Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Ajali ya Tanga ninauhakika kamanda wa Tanga alihojiwa akatoa hiyo idadi Watu 27 ila kama unavyojua inaweza kuongezeka saa yoyote..
Ajali iliyotokea Tanga ndiyo hiyo hiyo niliyosema kwenye post yangu, ila bus ilikuwa ikitokea Arusha kwenda Dar na kwa taarifa ya habari tbc1 saa 2 watu 33 walikuwa wameshakuwa comfirmed dead.
Mark you hawa kwa hesabu ya haraka ni nusu ya abiria wote wa bus maana mabasi ya Mohamed huwa hawabebi xtra passanger!
 
Nimesikia sasa hivi kwenye NPR ( National Public Radio) kuwa kuna ajali imetokea Tanzania ( mji haukutajwa) ambapo basi limeligonga lori na watu 33 wamefariki.
 
Basi la Mohamed Trans laua 27 mkoani Tanga


na Mwandishi Wetu




ZAIDI ya watu 27 wamefariki dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa katika ajali mbaya ya barabarani, iliyotokea mkoani Tanga jana.
Habari kutoka mjini Tanga ambazo Tanzania Daima ilizipata kutoka kwa baadhi ya walioshuhudia ajali hiyo, zilisema kuwa ajali hiyo ilihusisha basi la Kampuni ya Mohamed Trans, lililokuwa likitokea mjini Mombasa, kwenda jijini Dar es Salaam.


Hata hivyo mashuhuda hao walisema kuwa idadi ya watu waliofariki dunia katika ajali hiyo ilifikia 30 hadi jana saa mbili usiku na kazi ya uokoaji ilikuwa ngumu kutokana na miili mingi kung’ang’ania kwenye mabati ya basi hilo.


Akizungumza na Tanzania Daima jana kwa njia ya simu, Kamanda wa Polisi mkoani Tanga, Simon Sirro, alisema kuwa ajali ilitokea majira ya saa 10 alasiri katika Kijiji cha Kombo, wilayani Korogwe.
Alisema basi hilo lilipata ajali hiyo baada ya kupasuka matairi yake yote mawili ya mbele na kupoteza mwekekeo na kisha kugongana uso kwa uso na lori lililokuwa limesheheni masanduku ya bia.
“Natoka eneo la tukio kwenda katika Hospitali ya Wilaya ya Korogwe, waliofariki katika eneo la tukio walifikia 27, akiwamo dereva na utingo wa lori na wengine wengi waliopoteza maisha, walikuwa ndani ya basi hilo. Ni ajali kubwa na ya kutisha kwa kweli,” alisema Kamanda Sirro.


Alisema kati ya waliofariki dunia, wanaume ni 21 na wanawake sita, ambao walifariki dunia mara baada ya ajali hiyo kutokea katika eneo la tukio.


Alisema kuna uwezekano mkubwa wa idadi ya waliofariki dunia kuongezeka, kwani wapo waliofariki dunia wakati wakiwa njiani kupelekwa hospitali kwa ajili ya matibabu.




Kwa mujibu wa Kamanda Sirro, majina ya waliopoteza maisha katika ajali hiyo kubwa kutokea katika siku za hivi karibuni, yanatarajiwa kutangazwa leo.


Moja ya matukio ya kusikitisha ni pale baadhi ya wananchi wanaoishi jirani na mahali ajali hiyo ilipotokea, kupora na kuiba vitu mbalimbali kutoka kwa majeruhi na marehemu waliokuwa wakisachiwa kwenye mifuko yao.


Vitu vilivyokuwa vikiporwa ni simu za mkononi, fedha, saa, viatu na mabegi, mali ya majeruhi na watu waliopoteza maisha katika ajali hiyo.


Ajali nyingine kubwa ya aina hiyo, ilitokea mkoani Tanga Januri 12 mwaka huu ambapo watu 27 walifariki dunia baada ya basi la Kampuni ya Tashrif walilokuwa wakisafiria kutoka Dar es Salaam kwenda Tanga kuligonga lori lililokuwa limebeba shehena ya magogo.


