Mliofanikiwa kimaisha kwa kutumia kanuni ya 'Ubahili' mliwezaje, mbona mie nashindwa kabisa?

Mkuu nina ndugu yangu mmoja hivi kwa mfano, kwa bahati mbaya kila nikijaribu kumshika mkono mambo yanakuwa yanenda ndivyo sivyo. Biashara hazifanikiwa yaani kila kinachoguswa hakiendi. Nilidhani ni uzembe nikafanya alaysis nikagundua yapo mambo mengine huenda ni nje ya uwezo.
Usimuweke ndugu yako kusimamia biashara yako hautaweza kumcontorl na utagombana naye undugu utakufa bure ndugu ni WA kuweka mbali na Mali zako na vitega uchumi vyako labda kama uyo ndugu naye ni mchakarikaji Ila kama ni goigoi kaa mbali naye utalia na hutakiwa na la kumfanya
 
Shida haziishi Mkuu,

Mm ndo maana nilifurahi kuhamishiwa mkoani kikazi, Kituo changu cha kazi ni mkoa ambao Sina hata ndugu. Kama ni shida za ndugu na jamaa zote huwa najulishwa kwenye simu.

Zenye uzito huwa nasaidia, zisizo na uzito huwa nazipuuza.

Huwezi kumsaidia kila mtu, shida haziishi. Nilitumia miaka miwili tangu kuajiliwa kusaidia watu wa karibu. Kwasasa nasaidia ndugu wa damu na close friends tu. Tena kizuri ni waelewa wanajua Hali ni mgumu hata nikiwaambia Sina wanaelewa.

Kufanga kazi mbali na mkoa ambao ndugu na jamaa zako wanaishi ni nafuu zaidi kwa watu wenye mioyo ya huruma Kama ww.
 
Shida haziishi Mkuu,

Mm ndo maana nilifurahi kuhamishiwa mkoani kikazi, Kituo changu cha kazi ni mkoa ambao Sina hata ndugu. Kama ni shida za ndugu na jamaa zote huwa najulishwa kwenye simu.

Zenye uzito huwa nasaidia, zisizo na uzito huwa nazipuuza.

Huwezi kumsaidia kila mtu, shida haziishi. Nilitumia miaka miwili tangu kuajiliwa kusaidia watu wa karibu. Kwasasa nasaidia ndugu wa damu na close friends tu. Tena kizuri ni waelewa wanajua Hali ni mgumu hata nikiwaambia Sina wanaelewa.

Kufanga kazi mbali na mkoa ambao ndugu na jamaa zako wanaishi ni nafuu zaidi kwa watu wenye mioyo ya huruma Kama ww.
Mkuu nimekupata vema. Hapo inabidi usipende hata kujiunga kwenye magroup ya WhatsApp ya Familia/Ukoo. Maana ukiwa huko ni kama upo tu home bado. Kila wiki itakuja taarifa ya michango/matatizo. Na inakuwa haiishi. Noma sana Mkuu.
 
Mara nyingi wema wako hukuponza, ukienda kwa mzungu bila taarifa hata kama anakula wewe utaendelea kusoma gazeti mpaka amalize kula. Hata kama ukitoa taarifa kama budget yake hairuhusu anakunambia usiende. Huo ndio ubahili wenyewe, ukiufuata vizuri utakuta una akiba nzuri kwa mwezi. Ila usiache kulipa fadhila kwa waliokusaidia, kwa kadiri ya uwezo wako na mahesabu makali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Utajiri au mafanikio hayqji kwa kuwa bahiri mkuu,ni Nia na kuamua pasipo kugeuka nyuma au kujiulizauliza .uamie haswa.fanya kazi kwa juhudi na usisahau kutumia akili kwa kila Jambo,uthubutu ni muhimu pasipo hofu Wala woga. kanuni ndo hiyo
 
Mungu si Athumani, maana amekuwa akishusha thawabu zake kwa muda wa takribani miaka mitano sasa tangu nilipoanza kupataa namna ya kujiingizia kipato changu na kumudu gharama za kuishi. Kwakweli niwe muwazi kuwa maisha siyo mteremko sana na wala sipati pesa nyingi sana lakini pesa nazopata zinawezesha kugharamia mahitaji yote ya muhimu na kubakiza vichenji vya hapa na pale. Sasa changamoto ni kuwa, kwa muda wa miaka mitano sasa nikijifanyia tathmini sijafanikiwa kumiliki kitu chochote kama asset, siyo nyumba wala ardhi. Yaani chenji zote nazopata zinaishia kusaidia ndugu na jamaa.

