Mliofanikiwa kimaisha kwa kutumia kanuni ya 'Ubahili' mliwezaje, mbona mie nashindwa kabisa?

FAJES

JF-Expert Member
Oct 29, 2017
714
628
Mungu si Athumani, maana amekuwa akishusha thawabu zake kwa muda wa takribani miaka mitano sasa tangu nilipoanza kupataa namna ya kujiingizia kipato changu na kumudu gharama za kuishi. Kwakweli niwe muwazi kuwa maisha siyo mteremko sana na wala sipati pesa nyingi sana lakini pesa nazopata zinawezesha kugharamia mahitaji yote ya muhimu na kubakiza vichenji vya hapa na pale. Sasa changamoto ni kuwa, kwa muda wa miaka mitano sasa nikijifanyia tathmini sijafanikiwa kumiliki kitu chochote kama asset, siyo nyumba wala ardhi. Yaani chenji zote nazopata zinaishia kusaidia ndugu na jamaa.

Ukweli ni kuwa, nimetokea familia maskini na watu wengi kwenye circle yangu bado wana maisha magumu sana. Sasa kwakweli nakuwa na moyo wa huruma sana pale mtu anapokuja na kulia shida zake halafu nimnyime pesa kwa kisingizio kuwa nafanya savings. Huwa navuta kumbukumbu wakati ule nilipokuwa sina kitu na maisha yalivyokuwa magumu kisha napata huruma sana. Kwahiyo mtu akija, awe ndugu ama rafiki endapo atasema ana shida flani huwa naichukuwa kama shida yangu na kumsaidia. Huwa nashindwa kabisa kuwanyima hawa jamaa zangu. Kuna wakati nilisema labda nijifanye bahili na niwe na moyo mgumu lakini badae nikashindwa kabisa maana moyo ulikuwa unaniuma sana na nikawa kama nakuwa guilty kwakushindwa kumsaidia jamaa yangu. Huwa najiuliza hivi huyu ndugu akifa na ameomba pesa labda ya matibabu au chakula si nitaenda masibani na kumzika, kisha nitasema ni ndugu yangu wa karibu na nilimpenda sana? Sasa iweje nishindwe kumsaidia sasa akiwa hai?.

Hii tabia imenifanya nishindwe kufanya savings kabisa ili kujiendeleza kiuchumi na kutanuka zaidi. Yaani unakuta kwa mwezi nina requests za ndugu na jamaa zipo pending zakutosha. Unakuta nyingine nazi-hold hata miezi 4 kabisa kutokana na kuelemewa. Ikifika mwisho wa mwezi naanza ku-clear moja baada ya nyingine kama mtu anavyolipa mishahara watu wake. Nikipiga hesa kiasi nachosaidia watu kwa mwaka mpaka huwa najishangaa nimewezaje kutoa kiasi chote hicho. Lakini pamoja na hayo, kwakweli Mungu hajawahi kunipungukia kabisa. Sijawahi kukosa kabisa wala kupungukiwa. Ila ndio hivyo sina savings za kusema wala sima mali nayomiliki. Sasa swali langu, wale mliofanikiwa kutoboa kwa kuwa 'mabahili' mnawezaje kumudu hisia zenu pale jamaa zenu wanapoomba msaada kwenu na kuamua kuwakazia?
 
Mbona profile picture hako Ina kaulimbiu nzuri ya "be your own boss" unakwama wapi? Msaada unatakiwa kutokana na faida ya biashara yako na mshahara.
Mkuu, jamaa yako wa karibu sana anakufuata na kusema mkewe mgonjwa ama mama mzazi. Unawezaje kumnyima kwa kisingizio kuwa unafanya saving wakati akifariki utaenda kumzika? Huo ujasiri mwenzangu unawezaje? Naomba unije mbinu..
 