Wengi waliokufa ni abiria waliokuwa wamesimama katikati ya basi hilo wakiwa kwenye harakati za kutaka kushuka, ambapo walijikuta wakichanwa vipande vipande na magogo hayo yaliyokuwa kwenye lori hilo lililoegeshwa kando ya barabara hiyo.


Basi la Mohamed Trans laua 27 mkoani Tanga
 
Aisee mbona leo ajali mbili mfululizo? Tanga na Iringa. Haya majini yamekosa chakula ndo yameenda kunyonya damu za watu barabarani. Eeee MUNGU wa mbinguni iponye nchi yetu na pepo/majini yanayoua raia wetu. Poleni wafiwa MUNGU awatie nguvu.

Hakuna cha majini ni over speeding and carelessness of the drivers.
 
Ajali iliyotokea Tanga ndiyo hiyo hiyo niliyosema kwenye post yangu, ila bus ilikuwa ikitokea Arusha kwenda Dar na kwa taarifa ya habari tbc1 saa 2 watu 33 walikuwa wameshakuwa comfirmed dead.
Mark you hawa kwa hesabu ya haraka ni nusu ya abiria wote wa bus maana mabasi ya Mohamed huwa hawabebi xtra passanger!
Jana mimi siku pata nafasi ya kuangali taarifa ya habari lakini ninavyo jua mimi taarifa ya habari TBC1 jumapili huwa saa moja..vile vile tuwe makini wakati wa kupost thread kwasababu wengine wana weka kwenye jukwaa la siasa matokeo yake kunakuwa na duplication.... thread yako na yangu zilitofautina dkk 1.. anyway Mods wapo..
 
Sumry zimekuwa zinapata ajali maeneo yaleyale! Kulikoni? Isije ikawa kama Abood ambao huwa wanatoa sadaka ya ajali ya basi moja kila wanapoleta mabasi mapya!
Mkuu yaani kama ulikuwepo nilishawahi kuona sumry maeneo ya msitu fulani pale mafinga! Ile gari ilikuwa imegonga ng'ombe na kuua mtu mmoja pale pale kwa kubanwa na viti! Na jana tena ama kweli me nimeanza kuhisi kitu fulani pale lazima kunatakuwa na mtego sio bure! Wataalamu wambo yetu yalee ya mitego inabidi wafike pale ili kuweka mambo sawa!
 
picha ya ajali ya Tanga ya basi la Mohammed Trans

ajali-mohamedtrans-26-07-2009-2.jpg


Picha tu inatuonyesha kuwa basi lilikuwa mwendo mkali sana. Serikali naona kama hawako serious, mbona nchi nyingine speed ya mabasi ni 80km/hr na hakuna anayethubutu ku-over speed?
 
Aisee mbona leo ajali mbili mfululizo? Tanga na Iringa. Haya majini yamekosa chakula ndo yameenda kunyonya damu za watu barabarani. Eeee MUNGU wa mbinguni iponye nchi yetu na pepo/majini yanayoua raia wetu. Poleni wafiwa MUNGU awatie nguvu.

Hizo imani zenu za kichawi ndo zinasababisha albino wauawe halafu mnashangaa.... Wewe nini kina kusukuma mpaka useme majini, wakati ni mi-dereva yetu ya mabasi isiyokuwa na akili pamoja na serikali ya CCM isiyojua hata kujifunza nchi zingine wanafanya nini kudhibiti ajali. Wakikurupuka tu utasikia mara speed governor mara utumbo fulani, pumbafu kabisa
 
Rest In Peace!! Naamini siku misafara ya makuhani itakapo anza kupata ajali mbaya kama hizi na kuwaopoa wakiwa maiti ndipo wahusika watakaobaki hai wataamka toka usingizini na kuanza kujenga tanzania iliyo bora kwa wote!!
 