Ukweli ni kuwa, nimetokea familia maskini na watu wengi kwenye circle yangu bado wana maisha magumu sana. Sasa kwakweli nakuwa na moyo wa huruma sana pale mtu anapokuja na kulia shida zake halafu nimnyime pesa kwa kisingizio kuwa nafanya savings. Huwa navuta kumbukumbu wakati ule nilipokuwa sina kitu na maisha yalivyokuwa magumu kisha napata huruma sana. Kwahiyo mtu akija, awe ndugu ama rafiki endapo atasema ana shida flani huwa naichukuwa kama shida yangu na kumsaidia. Huwa nashindwa kabisa kuwanyima hawa jamaa zangu. Kuna wakati nilisema labda nijifanye bahili na niwe na moyo mgumu lakini badae nikashindwa kabisa maana moyo ulikuwa unaniuma sana na nikawa kama nakuwa guilty kwakushindwa kumsaidia jamaa yangu. Huwa najiuliza hivi huyu ndugu akifa na ameomba pesa labda ya matibabu au chakula si nitaenda masibani na kumzika, kisha nitasema ni ndugu yangu wa karibu na nilimpenda sana? Sasa iweje nishindwe kumsaidia sasa akiwa hai?.

Hii tabia imenifanya nishindwe kufanya savings kabisa ili kujiendeleza kiuchumi na kutanuka zaidi. Yaani unakuta kwa mwezi nina requests za ndugu na jamaa zipo pending zakutosha. Unakuta nyingine nazi-hold hata miezi 4 kabisa kutokana na kuelemewa. Ikifika mwisho wa mwezi naanza ku-clear moja baada ya nyingine kama mtu anavyolipa mishahara watu wake. Nikipiga hesa kiasi nachosaidia watu kwa mwaka mpaka huwa najishangaa nimewezaje kutoa kiasi chote hicho. Lakini pamoja na hayo, kwakweli Mungu hajawahi kunipungukia kabisa. Sijawahi kukosa kabisa wala kupungukiwa. Ila ndio hivyo sina savings za kusema wala sima mali nayomiliki. Sasa swali langu, wale mliofanikiwa kutoboa kwa kuwa 'mabahili' mnawezaje kumudu hisia zenu pale jamaa zenu wanapoomba msaada kwenu na kuamua kuwakazia?
Jaribu kujiweka kwenye hiyo orodha ya kuwasaidia wengine, kila mwezi jilipe kiasi fulani, ambacho hukigusi mwezi hadi mwezi na itakapofika baada ya mwaka, angalia umekusanya kiasi gani na kinaweza kununua au kuwekeza kwenye nini.
Kwa Tz matatizo na umasikini hauishi, usipokuwa muangalifu utakuja juta baadae.
 
Mara nyingi wema wako hukuponza, ukienda kwa mzungu bila taarifa hata kama anakula wewe utaendelea kusoma gazeti mpaka amalize kula. Hata kama ukitoa taarifa kama budget yake hairuhusu anakunambia usiende. Huo ndio ubahili wenyewe, ukiufuata vizuri utakuta una akiba nzuri kwa mwezi. Ila usiache kulipa fadhila kwa waliokusaidia, kwa kadiri ya uwezo wako na mahesabu makali.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapo kwene kulipa fadhila mkuu ndio shughuli haswa. Maana sie watoto wa maskini unakuta tumesaidiwa na utitiri wa watu. Sasa hapo kila mmoja mpaka umlipe fadhila ndio unajikuta kila mwezi unatatua shida za ukoo. Japo ni jambo la msingi sana kama unavyosema. Ila kama umezaliwa ushuani wala unakuwa hufahamiki na wana ukoo kiviile, maana wanakuwa wanakusikia tu juu juu. Shida akina sie wa vumbini, unakuta umesaidiwa na kila mtu yaani. Hapo familia zao wanakutegemea pia ulipe hiyo fadhila.
 
Zingatia yafuatayo: (Naongea kwa uzoefu na majuto, Trust me I know)

1. Kuwa na Malengo yako binafsi na yaandike mahali yaani uwe na malengo ya kwamba unataka kutimiza nini ndani ya miezi 6 au Mwaka. (Hakikisha hakuna mtu yeyote anajua hili even your wife)

2. Marufuku mtu yeyote kujua kipato chako(kwenye hili tumia 'nguvu' ya ziada kuficha)

3. Wazazi waliokuzaa wape kipaumbele nambari moja katika kuwasaidia. (No limits on this)

4. Misaada ya aina yeyote kwa wengine tofauti na wazazi I mean hata ndugu wa kuzaliwa hakikisha ni lazima na iwe 'Life Threatening' sio unamsaidia mtu fedha ya Vocha, really!!? Au eti braza nimeishiwa ninunulie Bia au King'amuzi kimeisha, Aisee mimi utasubiri sana.

