Mlipuko mkubwa waitikisa Arusha!

Mlipuko mkubwa waitikisa Arusha!

Usiku wa April 13 2014 kwenye baa
iitwayo ‘Arusha night park’ iliyopo Mianzini
Arusha ambayo siku zote ni miongoni
mwa sehemu zinazokua na mkusanyiko wa
watu wengi kuanzia jioni, limerushwa
bomu wakati watu mbalimbali wakitazama mpira.

Mkuu wa mkoa wa Arusha
ambae ni kiongozi wa Kamati ya ulinzi na
usalama ya mkoa ambae amethibitisha
kwamba ni watu 15 wamejeruhiwa
kwenye mlipuko huo.
Anasema wote wamepelekwa hospitali
ambapo uchunguzi wa awali umeonyesha
bomu hilo ni la kutengenezwa kwa mkono
na mpaka sasa hajajulikana alietekeleza
shambulio hilo.
Kwenye sentensi nyingine pia amesema
hakuna aliepoteza maisha kwenye
shambulio hilo ambalo uchunguzi wa awali
umeshatoka, ila baadae itatoka taarifa
rasmi pale uchunguzi kamili
utakapokamilika.
 
Naona wadau badala ya kuwaombea kwa Mola ndugu zetu na kushauriana vipi tutawasadia kwa hali na mali wengine mnaleta masihara kwenye mambo muhimu....

Ila hii inatisha itabidi watu tuanze kuchunguzana na kulindana tukiwa popote kwenye mkusanyiko.

Kwa hili naona wenye biashara kubwa na mikusanyiko ya watu wangeweka CCTV kwa faida yao na wote.
 
Great thinking. Ukweli ndio huo mkuu. Lengo ni kuhamisha akili za watu kutoka Dodoma ikizingatiwa kuwa kesho watu walikuwa wanasubiri kwa hamu kumsikiliza Tundu Lissu.

Wamemuogopa bure Tundu Lissu,amesema ukweli na amekuwa huru.Nawaonea huruma Wazee wangu ambao wengi wao ni wabunge toka nikiwa darasa la pili miaka 40 iliyopita,leo wanakutana na vijana ambao wanataka ukweli na wanautafuta,changamoto ni kubwa sana.

Ninawasiwasi matukio haya yanaweza kuwafanya watoto wa wazazi waliofariki kwenye milipuko hii kuishtaki serikali kwa kutaka kujua ukweli,sijui kama itatuwia rahisi kuwanyima haki hiyo,na ni muda mfupi tu uajao wataka kujua hatima yao na madai ya kulipwa mabilioni kama fidia.

Tanzania yangu sijui inaenda wapi.
 
Mbona hii nchi si ya amani tena kama tulivyokuwa tunajigamba! mara utasikia arusha kesho mtwara na kesho kutwa utasikia zanzibar kulikoni jamani mbona kama haya matukio yanafanya kwa kupangwa na chama fulani?
 
Tunaanza kama mchezo ila ikiwa serious tutajuta
 
itabidi ukitaka kunywa kiroba ukibebe ukanywee chumbani na wife,haiyumkiniki hali si shwari tena.
 
Arusha hivi punde watu wamerusha bomu la mkono kweny bar maarufu inayoitwa Arusha Night Park au Matiko Bar iliyopo eneo la Mianzini inasemekana watu wawili wamepoteza maisha ila majeruhi ni wengi sana tukio hili ni ndani ya nusu saa iliyopita. Watu kibao walikuwa wanacheki mpira unaambiwa watu wamekatika mikono yaani balaa majeruh ni wengi mno........

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
HAYA MABOMU YANAYORINDIMA Arusha siku kwa siku ni ya kuitakia mema mji wa Atown?

Mtakumbuka mabomu 2010(ubunge Lema akashinda tu),mabomu kanisani watu wakafa,mabomu (udiwani Kessy akashinda tu) na leo tena hotelini/bar watu hawana miguu!!

Arusha kunani?
hilil bomu la jana, (mtk bar)
a)la kisiasa?
b)kiuchumi-kuharibiana biashara?
c)au ni la kiharamia?
 
HAYA MABOMU YANAYORINDIMA Arusha siku kwa siku ni ya kuitakia mema mji wa Atown?

Mtakumbuka mabomu 2010(ubunge Lema akashinda tu),mabomu kanisani watu wakafa,mabomu (udiwani Kessy akashinda tu) na leo tena hotelini/bar watu hawana miguu!!

Arusha kunani?
hilil bomu la jana, (mtk bar)
a)la kisiasa?
b)kiuchumi-kuharibiana biashara?
c)au ni la kiharamia?

Bomu ni la kisiasa kwa kujaribu kuchafua hali ya hewa baada ya kushindwa kuokoa viti vyote vitano ambavyo viliachwa wazi na Chadema na kurudi kwa Chadema tena.

Umeona Lukivi alivyotoa vitisho jana huko Dodoma kanisani kutisha kama serikali tatu zikipita jeshi litachukua nchi?
 
Back
Top Bottom