Kila jambo ni kumshukuru mungu kwani heri na shari zote anapanga yeye, lakini hiki kawaida huwa kinapatikana ajali nyingisana tanzania sijui tatizo ni nini ndg zangu,mwenye kujua chanzo atujuze,mungu awape nafuu majeruhi wote wapate kupona haraka na azipokee kwa wema roho za marehemu wote
 
Hizo imani zenu za kichawi ndo zinasababisha albino wauawe halafu mnashangaa.... Wewe nini kina kusukuma mpaka useme majini, wakati ni mi-dereva yetu ya mabasi isiyokuwa na akili pamoja na serikali ya CCM isiyojua hata kujifunza nchi zingine wanafanya nini kudhibiti ajali. Wakikurupuka tu utasikia mara speed governor mara utumbo fulani, pumbafu kabisa


Mkuu hapo kuna ka kweli fulani. Kuna member aliyetaja habari za majini!!! Asilimia kubwa ya hawa owners wa magari ya abiria na mizigo hasa haya makubwa huwa wanafanya kazi hizo kwa ushirikina wa ajabu sana. Wana majini na madawa ya mazindiko ambayo kwa mara nyingi ni lazima yapate chakula ili yaweze kutema pesa. Fanya ka uchunguzi utakuta hawa owners kuna miiko yao fulani katika kufanya kazi zao!!!! Ni kwamba ukiingia ndani ya haya mabasi omba Mungu isiwe siku hiyo ni siku ya kafara!!!!

Ni kweli pia kuwa ajali nyingine zinatokana na uzembe wa drivers na nyingine ni hitilafu za kawaida za vyombo vya moto!!!

Poleni sana wafiwa. Ila pia trafic wetu ni vyanzo vya ajali nyingi maana wanakubali rushwa sana na ndiyo drivers wana kiburi sana hata ukipiga kelele apunguze mwendo huwa wana dharau maana anajua kuna mkubwa anamlinda yeye au bosi wake!!! Je tutafika??!!!
 
Inasikitisha, leo nimetoka dar na basi la mohamed trans na tulitangulizana na basi la sumry, lilikuwa likienda mwendo wa kawaida, ila nadhani kunatatizo moja kwa hawa wamiliki wa magari, hawafanyi maintanance pale inapohitajika, kama wanafanya itakuwa zima moto.
 
ukiona jina la basi lenyewe tu, kimbia mbio. maana ni la kidini kwenda mbele.sasa wewe utapandeje basi la watu wanaofuga majini? wanatoa sadaka wenzio. hata haliwaumi. wengi tulikuwa kwenye biashara za aina hiyo zamani kabla hatujampokea Yesu na kuacha maovu, tunajua kinachofanywa. hawa jamaa muda wao umeisha,biashara zao ndo za hivyohivyo, HAPO YAMEDONDOKA NI SADAKA KWA SHETANI UJUE HAPO WATATOA MABASI KAMA HAYO HATA KUMI MAPYAAAA. kuna asojua hili?
 
Hebu tusome kuhusu ajali ya Iringa
Katika ajali ya mkoani Iringa basi la Kampuni ya Sumry Namba T 974 AWL Nissan, likisafiri kutoka Dar es Salaam kwenda Tunduma, mkoani Mbeya jana lilipata ajali na kuua abiria mmoja.

Habari kutoka Iringa zinaeleza ajali hiyo ilitokea saa 10:30 jioni katika eneo la Malangali, mkoani Iringa zinaeleza kuwa ajali hiyo ilitokea baada ya tairi la basi hilo kuchomoka na kupinduka.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa, Evarist Mangalla, alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo, lakini akasema kuwa polisi walikuwa wakikusanya taarifa za awali kuhusu ajali hiyo.

Mangalla alisema kuwa ajali hiyo imejeruhi watu 10 wakiwamo watoto watatu na baadhi yao wamepelekwa hospitaliya Ilembula kwa matibabu.