5. Misaada mengine kama Malipo ya Ada, Fine au Manunuzi ya Dawa. Fanya kulipia wewe kisha watumie Risiti. Usimuamini mti yeyote kwenye Fedha ambayo ni jasho lako... Pesa ina ushetani wa ajabu sana.

6. Usipende wageni/ kumkaribisha kila mtu nyumbani kwako. Macho ya watu/ ndugu ya uchawi sana. In-fact kuwa makini na wageni wako na hasa ndugu wa karibu ukiweza muwe mnakutana nje na nyumbani. (Hili ni gumu lakini ni muhimu na lina faida kubwa sana)

7. Na 8. Ntaendelea...
 
Kama unafanyia kazi karibu na ndugu au ukoo wako hama nenda mikoa ya mbali na usi disclose/usitoe taarifa zako za kipato kwa ndugu maana ndg wengine hawajishughurishi akipata shida kidogo kwa furani
wakati ni sasa tumia kipato chako vizuri
Watu wa kuwasaidia ni wazazi wako tu hao wengine wapambane na khari zao binadamu hawana wema haohao unaowasaidia watakuja kukucheka
kiswahili ni lugha ya taifa...khaaaa......
 
Zingatia yafuatayo: (Naongea kwa uzoefu na majuto, Trust me I know)

1. Kuwa na Malengo yako binafsi na yaandike mahali yaani uwe na malengo ya kwamba unataka kutimiza nini ndani ya miezi 6 au Mwaka. (Hakikisha hakuna mtu yeyote anajua hili even your wife)

2. Marufuku mtu yeyote kujua kipato chako(kwenye hili tumia 'nguvu' ya ziada kuficha)

3. Wazazi waliokuzaa wape kipaumbele nambari moja katika kuwasaidia. (No limits on this)

4. Misaada ya aina yeyote kwa wengine tofauti na wazazi I mean hata ndugu wa kuzaliwa hakikisha ni lazima na iwe 'Life Threatening' sio unamsaidia mtu fedha ya Vocha, really!!? Au eti braza nimeishiwa ninunulie Bia au King'amuzi kimeisha, Aisee mimi utasubiri sana.

5. Misaada mengine kama Malipo ya Ada, Fine au Manunuzi ya Dawa. Fanya kulipia wewe kisha watumie Risiti. Usimuamini mti yeyote kwenye Fedha ambayo ni jasho lako... Pesa ina ushetani wa ajabu sana.

6. Usipende wageni/ kumkaribisha kila mtu nyumbani kwako. Macho ya watu/ ndugu ya uchawi sana. In-fact kuwa makini na wageni wako na hasa ndugu wa karibu ukiweza muwe mnakutana nje na nyumbani. (Hili ni gumu lakini ni muhimu na lina faida kubwa sana)

7. Na 8. Ntaendelea...
Asante sana Mkuu. Tunasubiri muendelezo.
 
Kama unafanyia kazi karibu na ndugu au ukoo wako hama nenda mikoa ya mbali na usi disclose/usitoe taarifa zako za kipato kwa ndugu maana ndg wengine hawajishughurishi akipata shida kidogo kwa furani
wakati ni sasa tumia kipato chako vizuri
Watu wa kuwasaidia ni wazazi wako tu hao wengine wapambane na khari zao binadamu hawana wema haohao unaowasaidia watakuja kukucheka
Mke atatoa na kukuibia juu.
 
Kama ukikataa nafsi yako INAKUSUTA mimi nakushauri endelea tu kuwapa , inawezekana unapata kwa sababu unatoa
 
Kama ukikataa nafsi yako INAKUSUTA mimi nakushauri endelea tu kuwapa , inawezekana unapata kwa sababu unatoa
Changamoto yake ni kwa nitaendelea kuwa 'an average person with regards to finances'. Yaani Mkuu inaonesha watoaji wengi huishia kuwa maskini ama watu wa kawaida sana kiuchumi huko mbeleni. Ineonesha ili ujijenge kiuchumi formula namba moja dhibiti milango ya kutolea fedha. Unapodhibiti milango ya kutoa pesa ni pamoja na hii habari ya kutoa pesa kwa watu kwa lugha ya kusaidia. Ndio wajuvi wanavyodai hivyo. Hasa waliofanikiwa tayari.. Hapo sasa inabidi kuchagua kimoja. Either ukubali kuwa mtoaji kwa watu na uishie kuwa mtu wa kawaida ama ukubali kuitwa bahili na majina mengine mabaya kama vile mchoyo ili utoboe. Haya maisha mkuu kiufupi ni complex sana.
 
Back
Top Bottom