๐Š๐ฐ๐ž๐ฅ๐ข ๐ก๐ฎ๐ฐ๐š ๐ง๐ข ๐ง๐ ๐ฎ๐ฆ๐ฎ, ๐ข๐ฅ๐š ๐ง๐ข๐ง๐š๐œ๐ก๐จ ๐ค๐ข๐š๐ฆ๐ข๐ง๐ข ๐ง๐ข ๐ก๐ข๐ค๐ข ๐ค๐ฎ๐ง๐š ๐ฆ๐ฐ๐š๐ง๐š๐Ÿ๐š๐ฅ๐ฌ๐š๐Ÿ๐š ๐ฆ๐ฆ๐จ๐ฃ๐š ๐š๐ฅ๐ข๐ฐ๐š๐ก๐ข ๐ค๐ฎ๐ฌ๐ž๐ฆ๐š ๐ก๐ข๐ฏ๐ข.
๐‘ด๐’–๐’๐’ˆ๐’– ๐’‚๐’Œ๐’Š๐’๐’Š๐’‘๐’‚๐’•๐’Š๐’‚ ๐’“๐’Š๐’…๐’‰๐’Š๐’Œ๐’Š ๐’š๐’‚ ๐’๐’‚๐’Œ๐’Š ๐’Ž๐’๐’‹๐’‚ ๐’๐’‚๐’‹๐’–๐’˜๐’‚ ๐’Œ๐’‚๐’ƒ๐’Š๐’”๐’‚ ๐’‚๐’Ž๐’†๐’๐’Š๐’‘๐’‚ ๐’‰๐’†๐’“๐’‚ ๐’š๐’‚ ๐’„๐’‰๐’‚๐’Œ๐’–๐’๐’‚ ๐’๐’‚๐’Œ๐’Š๐’๐’Š ๐‘ด๐’–๐’๐’ˆ๐’– ๐’‚๐’Œ๐’Š๐’๐’Š๐’‘๐’‚๐’•๐’Š๐’‚ ๐’“๐’Š๐’…๐’‰๐’Š๐’Œ๐’Š ๐’š๐’‚ ๐’๐’‚๐’Œ๐’Š ๐’•๐’‚๐’๐’ ๐’๐’‚๐’‹๐’–๐’˜๐’‚ ๐’‚๐’Ž๐’†๐’๐’Š๐’‘๐’‚๐’•๐’Š๐’‚ ๐’‘๐’†๐’”๐’‚ ๐’š๐’‚ ๐’Œ๐’–๐’‡๐’‚๐’๐’š๐’Š๐’‚ ๐’Ž๐’‚๐’†๐’๐’…๐’†๐’๐’†๐’
๐•ž๐•ก๐•’๐•œ๐•’ ๐•™๐•’๐•ก๐•  ๐•ฆ๐•Ÿ๐•’๐•จ๐•–๐•ซ๐•’ ๐•œ๐•ฆ๐•”๐•™๐•’๐•Ÿ๐•˜๐•’๐•Ÿ๐•ฆ๐•’ ๐•ž๐•จ๐•–๐•Ÿ๐•ช๐•–๐•จ๐•–
 
Kanuni kuu ... ni "frugality "

Kata matumizi yote yasiyokuwa ya muhimu..

Mfano unakuta mtu una decoder tatu nsani ya nyumba moja zote unalipia bundles /month

Unaunga unga mabando una surf net instagram unaangalia ujinga ujinga " bundle kwa mwezi ukipiga hesabu linafika hdai Tshs.50,000 +

Kiufupi ni kuacha tabia ya matumizi mabaya ya fedha kununua vitu usivyovihitaji au visivyo na umuhimu.. tofauti na hapo utajikuta uanjitumikisha/kutumikishwa kutafuta hela ambayo thamani yake inaishia kwenye upuuzi.

Ili uweze kusave inabidi kila kiasi unachopata kinaenda kwenye uwekezaji , kufanyia biashara ili pesa izae
 
Kama unafanyia kazi karibu na ndugu au ukoo wako hama nenda mikoa ya mbali na usi disclose/usitoe taarifa zako za kipato kwa ndugu maana ndg wengine hawajishughurishi akipata shida kidogo kwa furani
wakati ni sasa tumia kipato chako vizuri
Watu wa kuwasaidia ni wazazi wako tu hao wengine wapambane na khari zao binadamu hawana wema haohao unaowasaidia watakuja kukucheka
 
Msaidie kwa kumpatia kazi, kama una shamba, aende akasimamie vibarua n.k
Mkuu nina ndugu yangu mmoja hivi kwa mfano, kwa bahati mbaya kila nikijaribu kumshika mkono mambo yanakuwa yanenda ndivyo sivyo. Biashara hazifanikiwa yaani kila kinachoguswa hakiendi. Nilidhani ni uzembe nikafanya alaysis nikagundua yapo mambo mengine huenda ni nje ya uwezo.
 
Mkuu nina ndugu yangu mmoja hivi kwa mfano, kwa bahati mbaya kila nikijaribu kumshika mkono mambo yanakuwa yanenda ndivyo sivyo. Biashara hazifanikiwa yaani kila kinachoguswa hakiendi. Nilidhani ni uzembe nikafanya alaysis nikagundua yapo mambo mengine huenda ni nje ya uwezo.
Mfungulie biashara ya mitumba, akishindwa piga chini
 
Mungu si Athumani, maan amekuwa akishusha thawabu zake kwa muda wa takribani miaka mitano asa tangu nilipoanza kupataa namna ya kujiingizia kipato changu na kumudu gharama za kuishi. Kwakweli niwe muwazi kuwa maisha siyo mteremko sana na wala sipati pesa nyingi sana lakini pesa nazopata zinawezesha kugharamia mahitaji yote ya muhimu na kubakiza vichenji vya hapa na pale. Sasa changamoto ni kuwa, kwa muda wa miaka mitano sasa nikijifanyia tathmini sijafanikiwa kumiliki kitu chochote kama asset, siyo nyumba wala ardhi. Yaani chenji zote nazopata zinaishia kusaidia ndugu na jamaa.