Imeandikwa Mawazo Malembeka, Iringa.
CHANZO: NIPASHE
 
Hellow wana jamii..
Ninaomba tusaidiane mawazo na ushauri pia.
Kumekua na ajali nyingi sana haswa kwa barabara za Kwenda mikoa ya Kaskazini,Juzi tumesikia ajali mbaya sana ya basi la Mohamed Trans na limeua watu sio chini ya 20, nini kifanyike na kukabiliana na ajali hizi? kitu hiki kidhibitiwe kwa njia gani kuokoa maisha yetu?
Nani mzembe ni askari wa usalama barabarani? au ni madereva wa mabasi kwa mwendo kasi wanaokua nao.??
 
Last edited:
Hellow wana jamii..
Ninaomba tusaidiane mawazo na ushauri pia.
Kumekua na ajali nyingi sana haswa kwa barabara za Kwenda mikoa ya Kaskazini,Juzi tumesikia ajali mbaya sana ya basi la Mohamed Trans na limeua watu sio chini ya 20, nini kifanyike na kukabiliana na ajali hizi? kitu hiki kidhibitiwe kwa njia gani kuokoa maisha yetu?
Nani mzembe ni askari wa usalama barabarani? au ni madereva wa mabasi kwa mwendo kasi wanaokua nao.
 
Ajali inatokea mtu anapokwenda mbio sana au anapokwenda pole pole sana. Awali ya yote lazima isemwe kwamba ajali ya tairi bovu kupasuka haiwezi kuitwa ajali,kwa sababu ni jambo ambalo linategemewa kutokea.
 
Ajali hizi nyingi zinatokkea kwa sababu ya uzembe wa madereva, na pia factors nyingine:
1. Kasi kubwa bila kuangalia uimara wa matairi ya magari yao. Inatakiwa baada ya km kadhaa kusimama na kuangalia hali ya tairi. Siyo kwenda tu mpaka afike. Yanapata joto sana hasa kwenye lami

2. Ajali nyingi zinatokea kwenye ku-overtake bila kuwa na uhakika wa usalama mbele ya gari linalopitwa. Hizi ajali ni nyingi mno. Na huu ni uzembe wa madreva. Unakuta dreva ana-overtake kwenye kona tena akiwa mkuku, au kwenye bonde/mwinuko ambapo upeo wake wa kuona ni mdogo. Kuna haja ya madreva kurudi driving school. Na pia kupewa driving ethics kwa ajili ya magari ya kubeba watu wengi. Nasema hili la ethics kwa sababu wakati mwingine unashangaa madreva wa mabasi wakishindana utafikiri wako kwenye Formula One.
Lakini nafikri pia tutakapokuwa na barabara za njia mbili zitasaidia sana kwa vile mwenye ku-overtake hatakuwa na hatari ya kukutana na mwingine akija kwa upande wake

3. Umri wa madreva pia ni tatizo. Madreva baadhi ni vijana mno. Unakuta wanaendesha gari bila umakini unaotakiwa, tena wengine wakiwa wamekunywa. Serikali iweke umri maalum kwa waendesha mabasi. Labda wawe watu wa makamu ambao wanajali maisha ya watu. Wanathamini dhamana waliyopewa na jamii ya kubeba watu kuliko madreva vijana.

4. Dereva mmoja kuendesha kwa muda mrefu. Kuna kuchoka sana na kupunguza umakini. Matajiri wafualiwe na serikali wawe na madreva wa akiba ili waachiane mmoja anapochoka.

5. Uzembe wa wasimamizi wa usalama barabarani (askari). Hawajali. Hii pia inasababishwa na rushwa. Wangekuwa wakali ingeweza kupunguza ajali hizi nyingi.

6. Matairi yenyewe: labda kuna haja ya kuagiza matairi ya pekee kwa ajili ya nchi za joto kama zetu. Matairi mengi kwa kweli hayastahimili mwendo wa muda mrefu ndo maana yanapasuka. Yafaa kufanya uchunguzi na kuainisha tairi imara.
 
Back
Top Bottom