara. Mengi ya magari haya, yana mwendo mdogo kutokana na mizigo mizito au ubovu. hii inalazimisha magari mengine kuya overtake na hapo ndipo ajali nyingi hutokea.
Sasa nani alaumiwe?
Kama TRC isingehujumiwa,Macontainer mengi yange safirishwa kwa njia ya Reli hivyo ajali nyingi zinge epukika.