Ukweli ni kuwa, nimetokea familia maskini na watu wengi kwenye circle yangu bado wana maisha magumu sana. Sasa kwakweli nakuwa na moyo wa huruma sana pale mtu anapokuja na kulia shida zake halafu nimnyime pesa kwa kisingizio kuwa nafanya savings. Huwa navuta kumbukumbu wakati ule nilipokuwa sina kitu na maisha yalivyokuwa magumu kisha napata huruma sana. Kwahiyo mtu akija, awe ndugu ama rafiki endapo atasema ana shida flani huwa naichukuwa kama shida yangu na kumsaidia. Huwa nashindwa kabisa kuwanyima hawa jamaa zangu. Kuna wakati nilisema labda nijifanye bahili na niwe na moyo mgumu lakini badae nikashindwa kabisa maana moyo ulikuwa unaniuma sana na nikawa kama nakuwa guilty kwakushindwa kumsaidia jamaa yangu. Huwa najiuliza hivi huyu ndugu akifa na ameomba pesa labda ya matibabu au chakula si nitaenda masibani na kumzika, kisha nitasema ni ndugu yangu wa karibu na nilimpenda sana? Sasa iweje nishindwe kumsaidia sasa akiwa hai?.

Hii tabia imenifanya nishindwe kufanya savings kabisa ili kujiendeleza kiuchumi na kutanuka zaidi. Yaani unakuta kwa mwezi nina requests za ndugu na jamaa zipo pending zakutosha. Unakuta nyingine nazi-hold hata miezi 4 kabisa kutokana na kuelemewa. Ikifika mwisho wa mwezi naanza ku-clear moja baada ya nyingine kama mtu anavyolipa mishahara watu wake. Nikipiga hesa kiasi nachosaidia watuh kwa mwaka mpaka huwa najishangaa nimewezaje kutoa kiasi chote hicho. Lakini pamoja na hayo, kwakweli Mungu hajawahi kunipungukia kabisa. Sijawahi kukosa kabisa wala kupungukiwa. Ila ndio hivyo sina savings za kusema wala sima mali nayomiliki. Sasa swali langu, wale mliofanikiwa kutoboa kwa kuwa 'mabahili' mnawezaje kumudu hisia zenu pale jamaa zenu wanapoomba msaada kwenu na kuamua kuwakazia?

...................................................................
MOODS: Naomba isome kwenye heading kama 'ubahi(li) badala ya Ubahi(ri)'. Hili janga la l na r sijui litaisha lini tu. Bibi FaizaFox akipita hapa atanipa mikwaju ya maana. Nitaambiwa huko shule nilienda kusomea ujinga? Ha ha haaa.
Huwezi kuwanyima ndugu zako wenye shida wasaidie kwa tekniki sana.

mfano ndugu kakuomba 30000 mwambie sina hiyo pesa hapa nina 10000 tu sijui kama itakusaidia hii itamfanya aone unayo nia ila pesa huna,hapo utakuwa umesave 20000.

Kiukweli huwezi kutatua shida zote za ndugu zako hivyo usipoteze muda kuumia saana pale wanapotangaza shida zao kwako.

Shida unapopata mtu wa kuibeba basi ndo unaiona ni kubwa ila kama haujapata mtu wa kukubebea shida yako unakuwa unaibeba mwenyewe basi shida hiyo utaiona kawaida tu na maisha yataendelea.

Ndugu yoyote akiona kama kuna mtu wa kumpiga kirungu basi ataikuza shida,ila kama hana ataipotezea ama ataivumilia tu.


Tuwasaidie ndugu ila kama una bajeti yako ya laki moja uanzishe kamradi alafu jdugu anapiga simu umkopeshe pesa akatoe mchango wa harusi mwambie hauna pesa,huwezi kutoa pesa kwa mwmbo ya kipuuzi kama hayo.

Mambo wmbayo mtu wnayapanga yatokee siku filulani sasa kwa nini umchangie kama harusi,birthday why uchangie upuuzi kama huu wakuu ?

Hapana aisee tuchangiane kwenye magonjwa na dharura zinngine za msingi
 
Back
Top Bottom